Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Duu scholes aliwahi hitajika na AC Milan akaletewa hadi cheque asaini kiwango cha mshahara anachotaka badala yake alimwambia Rais wa Milan kwamba kama unataka kuninunua Mimi ili unipate basi inunue Manchester United. Passion ya hali ya juu sana hii!
Wewe ungekuwa mchezaji kwa kizazi hiki usingefanya ujinga alioufanya Scholes au Giggs.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila mimi hapo upande wakuifunga Manchester United nishawahi shuhudia mechi moja tu Tena akiwa Juventus (UEFA CHAMPIONS LEAGUE) TU sina kumbukumbu vizuri kama kuna Mechi zaidi ya hiyo alishangilia wala kuifunga Manchester United.
Maana kuna Mechi kibao nilikuwa naona Jamaa anajifanya kukosa makusudi ama kujiangusha tu ili asfunge maana hizo chance kwake sio Rahisi kihivyo kukosa hata kama angekuwa mtu mwingine.
Ko kuwafunga Mala moja sioni kosa huenda anasababu zake maana kilikuwa ni kipindi Cha José Mourinho na watu walikuwa hawamtaki huenda alifanya hivyo kwa lengo lakuongeza hamasa (chachu) kwa watu juu yakumchukia na Kumponda atoke OT.
Mimi huyu kijana alinitoka kuna mwaka Fulani aliitumia sana Man u ktk kutaka aongezewe mshahara pale real Madrid akawa anafanya drama nyingiii! Mara kwenye akaunt yake ya Twitter aandike "i miss red", Mara aposti picha enzi yupo Man U, waandishi wakawa wanamuuliza kwa nini anafanya hayo akawa anawaambia Manchester United ni nyumbani kwake Hivyo anapamiss nyumbani. Baada ya kuongezewa mkataba mnono kuna siku mwandishi akamuuliza kwamba " uliwahi sema unaimiss Man U kwa sababu ni nyumbani je kwa kusaini mkataba mwingine tena wa muda mrefu unahisi utapata fursa ya kurudi Man U!? Akamjibu mwandishi moja ya maneno alojibu ni "Hey stop telling me stupidity things, am a real Madrid player". Kwa kweli baada ya hapo sijawahi kuwa na affiliation nae tena. Na kuna mechi tulicheza na juve kama sikosei alifunga goli na akashangilia sana,legend wa timu fulani hawezi Fanya hivyo tena ukizingatia cr7 hajawahi chukiwa na washabiki wa Man U.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila mimi hapo upande wakuifunga Manchester United nishawahi shuhudia mechi moja tu Tena akiwa Juventus (UEFA CHAMPIONS LEAGUE) TU sina kumbukumbu vizuri kama kuna Mechi zaidi ya hiyo alishangilia wala kuifunga Manchester United.
Maana kuna Mechi kibao nilikuwa naona Jamaa anajifanya kukosa makusudi ama kujiangusha tu ili asfunge maana hizo chance kwake sio Rahisi kihivyo kukosa hata kama angekuwa mtu mwingine.
Ko kuwafunga Mala moja sioni kosa huenda anasababu zake maana kilikuwa ni kipindi Cha José Mourinho na watu walikuwa hawamtaki huenda alifanya hivyo kwa lengo lakuongeza hamasa (chachu) kwa watu juu yakumchukia na Kumponda atoke OT.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mchezaji professional hawezi kujiangusha ili asifunge.
 
How you name Valencia,De Gea,OGS ,Oshea United legend and CR7 is not among them.



Sent using Jamii Forums mobile app
Naona kama hao wengine walikuwa na shauku kubwa ya kucheza muda mrefu Man U na ni watumishi watumwa kwa badge ya Man U ilihali CR7 ni kama alikuwa ana pitisha muda tu kabla ya kwenda akupendako. Naamini hata Man U asingechukua UEFA na vikombe vya ndani bado yeye angefika ktk huo muda alioomba kuondoka angefanya hivyo na akatembea tu.
 
Probably.

Unaweza kunielewesha zaidi?
Kikubwa hapo ni kwamba pamoja na umaarufu alioupata na mafanikio pale Man U bado haikuwa na maana nzuri kuomba kuondoka ktk umri Mdogo vile. Hii manake yeye ni kama alikuwa anasikilizia tu muda ukifika afosi kuondoka kwenda timu aipendayo zaidi.
 
Kikubwa hapo ni kwamba pamoja na umaarufu alioupata na mafanikio pale Man U bado haikuwa na maana nzuri kuomba kuondoka ktk umri Mdogo vile. Hii manake yeye ni kama alikuwa anasikilizia tu muda ukifika afosi kuondoka kwenda timu aipendayo zaidi.

Nimekuelewa, huoni kama huo ni ubinafsi wetu washabiki?

Kwamba hatutaki wachezaji tunaowakubali wakatafute maisha bora zaidi kwingine!
 
