Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

unnamed.jpg

Pogba akibaki

Brooks + Sancho + Timo Werner = €225

Pogba akisepa

Madison + Sancho = €180

Ikitokea Ole ashindwe yeye tu.
 
Huwezi leta presha kwenya club kubwa kama Chelsea wewe...

Sisi tuna uhakika wa kushiriki uefa kwa misimu mingine saba mfululizo na kubeba angalau matatu...uku mengine tukiishia hatua ya nusu au fainali kabisa...

This is Chelsea

#CFC

Sent using Jamii Forums mobile app
Dogo olachuga huwa ananifurahisha sana ebu ona majigambo yake ha ha ha!!
 
likizo yangu imekwisha
  1. phil jones
  2. jesse lingard
  3. andreas perreira
  4. marcos rojo
operation safisha taka taka inapaswa iendelee kwa kuwaondoa watumishi hao wanne (nitamheshimu sana OGS kama atatimiza mpango huu)

kama tutawaondoa hao walinzi wawili hakutakuwa na ulazima wa kutafuta mlinzi mwengine wa kati kwa bei ya gharama kwa sababu chris smalling tunaweza kumrudisha kikosini, vile vile upo uwezekano wa kumtumia luke shaw kama mlinzi wa kati hata kwenye mfumo wa kutumia walinzi wa nne ikitokezea harry maguire anahitaji mapumziko (hakuna lisilowezekana kwa mchezaji professional kubadilishwa nafasi pia references zipo nyingi kama vile david alaba, joshua kimmich, philip lahm na sergio ramos),

ukiachana na ole gunnar solskjaer na benchi lake la ufundi , kiukweli jesse lingard na andreas perreira wameturudisha nyuma sana msimu huu kwenye kampeni yetu ya kurudisha ubora wa timu yetu (ole aliweka matumaini makubwa sana kwa hawa vijana kabla ya ligi kuanza, bahati mbaya wameshindwa kumtihibitishia mwalimu na mashabiki juu ya umuhimu wao wa kuendelea kuaminiwa kikosini)......

kuna kila dalili mmoja wao kati ya hao wawili nafasi yake ikazibwa na mchezaji wa kiengereza japokuwa wapo wageni wenye viwango vizuri kama van der beek na martin ordegaard, kwa sasa ni wachezaji wawili tu ndio wamekuwa kwenye rada (james maddison na jack grealish), sidhani kama tuna uwezo wa kuwasajili wachezaji wote wawili kwa pamoja.

yupi ni bora kati yao msimu huu?
kiukweli sifahamu kwa sababu kwanza sijawahi kungalia mechi za aston villa hata mara moja (labda tumuulize ujugu kuhusiana na grealish) , pia nikiangalia takwimu za maddison nahisi kama kiwango cha utoaji huduma kimepungua sana msimu huu pengine ni mabadiliko ya kimajukumu aliopewa na mwalimu ndio chanzo (sina uhakika)... wanavyosema wadau ni kwamba faida ya jack grealish ana uwezo wa kucheza nafasi tofauti kwa kiwango cha juu.

andreas perreira ana miaka 24 ya kuzaliwa, naweza kusema ndiye mchezaji wetu aliyetumika kwenye nafasi nyingi tofauti bila ya kulalamikia maamuzi ya walimu, alipokuwa spain (granada na valencia) kwa nyakati tofauti kama nitakuwa sahihi alitumika kama winga, aliporudi klabuni chini ya jose alitumika kama double pivot midfield, alipokuja ole amekuwa akipendelea sana kumtumia kwenye mfumo 4-3-3 na pia kama namba 10.

andreas amejaaliwa bidii ya kupambana, solid mentality lakini amenyimwa ubora (quality), hana sifa za kuwa winga bora, hana sifa za kuwa kiungo bora wa ulinzi kama makelele, hana sifa za kuwa kiungo mshambuliaji bora hususani anapokuwa na mpira ndio maana si ajabu kumkuta akiwa na takwimu zisizoridhisha akiwa kama ni kiungo mshambuliaji.

