Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Jumanne ktk comment yangu #136,087 nilimwambia hiki kitu Darmian

Darmian,

Ubingwa kumpa Liverpool bado mapema sana, japo ndio timu pekee katika kubwa walio serious zaidi. Mechi mbili zijazo kwa Liverpool zinaweza kuwapandisha morali au kuwashusha. Mechi ijayo wataenda Villa Park kucheza na Aston Villa hawa ni sawa na farasi mweusi asiye angaliwa na wengi kwa hiyo hawachezi kwa presha ila kiukweli wapo moto sana, wamecheza mechi nne msimu huu wameshinda zote ya mwisho walimfunga Wolves kwake 3 bila.

Baada ya Aston Villa wataenda mji wa Walton pale pale Liverpool kucheza na Everton, kwa form ya sasa ya Everton wakishinda pale Goodison Park basi Liverpool confidence yao inaweza kuwa juu mno ktk mbio za ubingwa ila wakianza kwa kufungwa inaweza kubadili hali yao ya kujiamini pia.
Big Up kwa kuliona hili mkuu..
 
Mr Drmian pole sana Chifu kwa kichapo cha leo. Ed Woodward mna mpango gani naye pale Man U? maana naona yuko kimaslahi tu wala haguswi kabisa na hali ambayo timu yenu inapitia Chifu.
Ed woodward kosa lake ni kukubali kuwa na benchi la ufundi lenye uwezo mdogo..apart from that sioni shida yake kubwa..Kama hela zishatoka sana
 
Ed woodward kosa lake ni kukubali kuwa na benchi la ufundi lenye uwezo mdogo..apart from that sioni shida yake kubwa..Kama hela zishatoka sana
Sawa sawa Mkuu, so unadhani hili tatizo halionagi mda mrefu tu? na kwanini ashindwe kutumia plan B kama plan A ilishafeli na inaendelea kufeli hadi hivi sasa?
 
chilubi,

Unakosa kutizima taswira pana zaidi ya uhalisia, timu nzuri hujengwa kwa zaidi ya matumizi ya pesa nyingi, pesa ni moja ya variable tu ktk the whole equation. Unamfahamu mtu mwenye majukumu ya kuajiri kocha wa Manchester United? Mtu mwenye majukumu wa kuajiri watafuta vipaji wa timu? Hujakosea ubashiri wako, ni Ed Woodward. Mpaka sasa tumeshaajiri makocha zaidi ya 5 chini ya Ed na wawili ni manguli wameshinda mataji ya kila aina kwa ujumla wao wana mataji zaidi ya 50 (Jose & LVG), bado tu unaamini ni coaaching area ndio pana upungufu? Ni kweli Ole ni average ila nani amemuajiri Ole?

Kuweka kumbu kumbu sawa, sisi Manchester United ndio tumetumia pesa nyingi sana kwa miaka 7 toka Ed awe bosi mkuu kuliko timu yoyote pale Uingereza tumewazidi mpaka Manchester City. Timu nzuri hujengwa na combination ya smart talents from football executive to recruitment teams hata uwe na pesa kama za Jeff Bezos usipokuwa na watu smart hasa hasa wale ma-chief strategist ni kazi bure. Hujiulizi kwa nini timu kama Liverpool wanafanya vizuri ila hawatumii kuliko sisi? Kuna watu behind the scenes wanafanya kazi kile tunachoona sisi mashabiki uwanjani ni product ya mwisho kabisa baada ya kuwa na smart chief stategist (football executive) anaajiri watu sahihi ktk kila idara kuanzia coaching staffs, recruitment staffs & negotiators. Hivyo vyote vikiwa sawa hata uwanjani panakuwa sawa. Fanya simple observation Manchester United chini ya Peter Kenyon (1997 - 2002, huyu ndiye aliyeijenga Chelsea pia, 2003 - 2009) Vs David Gill (2003 - 2013) Vs Ed Woodward (2013 - up to date).

Ni zaidi ya pesa ili uweze kujenga timu nzuri, kitu kikubwa kuliko vyote unahitaji kuwa na very smart football executive hao wengine wote wanaajiriwa na huyu mtu. Ukiwa na huyu mtu kilaza hata ulete malaika awe kocha mkuu timu itafanya hovyo tu maana hapatakuwa na technical coordination nzuri.
 
Klopp,,, pep na arteta nani mwenye cv kubwa? Toka mshinde masinia na birika mnamaneno nyie daaa
Mngeshinda nyie , kwan CV ndio inacheza ,hao wanafunguka wameshaamini ligi ni zao. Kumbe watu wamebadilika

Siumeona Leo umekuka 6 hapo hapo kwako
 
Back
Top Bottom