Mc cane
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 5,569
- 10,527
Mkuu, kuna watu wanaamini mfumo wa ATM hauendani na kipaji cha Joao Felix
Lakini mbona Griezman ame shine pale ATM kwa mfumo ule uliopo
Na Joao alikuwa ni like to like replacement ya Griezman
Kuna tatizo sehemu zaidi ya mfumo wa uchezaji wa ATM
Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini mbona Griezman ame shine pale ATM kwa mfumo ule uliopo
Na Joao alikuwa ni like to like replacement ya Griezman
Kuna tatizo sehemu zaidi ya mfumo wa uchezaji wa ATM
baadhi ya nyakati wachezaji wa ulaya ambao tunawafahamu kama ni professional (wa tabia, matendo na fikra) hufanya maamuzi ambayo hayatofautiani na yale yanayochukuliwa na wachezaji wa kiswahili (unampongeza samatta kwa kucheza aston villa ila wewe unakataa ofa ya tp mazembe, unakimbia sweden na unaikataa al ahly ya sudan kwa sababu ya hamida)
diego simeone ameshafundisha atletico madrid kwa takribani miaka mitano na falsafa yake ya ufundishaji haijabadilika hata kwa sekunde moja (ni mtu anayeamini team work kuliko kutegemea miujiza ya mchezaji mmoja).
huyo felix alikuwa halifahamu jambo hili pamoja na washauri wake?
ndio yale ya alexander hleb (fundi) anaondoka arsenal akiwa ni mchezaji muhimu sana na hatimaye anaelekea barcelona akiamini kwa uwezo aliojaaliwa hatoweza kuwekwa nje, kwa akili ya kawaida ina maana alexander alikuwa hafahamu ya kwamba kwa uwezo aliokuwa nao na style yake ya uchezaji hatoweza kumweka nje andreas iniesta pamoja na thiery henry kwenye mfumo wa 4-3-3?
pia rejea ishu ya:
alexander song na barcelona ya sergio bosquet
mascherano na barcelona ya sergio bosquet
cesc fabregas dhidi ya xavi hernandez
sipingani na sera au tabia ya mchezaji kwenda kutafuta changamoto mpya ya kazi yake bali napingana na tabia ya mchezaji husika kuhama sehemu ambayo inaweza kumhudumia mahitaji yake yote na kuelekea sehemu ambayo haitoweza kumhudumia kimahitaji (wengi wao hufikiria mahitaji muhimu ni ongezeko la mshahara na makombe).
joao felix alihitaji timu mfano wa borussia dortmund ila kwa mazingira ya usajili wake isingeliwezekana kwa sababu kila upande ulishaonyesha tamaa ya kuvuna fedha haramu bila ya kuangalia mustakabali wa felix kikazi.
atletico wamelipa takribani paundi millioni 100 kupata huduma yake, ni vigumu sana kumpata mjinga wa kulipa zaidi ya kiwango kama hicho au asilimia 70 ya kiwango hicho (kumuuza kwa bei ya hasara).
labda vichaa wanaoitwa barcelona wanaweza kulipa fedha kama hiyo, kama waliweza kulipa kwa dembele, coutinho, griezman, (paulinho na malcom) kwa nini wasilipe haliyakuwa wanatafuta mbadala wa lionel messi.
kinyume chake itakapomaliza corona miaka miwili ijayo huenda tukamuona joao felix kwenye ardhi ya china au japan akicheza soka pamoja na iniesta, hulk, ramirez, oscar n.k
----------------------------------------------------------
Alexander Hleb has admitted that he “made a mistake” leaving Arsenal for Barcelona in 2008. The Belorussian moved to Spain for a fee in the region of €15 million but failed to make an impact, being loaned out after just one season before finally leaving the club on a permanent basis in 2012.
Sent using Jamii Forums mobile app