ukiniuliza ni eneo gani bora ambalo andreas anacheza vizuri, jibu litakuwa sijui na sitaki kujua..
ni muda muafaka kwake yeye kutafuta timu isiyokuwa na presha ili apate kujijenga zaidi kwenye career yake ya soka na pia kulitambua zaidi eneo lake sahihi la kiuchezaji, hata kama atabaki msimu ujao nahofia atakuwa na msimu mgumu sana kiuchezaji.

habari njema kwa wote ni kwamba fred ameanza kutoka usingizini japokuwa ana ugonjwa wa kuanguka ovyo kama wilder..
tuliowahi kumtukana fred tukutane hapa tupate kuandaa waraka wa kuunga mkono juhudi za muheshimiwa manywele.
 
Ole anafanya kazi nzuri tuendelee kuheshimu maamuzi yake na rebuild anayofanya.

Kuhusu nani aje achukue nafasi ya Lingard au Pereira kama nikuchagua basi chaguo langu itakuwa. Donny Von De berk, James Madison, Martin Odergard na Jack Grealish atakuwa last option lakini mtu sahihi kwa timu inayopambania ubingwa ni Donny Von De Berk.

Kuhusu Pereira nilishasema sana humu kuwa alichonacho miguuni mwake kichwani hakipo hili ndiyo linalomfanya ashindwe kutekeleza majukumu yake sawa sawa, lakini anaweza kubaki kama squad player ila siyo regular starter huenda akaimprove hata uzeeni

Kuhusu defence yetu nafikiri ni muda sasa Phil Jones aone aibu walau mwenyewe aamue kuondoka man united maana hakuna timu inayomhitaji hata zile za daraja la tatu kwanini asistaafu tu ?

Bado naamini kwa mwelekeo tunaoenda sasa tuko kwenye right track tuendelee kula mtori nyama tutazifikia hivi karibuni.
likizo yangu imekwisha
  1. phil jones
  2. jesse lingard
  3. andreas perreira
  4. marcos rojo
operation safisha taka taka inapaswa iendelee kwa kuwaondoa watumishi hao wanne (nitamheshimu sana OGS kama atatimiza mpango huu)

kama tutawaondoa hao walinzi wawili hakutakuwa na ulazima wa kutafuta mlinzi mwengine wa kati kwa bei ya gharama kwa sababu chris smalling tunaweza kumrudisha kikosini, vile vile upo uwezekano wa kumtumia luke shaw kama mlinzi wa kati hata kwenye mfumo wa kutumia walinzi wa nne ikitokezea harry maguire anahitaji mapumziko (hakuna lisilowezekana kwa mchezaji professional kubadilishwa nafasi pia references zipo nyingi kama vile david alaba, joshua kimmich, philip lahm na sergio ramos),

ukiachana na ole gunnar solskjaer na benchi lake la ufundi , kiukweli jesse lingard na andreas perreira wameturudisha nyuma sana msimu huu kwenye kampeni yetu ya kurudisha ubora wa timu yetu (ole aliweka matumaini makubwa sana kwa hawa vijana kabla ya ligi kuanza, bahati mbaya wameshindwa kumtihibitishia mwalimu na mashabiki juu ya umuhimu wao wa kuendelea kuaminiwa kikosini)......

kuna kila dalili mmoja wao kati ya hao wawili nafasi yake ikazibwa na mchezaji wa kiengereza japokuwa wapo wageni wenye viwango vizuri kama van der beek na martin ordegaard, kwa sasa ni wachezaji wawili tu ndio wamekuwa kwenye rada (james maddison na jack grealish), sidhani kama tuna uwezo wa kuwasajili wachezaji wote wawili kwa pamoja.

yupi ni bora kati yao msimu huu?
kiukweli sifahamu kwa sababu kwanza sijawahi kungalia mechi za aston villa hata mara moja (labda tumuulize ujugu kuhusiana na grealish) , pia nikiangalia takwimu za maddison nahisi kama kiwango cha utoaji huduma kimepungua sana msimu huu pengine ni mabadiliko ya kimajukumu aliopewa na mwalimu ndio chanzo (sina uhakika)... wanavyosema wadau ni kwamba faida ya jack grealish ana uwezo wa kucheza nafasi tofauti kwa kiwango cha juu.

