RW ndio huyo Sancho tunamfukuzia mkuu
Striker tunaweza kutafuta ila sio under pressure (dalili zinaonesha hivyo), kuja kwa Sancho automatically atam push Greenwood awe namba 9 back up ya Martial, japo haimaanishi kuwa ndio kamwe hatapangwa winger ya kulia, pia haimaanishi mbele ya safari hawezi kuwa mbele ya Martial kwenye machaguo ya kocha.
RB tusahau mkuu wangu, bora hata ungewaza LB, maana Shaw spana mkononi, kuna tetesi Brandon anaweza kwenda kwa mkopo ingawa inategemeana na a lot of factors.
Upande wa RB Ole anaweza kuendelea kumuamini AWB na Dalot, japo Dalot anaweza kuondoka (kwa kutaka au kuuzwa) na Ole akamuamini Laird bwana mdogo mwingine kutoka academy U23, japo yeye ana miaka 18 (huyo ndio Ole wetu wakuu)
CB kuwa na new addition ni ngumu, Ed ameshatumia £142M kwa miaka hii 3 au 4 kwa Bailly, Lindelof na Maguire. Uwezekano uliopo akimuuza Smalling, Rojo na Jones au 2 kati ya hao ni kuongeza CB kutoka ndani kwa kuwapandisha Teden Mengi mwenye miaka 18 lakini kafanya vizuri sana kwenye timu ya U23 na kuendelea kuwaamini Axel na Bailly kama Back up ya kapteni na Lindelof.
CM/CDM ni moja kati ya nafasi ambazo mimi natamani iwe kipaumbele chetu, ila kitendo cha Matic kupewa mkataba wa muda mrefu inanifanya niamini kuwa kwenye nafasi hiyo kwa msimu wa 2020/2021 tutatumia rasilimali zilizopo klabuni.
Ndidi kuna jarida nilisoma yeye kwa miaka 3 mfululizo ndiye CDM/HM mwenye ball recoveries/tackles (au vyote) nyingi kuliko yoyote kwenye ligi kubwa 5 Ulaya.
Kuna wakati kocha wake wa Genk alisema huu jamaa miguu yake ina darubini ya kuona mipira unapotaka kupeleka na upinzani. Kwenye hiyo nafasi naona Ndidi is the man, sio tu kwa kile ninachosoma majaridani, hata kwa utulivu ninaouona akiwapa Soyuncu na Evans pale Leicester.
United tumefocus kwenye dili la Sancho sana kiasi kwamba tunaweza jikuta dirisha linafungwa tumefanya usajili mmoja tu, wakati bado tunahitaji wachezaji wengine sio chini ya wawili yaani CB, RW na RB na ikiwezekana Midfield moja ya kibabe (mkata Umeme) kama Partey au Ndidi ila EdWood na jopo lake wanakomaa na Sancho mwisho wa siku tutashindwa kusajili the right players,
Inatakiwa tujifunze kwa City wako wakitaka mchezaji dili haichukui wiki mbili tayari wameshasajili