Kiukweli upande wangu mim alivoondoka katika umri ule nilimchukia sana niliona bado mdgo kama alikua anaipenda utd angekaa zaidi atupe mataji mengi maana aliondoka at his peak..mpaka leo I'm not his fan

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuelewa, huoni kama huo ni ubinafsi wetu washabiki?

Kwamba hatutaki wachezaji tunaowakubali wakatafute maisha bora zaidi kwingine!
Maisha bora kipesa siyo!? Kijana hakuomba kuongezewa mkataba mzuri zaidi Bali aliomba kujiunga na Real Madrid tena akiwa Mdogo kabisa! Hapo ndo panapotia shaka juu ya loyalty na passion yake kwa Man U mkuu.
 
Maisha bora kipesa siyo!? Kijana hakuomba kuongezewa mkataba mzuri zaidi Bali aliomba kujiunga na Real Madrid tena akiwa Mdogo kabisa! Hapo ndo panapotia shaka juu ya loyalty na passion yake kwa Man U mkuu.

Swala siyo mshahara tu, ni pamoja na commands kwenye endorsements.

Kwa kiwango chake, kuna endorsements kibao ambazo ni rahisi kuzipata Spain zaidi kuliko angeendelea kuhangaika na Uingereza.

Anyway, kwangu mimi naona washabiki tunakuwa hatupendi wachezaji wetu wahame kwenda kutafuta maisha mapya, ila akiuzwa tunafurahi na kuona kawaida.

Labda nikuulize: Beckham ni legend wa Man Utd?
 
Man United vs Real Madrid Ronaldo aliwafunga United robo finally UEFA Champions League.

Kocha wa Man United alikuwa Sir Alex Ferguson Madrid alikuwa Jose Mourinho.

Mwamuzi wa mechi hii alikuwa Cuynet Cakir.

Madrid alifunga magoli yake baada ya Luis Nani kutolewa kwa red card ya hovyo kabisa kuwahi kutokea kwa kumchezea Faulo Alvaro Albeloa.

Real Madrid wakawa knocked out kwenye Semi final na Borussia Dortmund.

Ronaldo hakushangilia lile goli.
Ila mimi hapo upande wakuifunga Manchester United nishawahi shuhudia mechi moja tu Tena akiwa Juventus (UEFA CHAMPIONS LEAGUE) TU sina kumbukumbu vizuri kama kuna Mechi zaidi ya hiyo alishangilia wala kuifunga Manchester United.
Maana kuna Mechi kibao nilikuwa naona Jamaa anajifanya kukosa makusudi ama kujiangusha tu ili asfunge maana hizo chance kwake sio Rahisi kihivyo kukosa hata kama angekuwa mtu mwingine.
Ko kuwafunga Mala moja sioni kosa huenda anasababu zake maana kilikuwa ni kipindi Cha José Mourinho na watu walikuwa hawamtaki huenda alifanya hivyo kwa lengo lakuongeza hamasa (chachu) kwa watu juu yakumchukia na Kumponda atoke OT.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pale United Christiano Ronaldo alikuwa ameshashinda kila kitu huoni kuwa ilikuwa sahihi kwake kwenda kutafuta changamoto mpya?
Kikubwa hapo ni kwamba pamoja na umaarufu alioupata na mafanikio pale Man U bado haikuwa na maana nzuri kuomba kuondoka ktk umri Mdogo vile. Hii manake yeye ni kama alikuwa anasikilizia tu muda ukifika afosi kuondoka kwenda timu aipendayo zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiukweli upande wangu mim alivoondoka katika umri ule nilimchukia sana niliona bado mdgo kama alikua anaipenda utd angekaa zaidi atupe mataji mengi maana aliondoka at his peak..mpaka leo I'm not his fan

Sent using Jamii Forums mobile app

Then nadhani wewe ni mbinafsi, kama kigezo cha ulijendari kwako ni kuzeekea katika timu yako.... Naweza kusema Ronaldo ameshinda kila kitu ambacho angeweza kushinda na Man Utd na tunapaswa kumshukuru kwa mchango wake kwa kipindi ambacho amekua mtumishi wetu pale O.T

Hoja ya kwamba angeendelea kubaki sioni kama ina mashiko ukizingatia soka ni ajira ya muda mfupi. Ronaldo kama binadamu nayeye anashauku ya mafanikio binafsi (angeendelea kubaki UTD sidhani kama angelishinda mataji na tuzo binafsi nyingi kama ambavyo amefanya na R.Madrid).
Labda kama tutasema sisi UTD tunajali timu yetu tu bila kuangalia tutaathiri vipi maisha ya watu wengine.

Kwa mimi, Ronaldo ni legend pale old trafford kwa kuzingatia muda aliokaa na mchango wake.
 
Halafu lazima tujue kwamba Ronaldo ni kijana tuliyejuana naye ukubwani tu, kijana mzaliwa wa Madeira Ureno kuwa loyal kwa Man Utd (ya Uingereza) naona kama ni hisani tu, labda kama angekua ni Mwingereza tena mzaliwa wa jiji la Manchester...

