jose mourinho pamoja na jopo la scouting nahisi walitufanyia uhuni kwenye dili la usajili linalomuhusu dalot, kwa ufupi sielewi iliwezekana vipi klabu kubwa kama man utd kukubali kulipa takribani paundi millioni 20 kwa mchezaji aliyecheza takribani mechi 8 tu za mashindano (labda waliona muelekeo mwema kwake kupitia video za play station)
huu ni msimu wa tatu tokea asajiliwe lakini bado ameendelea kustruggle na kibaya zaidi ameingia kwenye kundi la wachezaji wenye takwimu mbovu za kiafya (akiungana na jones, tuanzebe na bailly)
performance yake anayoionyesha uwanjani kadri anapopewa nafasi haishawishi ya kwamba siku moja atakuwa ni fullback mwenye quality zote tunazozihitaji ila umri wake (ana miaka 21) unashawishi ya kwamba siku moja anaweza kuwa mchezaji mahiri kama yule tuliyemshuhudia mechi ya PSG.
si jambo rahisi kurudisha gharama tulizotumia kumsajili kutokana na kiwango chake, fitness na pia kuzuka kwa janga la corona kumeliathiri kwa namna fulani soko la fedha kwa baadhi ya timu,
endapo klabu itaamua kumuweka sokoni kwa jumla basi sitochukia,
endapo klabu itaamua kumtoa kwa mkopo wa muda mrefu pia sitochukia (nadhani huu utakuwa ni uamuzi bora zaidi kwa sababu huenda timu atakayokwenda itamfanya apande thamani yake kuliko kuendelea kukaa benchi).