Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu Napenda kutoa wazo tukakupime akili samahani lakini. Me naona hata akili yako inatu DNA twa COVID 19,UBISHI,UJUAJI UROPOKAJI na KIGEUGEU kulingana na hizo hoja zako mpaka sasa najitahidi kuamini ni wewe ninaekujua lakini nashindwa.
Haya ndo maswala nasemaga unachangia kitu kama "HUNA KICHWA JUU YA MABEGA".

Sent using Jamii Forums mobile app
huyu jamaa ndumilakuwili
 
Club official statement
skysports___B-PiscGIZYR___.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
JUVENTUS wanajipanga kuhakikisha wanatimiza ndoto zao za kumsajili kiungo wa Manchester United, Paul Pogba kwenye dirisha lijalo la usajili.
Kwenye mpango huo, miamba hiyo ya soka ya Italia imepanga ama kumtumia mshambuliaji Paulo Dybala au kiungo Miralem Pjanic kwenye dili la kuwashawishi Man United.
Pogba anaonekana kuwa kwenye nyakati zake za mwisho za maisha huko Old Trafford na huenda akaachana na timu hiyo kwenye dirisha lijalo la usajili huku Juventus wakimtaka mchezaji wao wa zamani arudi kwenye kikosi.
Real Madrid nao wanatajwa kuhitaji saini ya mchezaji huyo na hapo ndipo panapowafanya Juventus kutaka kuwapa Man United ofa ya mchezaji ili kushinda kwenye vita hiyo.
Man United wapo tayari kuachana na Pogba kama tu kutawekwa mezani Pauni 100 milioni huku mchezaji mwenyewe akidai kwamba atakasirika kama klabu hiyo itatumia kipengele kilichowekwa kwenye mkataba wake cha kuongeza mwaka mmoja zaidi wa kuendelea kubaki kwenye kikosi hicho. Mkataba wa sasa wa Pogba utafika tamati mwakani, lakini ndani yake kuna kipengele kinachowaruhusu Man United kumwongezea mwaka mmoja. Juventus wao wanamtaka na wapo tayari kuachana na mmoja wa wachezaji wao Pjanic na Dybala.

Rudi Nyumbani Kumenoga.
 
Back
Top Bottom