inasemekana tumefikisha mechi 11 bila ya kupoteza, kivyovyote kuna mabadiliko makubwa sana ya kiucheza ambayo tumeyapitia kwa nyakati hizi na ni tumaini la kila mdau wa man utd kuendelea kuomba hali hii tunayokwenda nayo izidi kuimarika zaidi na si kurudi tena nyuma kama ilivyokuwa msimu uliopita.
LASK waliwafunga sporting lisbon,PSV, AZ alkamaar cha kufurahisha zaidi hawa jamaa waliruhusu magoli manne kwenye kampeni yao ya EL (ila leo tumewafunga magoli matano kupitia wachezaji tofauti)
andreas perreira na
jesse lingard ndio wanadamu waliokuwa wanasababisha uwanjani tuwe pungufu pindi tunapocheza na kibaya zaidi tulikosa wachezaji wa kuziba nafasi zao (si kwa sababu hawakuwepo wachezaji wa kuchukua nafasi zao bali na wao pia hawakuwa kwenye viwango vyenye kueleweka).
fred alikuwa ovyo ila kwa sasa yupo vizuri
nemanja matic alipoteza muelekeo baadae akapata majeruhi, kuumia kwa mctominay kulimrudisha upya nemanja matic kwenye ulimwengu wa soka (kwa sasa unahitaji kuwa na degree ya roho mbaya pindi unapochagua mchezaji wa kuanza kwenye mechi kati ya
nemanja matic na
scott mctominay)
brandon williams amenivutia sana eneo la upande wa kulia (dogo ni asset inayo-ongezeka thamani ya ubora kama ilivyo ardhi).
victor lindeloff vs eric bailly (hii ni mechi ngumu sana)
bruno fernandez vs paul pogba (nimeshakata tiketi ya kushuhudia huu mpambano wa wanaume)
tumebakisha wachezaji watatu hadi wanne ili tuwe na timu ya ushindani.