hivi huwezi kuwa legend kwa team zaidi ya moja
- labda tukisema sir alex ferguson ni legend wa Aberdeen na man utd itakuwa si sahihi, au aberdeen hawana haki ya kumshukuru sir alex ferguson kwa mafanikio aliowapatia?
- tukisema kenny daglish ni legend wa blackburn rover, celtic na liverpool tutakuwa tunakosea?
- hivyo hivyo kwa ronaldo
kama tunaiangalia tafsiri ya legend kwa kigezo cha umri na kuhudumu klabu kwa muda mrefu basi ronaldo hawezi kuwa legend kwa sababu ameondoka man utd akiwa na miaka 24 (amedumu klabuni miaka 6, miaka mitatu ya mwishoni akiwa kwenye ubora, nguvu kubwa zaidi aliitumia real madrid ndio maana si ajabu alikwenda kubeba tuzo lukuki huko spain), tofauti na wayne rooney aliyeondoka klabuni akiwa na miaka takribani 30, miaka yake 12 akicheza soka la kiwango cha juu tofauti na CR7 tuliyemvumilia kwa miaka takribani miwili hadi mitatu
kama tunauangalia mchango wa mchezaji husika basi ronaldo anaingia katika kundi la wachezaji muhimu zaidi kuwahi kutokezea ndani ya klabu kama wengineo (tulishinda makombe matatu mfululizo ya ligi kuu huku yeye akiwa ni tegemezi, tumecheza mara tatu mfululizo nusu ya fainali ya champions league na kubeba ubingwa mara moja)
kuhusu ishu ya nidhamu hata hao wengineo mfano paul scholes, rooney, giggs, cantona, roy keane, david beckham kwa nyakati tofauti waliwahi kuonyesha matendo maovu dhidi ya klabu kwa sababu zao binafsi kama vile ishu ya mkataba, kulinda heshima zao (ego).
turejee mgogoro wa rooney na man utd kuhusiana na mustakabali wake na klabu (rooney alifika kuponda sera za uendeshaji wa klabu hadharanu hususani kwenye ishu ya usajili, kumbe kelele zote alitaka ongezeko kubwa la mshahara wake, hivi tusema na yeye hakuwa na mapenzi ya ukweli na united?)
paul scholes aliwahi kugoma kuingia uwanjani mnamo mwaka 2001 kwa sababu ya hoja ya kikosi dhaifu kilichochaguliwa kucheza dhidi ya arsenal, hatimaye akapigwa faini, ndipo kipindi hicho tetesi za kuelekea Inter milan zikaanza kuzagaa , pia ujio wa sebastian veron ulipelekea achezeshwe nafasi isiyompendeza(namba 10) na jambo hilo likazidi kumkosesha amani, ndio maana sven goran erikson alikuwa anamtumia paul scholes left winger kama ilivyokuwa man utd, kwa kuwa mzee alikosa bahati mzigo wa matusi ukamuangukia yeye na si ferguson aliyeanzisha tabia ya kumbadilisha nafasi paul scholes tokea mwanzoni.
rejea sakata la cantona na kung fu zake
rejea sakata la roy keane (mpaka leo anamchukia fergie)
rejea sakata la beckham na fergie
rejea sakata la nistelrooy
cristiano ronaldo tokea mwanzoni alishaweka wazi dhamira yake ya kutaka kuichezea real madrid kabla hata hajawa nyota muhimu ndani ya kikosi chetu, halafu ile ishu yake ya usajili kipindi kile ilichafuliwa zaidi na sepp blatter (aliwahi kusema kuna timu zinawafanya wachezaji kuwa ni watumwa na haikuwa kauli yenye kupendeza masikioni mwa united ila ni kauli yenye kupendezwa masikioni mwa ronaldo kwa sababu aliona amepata mtetezi atakayemsaidia kutimiza ndoto zake za muda mrefu za kuichezea real madrid kwani hakuna mtu aliyekuwa tayari ndani ya united kumpoteza ronaldo kijinga jinga)
I am a slave, says Ronaldo as he pushes for Madrid move