andreas perreira ana miaka 24 ya kuzaliwa, naweza kusema ndiye mchezaji wetu aliyetumika kwenye nafasi nyingi tofauti bila ya kulalamikia maamuzi ya walimu, alipokuwa spain (granada na valencia) kwa nyakati tofauti kama nitakuwa sahihi alitumika kama winga, aliporudi klabuni chini ya jose alitumika kama double pivot midfield, alipokuja ole amekuwa akipendelea sana kumtumia kwenye mfumo 4-3-3 na pia kama namba 10.

andreas amejaaliwa bidii ya kupambana, solid mentality lakini amenyimwa ubora (quality), hana sifa za kuwa winga bora, hana sifa za kuwa kiungo bora wa ulinzi kama makelele, hana sifa za kuwa kiungo mshambuliaji bora hususani anapokuwa na mpira ndio maana si ajabu kumkuta akiwa na takwimu zisizoridhisha akiwa kama ni kiungo mshambuliaji.

ukiniuliza ni eneo gani bora ambalo andreas anacheza vizuri, jibu litakuwa sijui na sitaki kujua..
ni muda muafaka kwake yeye kutafuta timu isiyokuwa na presha ili apate kujijenga zaidi kwenye career yake ya soka na pia kulitambua zaidi eneo lake sahihi la kiuchezaji, hata kama atabaki msimu ujao nahofia atakuwa na msimu mgumu sana kiuchezaji.

habari njema kwa wote ni kwamba fred ameanza kutoka usingizini japokuwa ana ugonjwa wa kuanguka ovyo kama wilder..
tuliowahi kumtukana fred tukutane hapa tupate kuandaa waraka wa kuunga mkono juhudi za muheshimiwa manywele.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Manchester United wanajiandaa kumuuza kiungo Jesse Lingard, 27, na Andreas Pereira, 24, kwa ajili ya kugharamia uhamisho wa kiungo Jack Grealish,24. (Express)
 
Grealish anapewa hizo sifa kwa sababu ni Muingereza tu.

Kamuangalia vizuri Owen Cantwell, James Madison, Martin Odergard ujaribu kuwalinganisha na huyo Grealish.

Kwnn humkubali J.Grealish?

7goals & 6 assist. Ikiwa anacheza timu yenye hatihati ya kushuka daraja.

Anacheza multiple postions; AM, CM,LW.

Kiongozi uwanjani.



Beggars can't be choosers

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fred leo kupumzika

Kuna uwezekano katikati akaanza Matic, Tominay na BF

Leo lazima tuanzishe kikosi chetu imara, hata kama tutachanganya wachezaji wa second eleven wachache. Tukumbuke Club Bruges sio wabovu kiivyo walitoa suluhu ya 2 - 2 na Madrid kwenye UCL pale Bernebeu

Game ya leo ni a must win game, draw ya 0 - 0 itatufanya tuendelee kuwepo ndani ya mashindano, hata hivyo hatupaswi kuwa na hiyo mentality, tunapaswa kushinda mechi ya leo kwa ajili ya kuvuka na kwa ajili ya kuvuka kwa heshima

Bruno kuendelea kuwa mkombozi wetu? Hilo ni jambo la kusubiri. Ighalo kupewa dakika zaidi na kufunga akaunti yake ya mabao pale United........ Nani anajua

Tukutane saa 5:00 usiku, usiku wa UEFA..... Ni UEFA EUROPA LEAGUE




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu hii game wanaonesha nasikia ni Startimes!

Kwani kuna decoder zingine tofauti na Startimes wataonesha?

Sent using Jamii Forums mobile app
huku kwetu zenji hatujawahi kukosa kuangalia mechi kwa kisingizio cha king;amuzi (zanzibar cable, coconut digital wapo onfire), sielewi hizi kampuni zinapata wapi haki miliki ya kuonyesha hizi mechi (sijui wanaibia?) wakati kampuni nyengine kubwa kama vile dstv, azam wanakosa mamlaka ya kuonyesha mechi.

bein sport
channel+ ya ufaransa zote hizo hamupati kwenye ving'amuzi?
 
Back
Top Bottom