Sijui kwanini hivi vimashabiki vya Arsenane , Chelsea na Liverpool vipo teyari kuungana na kuona man u inaangamia kwa kutoingia top 4. Cha ajabu yaani hata Arsenane ambaye yuko mahututi huku akipumlia mdomo na kula chakula kupitia mishipa akiwa hoi kupambana na hali yake kuingia Europa naye bado tu focus yake ipo kwenye matokeo ya Man u. Ila nimekuja kugundua kuwa mziki wa Ferguson wa kutawala Premier league mara kwa mara mfululizo from 1992 to 2013 ndicho kinachowaogopesha mashabiki wa timu pinzani kwamba man wakiingia tu kwenye form basi kuna hatari ya utawala kurudi tena kwa Mfalme Man U. Na sasa ukiangalia dalili zilizopo kwa sasa na rekodi zilizowekwa toka Fundi Bruno kaingia yaani ni tishio.
1. Kwanza ukianza na best front three kuliko timu yoyote Uingireza Yaani Rashford, Martial na Greenwood wenye magoli 60 mpaka sasa,, na tukumbuke hii rekodi mara ya mwisho ilikuwa kipindi cha Ferguson tukiwa na Rooney , Vanpersie na Chicharitto, hivyo dalili za ile man u ya Ferguson inaanza kurejea.
2. Pia Manu kuwa Unbeaten 19 games,, hata Mourinho hakuweka hii record bali ni Man u ya Ferguson ndiyo ilikuwa na uwezo . Ila tumeona toka dirisha dogo la usajili lifungwe tunaona mambo yamewezekana.
3. Martial kuwa striker wa kwanza Man u kufunga hatrick premier league toka enzi za Ferguson na hivyo kufuta ukame wa hatrick kwa washambuliaji wa Man u ,,Sasa hapa tutegemee nyinginezo msimu ujao kutoka kwa Bruno,Rashford,Martial na hata Sancho kama ikitokea kasajiliwa.
4. Man u kuwa timu ya kwanza premier kufunga mabao matatu au zaidi kwenye mechi nne mfululizo. Tukumbuke Ferguson hakuwahi kufanya hiki kitu, hata Arsenal ya 2004 nayo haikuwahi kufaya hili jambo, ila pia na Mancity iliyoweza kufikisha pointi 99 kwa misimu miwili haikuweza kufanya huu mziki uliofanywa na United ya sasa.
5. Man u kuzalisha kinda Mason Greenwood mwenye umri wa miaka 18 ambaye kafunga bao 9 premier League. Tukiseme tuangalie rekodi ya toka Ferguson ameondoka yaani hakuna kabisa, Na isitoshe ukiangalia rekodi ya Chelsea,Arsenal na Liverpool nao pia hawana na hawatakuwa na kinda wa miaka 18 kufunga bao 16 msimu mmoja. Hapa tena msimu haujaisha huenda mechi za Europa akafikisha bao 20, Na tukisema tuangalie rekodi ya timu pinzani za top 4 utapekuwa data base nzima ya premier league na kuambulia utupu, na kama kuna rekodi basi ni miaka 20, 30 au 50 iliyopita ili kumpata kinda wa miaka 18.
6. Bruno kufunga bao 7 na assist 7 kwenye mechi 11 hivyo kutengeneza bao 14 na kumfanya kuwa Midfielder pekee aliyecheza mechi 11 na kuzalisha bao 14 premier league. Ndio maana hata asipofunga lazima atoe assist . Tukumbuke hata ukiangalia waliokuwa midfielders bora kama Fabregas, Yaya toure, Lampard na Hata Kelvin De Bruye bado hawana rekodi ya 11 few matches with 7 goals na assist 7,, Yaani ni jina la BRUNO FERNANDES PEKEE.
Sasa mashabiki wa Chelsea , Arsenal na Liverpool msiogope hizo takwimu na kupanic kwamba utawala wa premier league miaka 2020 na kuendelea inaweza ikarudi kwa mfalme, na hapa bado hatujasajili na je tukisajili si ndio mtakufa na presha. Mafanikio ya sasa hizo zote ni juhudi za wachezaji , kocha na mipango ya Mungu. Kama hii decade ya 2020 to 2030 Mungu kapanga iwe ya Mfalme man u basi hamna jinsi itabidi mzoee kama mlivyozoea 20 years ya utawala wa Ferguson.
MAN U wll always be RED..