Tumpime kwa mchango wake kwa kipindi alichokua nasisi na sio wenzetu walifaidika nae vipi.

Hata ile biashara tuliyofanya na Madrid ilikua ni hela nzuri sana kwa kipindi kile kwa hiyo aliondoka kwa faida, ingekua aligoma kusaini mkataba na kuondoka bure hapo sawa.
 
Hata takwimu zake pale united kwa muda aliokaa pale zinatosha kabisa kumpa sifa ya legend wa united.

Kama Ronaldo siyo legend wa united vipi kuhusu Beckham na Rud Van Nistrooy au Robin Van Persie ?
Halafu lazima tujue kwamba Ronaldo ni kijana tuliyejuana naye ukubwani tu, kijana mzaliwa wa Madeira Ureno kuwa loyal kwa Man Utd (ya Uingereza) naona kama ni hisani tu, labda kama angekua ni Mwingereza tena mzaliwa wa jiji la Manchester...

Tumpime kwa mchango wake kwa kipindi alichokua nasisi na sio wenzetu walifaidika nae vipi.

Hata ile biashara tuliyofanya na Madrid ilikua ni hela nzuri sana kwa kipindi kile kwa hiyo aliondoka kwa faida, ingekua aligoma kusaini mkataba na kuondoka bure hapo sawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona kama hao wengine walikuwa na shauku kubwa ya kucheza muda mrefu Man U na ni watumishi watumwa kwa badge ya Man U ilihali CR7 ni kama alikuwa ana pitisha muda tu kabla ya kwenda akupendako. Naamini hata Man U asingechukua UEFA na vikombe vya ndani bado yeye angefika ktk huo muda alioomba kuondoka angefanya hivyo na akatembea tu.
Hata Phil Jones,Lingard wana shauku ya kucheza United muda mrefu so wao ni legend while CR7 sio

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swala siyo mshahara tu, ni pamoja na commands kwenye endorsements.

Kwa kiwango chake, kuna endorsements kibao ambazo ni rahisi kuzipata Spain zaidi kuliko angeendelea kuhangaika na Uingereza.

Anyway, kwangu mimi naona washabiki tunakuwa hatupendi wachezaji wetu wahame kwenda kutafuta maisha mapya, ila akiuzwa tunafurahi na kuona kawaida.

Labda nikuulize: Beckham ni legend wa Man Utd?
Naamini hivyo kwa sababu yeye alikulia pale na alikuwa anaipenda sana timu ila hitilafu na mwalimu ikafanya mwalimu asihitaji tena kuendelea nae. Ila hata baada ya kuondoka na kustaafu mpira bado Becks anaipenda sana timu. Becks ni kama Roy Kean tu,ni watu walokuwa wakiipenda timu na wanafia timu haswa ila mwisho wa siku Ferg nae alikuwa na ubinadamu wake
 
Then nadhani wewe ni mbinafsi, kama kigezo cha ulijendari kwako ni kuzeekea katika timu yako.... Naweza kusema Ronaldo ameshinda kila kitu ambacho angeweza kushinda na Man Utd na tunapaswa kumshukuru kwa mchango wake kwa kipindi ambacho amekua mtumishi wetu pale O.T

Hoja ya kwamba angeendelea kubaki sioni kama ina mashiko ukizingatia soka ni ajira ya muda mfupi. Ronaldo kama binadamu nayeye anashauku ya mafanikio binafsi (angeendelea kubaki UTD sidhani kama angelishinda mataji na tuzo binafsi nyingi kama ambavyo amefanya na R.Madrid).
Labda kama tutasema sisi UTD tunajali timu yetu tu bila kuangalia tutaathiri vipi maisha ya watu wengine.

Kwa mimi, Ronaldo ni legend pale old trafford kwa kuzingatia muda aliokaa na mchango wake.
Mimi namuona ni mtu aliyekuwa hana loyalty kwa ile timu. Alipotufunga akiwa Madrid hakushangilia nadhani alifanya vile kwa kuwa alijua hafahamu kesho yake, ila alipotufunga akiwa Juventus naamini alishangilia sana kwa sababu ashajua uwezekano wa kesho yake kuwa Man U ni kama Mdogo au hakuna.
 
Mimi namuona ni mtu aliyekuwa hana loyalty kwa ile timu. Alipotufunga akiwa Madrid hakushangilia nadhani alifanya vile kwa kuwa alijua hafahamu kesho yake, ila alipotufunga akiwa Juventus naamini alishangilia sana kwa sababu ashajua uwezekano wa kesho yake kuwa Man U ni kama Mdogo au hakuna.

Mifumo imebadilika sana baada ya mpira na michezo mingine kuwa kibiashara zaidi.

Hatuangalii loyalty siku hizi, ni business tu.

Leo hii utakuta mchezaji ni brand inayojitegemea, zamani mchezaji alikuwa ni mali ya timu kwa 100%.

Sasa hivi hicho kitu hakipo. Mchezaji akiichoka timu anaondoka, na timu ikimchoka inamtema.
 
Back
Top Bottom