Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

★Shida wanaangalia kwenye makosa tu ndio wnasema kuna jamaa mwingine ety kasema Jana Dalot wako alikuwa hakimbii kazidiwa mbio na MaTa★
Mimi naamini Diogo Dalot akicheza right wing anafanya vizuri kuliko kwenye defence.

After all anatumia miguu yote left na right hivyo anaweza kufunga kwenye near post na far post.
 
Tunajua hilo..ila yeye ndo anayetokea kulia na amefanya vizuri kwa kiasi chake..na tusiposajili am sure yeye ndo ataendelea kuwa first choice kwenye hilo eneo kwenye mechi nyingi.
Winger anatakiwa awe na speed,aweze kumiliki mpira,kupiga chenga kutengeneza nafasi na kufunga katika vyote Greenwood ni mzuri kwenye kufunga magoli Tu mengi ya United yanatokea upande wa kushoto

Kocha unatakiwa kumchezesha mchezaji kutokana na strength zake
 
Winger anatakiwa awe na speed,aweze kumiliki mpira,kupiga chenga kutengeneza nafasi na kufunga katika vyote Greenwood ni mzuri kwenye kufunga magoli Tu mengi ya United yanatokea upande wa kushoto

Kocha unatakiwa kumchezesha mchezaji kutokana na strength zake
Sasa si ndo maana tunasema tunamtaka mtu kama Sancho ndo aje acheze hilo eneo..otherwise kwa kikosi tulichonacho Greenwood ataendelea kutokea hukohuko kulia kama first choice
 
Mechi hizo OLe akipanga hiki kikosi asubuh tuu tunaongoza hilo group.

De gea

AWB. Maguire. Upemecano. Telles.

Bruno Matic Vdb

Sancho. Cavan Martial


Subs: Henderson, Baily, Shaw, Pogba, Fred, Rashford, Greenwood

NB: niko naota.
Hakika mkuu...
 
Arsenal Tuna hati miliki ya FA , kwaio tunabeba tena...... pia tunabeba hii carabao.... Ligi tunamuachia Liverpool... Uefa watabeba wababe kama Bayern/Madrid.......

NINYI CHELSEA, MAN CITY NA MAN U MUENDELEE KUJIANDAA NA MSIMU UJAO WA 2021/2022.


#COYG
#COYG
 
UEFA

1601618585952.png
 
★Jambo jema kama itafanikiwa
SOMA hiyo. Jadon Sancho anaamini atakuwa mchezaji wa Manchester United kabla ya dirisha kufungwa Jumatatu.

Winga huyo Mwingereza, Sancho mwenye umri wa miaka 20, amewataka washauri wake wa mambo ya uhamisho “kuondoa vikwazo vyote” ili kukamilisha dili lake la kutua Old Trafford akitokea Borussia Dortmund.

Sancho hakujumuishwa kwenye kikosi cha Dortmund katika mchezo wa Kombe la Ujerumani dhidi ya Bayern Munich juzi Jumatano.

Kocha wa Man United, Ole Gunnar Solskjaer anazidi kupata uhakika wa kunasa huduma ya mchezaji huyo chaguo lake kwenye dirisha hili kabla halijafungwa.

Ripoti za kutoka Ujerumani, Dortmund wameshakubali kumpoteza supastaa wao huyo, licha ya kudai hadharani kwamba wanaamini atabaki.



Kuna mtu wa karibu kabisa na Sancho, alisema: “Anataka dili hili kukamilika.

“Amemwambia wakala wake na washauri wake kufanya kila wanaloweza kuhakikisha jambo hilo linakamilika.

“Wanapambana kwa ajili yake aondoke.”

Dortmund imeripotiwa kwamba inataka walau Pauni 80 milioni kwanza na kisha nyongeza nyingine.

Chanzo cha karibu kabisa za kuhusu mchakato wa dili hilo la uhamisho lililochukua muda mrefu kwenye dirisha hili la majira ya kiangazi, kinafichua kwamba Sancho atawagha-rimu Man United Pauni 95 milioni, tofauti na kiwango cha Pauni 108 milioni ambacho Dortmund inataka kulipwa.

Wasimamizi wa mambo hayo ya uhamisho wamekuwa kwenye mazungumzo ya kukamilisha dili hiyo kimyakimya ili kuhakikisha linakamilika kabla ya dirisha kufungwa Jumatatu ijayo.

Chanzo hicho kilifichua: “Kuna jambo dogo sana linachelewesha...ni suala la nani aanza kwanza.

“Man United itaongeza ofa yao au Dortmund itakubali ofa ya pesa ya chini? Manchester United wao inafikiria kupeleka ofa ya mwisho kabisa kwa ajili ya mchezaji huyo hadi kufikia jana Jumatano na inaamini itavuka vikwazo vyote na kufanya mambo kukamilika haraka.”

Kuwasili kwa Sancho huko Old Trafford kutafungua milango ya winga, Daniel James kwenda kujiunga na Leeds United na jambo hilo linaweza kuwa kwa mkopo wa msimu mzima au dili la jumla kama wababe hao wanaonolewa na Marcelo Bielsa watakuwa na mkwanja wa kunasa huduma yake jumla



Sent from my itel S31 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom