Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Nafikiri tumpe OLE MUDA..
Watu wanaweza kumlaumu kwa 7bu ya kuchelewa kufanya sub ila kwny benchi kuna watu gani wa kubadilisha matokeo!?

Kikosi chetu ni kibovu lakini pia kocha nae kuna vitu inabidi aImprove kwny mipango yake..

Kimsingi me naona tumletee wachezaji anaowataka alaf tuone atafanyaje..Akizingua tumfukuze.
 
Acha kujifariji mkuu. Hakuna bahati kwenye soka . Ukishindwa kutumia nafasi unazopata lazima utaadhibiwa tu

Umesema kabisa hapo kuwa timu imetengeza nafasi nyingi ila mpira uligoma kuingia wavuni , maana yake ni kuwa Man u weren't clinical. Sevilla wao 5 shots 3 on target 2 goals. They took their chances .

Man Hakuna natural number 9 pale mtu ambae ni muuaji type ya Aguero, Lewandowski Cavani .,martial sio NATURAL number 9

Katika game hizi 2 copenhagen na sevilla Man wamepiga zaidi ya shots 30 lakini magoli mawili yaliyopatikana ni kwa njia ya penat . Nafasi zinatengenezwa kweli ila umaliziaji hafifu

Enewei body language ya wachezaji wenyewe ilikua inaonesha kuwa nafasi ya 3 inawatosha na msimu ujao watacheza UCL hivo waliona hawana presha sana

Hivi kumbe na nyie mnajuaga kuwa bila penalty hamna matokeo yoyote ya kueleweka
 
Adjustments.jpg
 
CB: Magalhães (£18)
DM: Neves (£45) // Ndidi (£40)
RW: Sancho (£108)
ST: Mitrović (£18)

Magalhães, huyu ni kama Wan-Bissaka wa katikati. Akija United ataimarisha ukuta wetu vizuri sana.

Neves // Ndidi. Hawa ni aina ya wachezaji muhimu sana katika eneo la kati, ukizingatia Matić umri umeenda tukimpata mmoja wapo kati ya hao kiungo chetu kitakuwa imara sana.

Sancho. Tumeteseka miaka mingi sana kumpata mtu sahihi wa kucheza kama Right Winger, James kaja ila bado ana mengi ya kujifunza. United wanapaswa kuvunja kibubu. Sancho ni mtu sahihi tunapaswa kuitumia hii nafasi kujiimarisha.

Mitrović. Sio mchezaji ambaye yupo sokoni ila ni cheap option ya nafasi ya striker. Huyu jamaa sipatii picha akizungukwa na Rashford, Sancho, Pogba, Bruno. He's far better than Martial. Ni moja ya mmaliziaji mzuri sana.

Hawa wachezaji wote umri wao unaendana na sera za timu. Kwa umri wao wanakupa muda mzuri kuunda kikosi huku bado wakiwa katika umri mzuri kucheza soka.

NOTE: HIZI TRANSFER ZOTE HAZITAFANYIKA MSIMU HUU ILA HIVI NDIYO JINSI UNITED WANAPASWA KUINGIA SOKONI.
Magalhaes close joining Arsenal
 
Kunawakati mpira una amriwa na bahati, Timu imecheza vizuri imepata nafasi nyingi ila bahati aikua kwa man u.sevilla wamecheza kiasi ila bahati ilikua upande wao.

Mmekojolewa maziwa meupe meupe mazito yanalendemka
 
Back
Top Bottom