D A E M U S H I N
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 22,633
- 121,022
khofu yangu ipo kwa timu zitakazohitaji huduma ya harry kane sidhani kama wataweza kuhimili gharama zake za usajili (amebakisha miaka 4 kwenye mkataba wake) pamoja na mshahara wake (bila ya kusahau ugumu wa kufanya biashara na daniel levy ukimuongezea na jose mourinho anayehitaji kujenga timu ya ushindani)Kwenye safu ya ushambuliaji kwa umri wa Ighalo sioni kama atapewa permanent Contract lakini sokoni hakuna watu watakaoweza kununulika kwa dau dogo, kilichowazi ni kwamba Harry Kane kama Tottenham hawatafika top four huenda akaondoka Tottenham dau lake Daniel Levy anajua.
mauricio pochettino endapo atafanikiwa kupata offer ya kufanya kazi kwenye timu kubwa (kati ya man city, psg au man utd) basi upo uwezekano wa kumshawishi harry kane ajiunge naye kwenye timu, kinyume chake si guardiola. thomas tuchel, zidane, bayern munich watakaokuwa tayari kulipa zaidi ya paundi millioni 130 kupata huduma ya harry kane.
kinyume chake
== bayern munich - robert lewandowski bado wataendelea kumtegemea kwa misimu mengine miwili
== psg - mauricio icardi (wanaweza kumsajili rasmi baada ya kumalizika kwa mkopo, amewafungia magoli 20 kwenye mechi 31)
== josep guardiola-sergio aguero ataendelea kuwepo chini yake, bila ya kusahau zimwi la financial fair play bado linawatafuna
== barcelona - ni kweli wanahitaji mrithi wa luis suarez ila sidhani kama harry anaweza kuvutiwa na offer ya kucheza barcelona japokuwa ni ndoto ya kila mchezaji kucheza pamoja na mtakatifu messi lionel, jambo baya zaidi kwa miaka hii ya karibuni barcelona wamefanya usajili kwa kuleta wachezaji kwa kutumia gharama kubwa lakini bado wameshindwa kukiepuka kivuli cha messi kiutegemezi (watakuwa makini sana kufanya usajili msimu ujao)
== real madrid - sikio la kufa kwa kylian mbappe (zidane anamuhitaji sana mbappe kuliko paul pogba ndivyo ninavyoamini), ni rahisi kulipa paundi millioni 150 kupata huduma ya mbappe kuliko hela hiyo kuielekeza kwa harry kane, bila ya kusahau real madrid wanaweza kuvunja kikwazo (release clause) kilichowekwa na wakala wa erling haarland ili kupata huduma yake kuliko kutumia mara mbili ya fedha kupata huduma ya harry kane.
ukiziangalia timu zote tajwa hapo juu utagundua takribani zote zinasumbuliwa na matatizo yasiozidi mawili (maeneo watakayoyafanyia kazi kwenye usajili) tofauti na manchester united ambao kwa akili ya haraka haraka tungelipendelea kushuhudia usajili wa wachezaji watatu wenye viwango vikubwa, kivyovyote harry kane ni mchezaji muhimu sana tunayemuhitaji nyakati hizi tunazojiandaa kurudisha ubora wetu wa kiushindani barani ulaya, kikwazo kikubwa itakuwa ni bajeti ya usajili sidhani kama inatosheleza kuelekeza nguvu sehemu nyenginezo kama tutaweka kipaombele kwa harry kane.
pia tumekuwa tukiimba wimbo wa kuhitaji winga wa kulia (kiitikio chetu ni jadon sancho), kwa hesabu za haraka haraka utahitaji takribani paundi millioni 250 kufanya usajili wa wachezaji hao wawili (jadon sancho, harry kane), bila ya kusahau hadithi za kumhitaji kiungo mshambuliaji mwengine atakayeziba nafasi ya jesse lingard, andreas perreira (hapa kwa kiasi kikubwa tunamuangalia jack grealish au james maddison)
harry ni mshambuliaji mwenye uhakika wa kukupa magoli 25 kwa msimu mmoja pindi anapokuwa fiti ( 181 goals and 30 assists in 278 games for Spurs ), lakini tatizo kubwa ninaloliona ukiachana na gharama za usajili ni kuhusu afya yake (injury prone), ukiangalia takwimu zake kiwango chake cha ufungaji wa magoli kimekuwa kikipungua kila msimu kutokana na kukosa muda wa kutosha wa kucheza.
59 League goals in 67 games in 16/17 season and 17/18 season (0,88 goals per game)
28 League goals in 48 games in 18/19 season and 19/20 season (0,58 goals per game)
16/17 (0.96 goals per game) = amecheza mechi 30
17/18 (0.81 goals per game) = amecheza mechi 37
18/19 (0.60 goals per game) =amecheza mechi 28
19/20 (0.55 goals per game) = msimu huu amecheza mechi 20
ninachokiona mimi klabu itatafuta cheap option (labda ighalo, joshua king) then fedha nyengine zitaelekezwa kwenye usajili wa jadon sancho (haijalishi tumepata tiketi ya UEFA au kinyume chake), unajua tunaelekea mwaka wa 10 tumeshindwa kupata winga atakayekata kiu ya hitaji letu.
usajili wa harry kane na jadon sancho unahitaji maamuzi ya kibabe kwa sababu wote tunawahitaji kama ubongo na uti wa mgongo, wengi wetu hatufurahishwi na safu yetu ya ushambuliaji kuongozwa na anthony martial, pia wengi wetu hatufurahishwi kuona eneo letu la winga wa kulia linaongozwa na juan mata, jesse lingard na daniel james.