ingelipendeza kama wangelimpa mkataba wa miaka 2 wenye kipengele cha kumuongezea mwaka 1 kama walivyofanya kwa juan mata...
========================
kupewa kwake mkataba wa muda mrefu haimaanishi ya kwamba atakuwa ni mchezaji wa uhakika wa kikosi cha kwanza bali performance yake ndiyo itakayoamua mustakabali wake kama ilivyo hivi sasa (mwanzoni mwa msimu muda mwingi aliutumia benchi), ina maana ikiwa klabu itachoshwa na uwepo wake wana uwezo wa kumruhusu aondoke huku klabu ikitengeneza faida ya mauzo yake kama ilivyokuwa kwa ashley young tofauti na kuondoka mwishoni mwa msimu huu.
Management imezungumzia ishu ya experience aliyonayo na heshima kwa young players
kwa tafsiri ya haraka ni kwamba klabu haipo tayari kwa sasa kuingia sokoni kwa lengo la kutafuta midfield mwenye sifa yake (tetesi za ndidi, partey na wengineo zimezimwa rasmi) ila wataendelea kuwatumia hawa waliopo (fred na scott) huku wakiendelea kuyafuatilia maendeleo ya kisoka kwa wachezaji vijana waliopo klabuni (garner na levitt).
cha umuhimu ni kuomba mzee matic aendelee kucheza kwa nidhamu hii aionyeshayo majira haya ya 2020, huenda atakuwa ndiye michael carrick wetu.
=================
halafu hii ishu ya kuextends mkataba mpya kwa mchezaji asiye na impact kubwa sana uwanjani nayo ni kama kamari, nakumbuka katikati ya msimu uongozi wa klabu ulimshinikiza ashley young asaini kandarasi mpya huku mashabiki wengi tukichukizwa na uamuzi huo bahati nzuri sana ashley young alisoma alama za nyakati na hatimaye akaamua kuondoka mwezi January.
rejea ishu ya fellaini, alipewa kandarasi mpya kwa sababu ya shinikizo la mwalimu lakini tulipofanya mabadiliko ya benchi la ufundi tukapata bahati ya kumuuza kwa hela nzuri...
kwa sasa tumecheza kamari kwa marcos rojo na phil jones, wote hawa tumewapa mkataba wa muda mrefu huku mustakabali wao ukiwa haujulikani (mpaka sasa hakuna timu zilizoonyesha nia za kuwahitaji)
nadhani ndio maana baadhi ya mashabiki wana wasiwasi na hii dhana ya kutoa mkataba wa muda mrefu kwa wachezaji waliovuka peak ya ubora wao