Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mnatozwa buku!!! Sisi kwetu jero
 
Huu ni muda sahihi wa ku-fix matatizo beyond coaching staff, we need to fix all structures starting from players to executives.

Sehemu ya board it's our biggest handicap kwa sbb we're owned by Americans who naturally aren't football-lovers like Brits or Spaniards or Italians, half of the Board comprises of the Glazer family leaving the rest to the suits who run the business. They need to have atleast 3 out of the 12 positions occupied by football minds guide to offer insight on football.

Ningependa sana ktk hizi nafasi 3 za independent directors mbili waingie Fergie na David Gill. Board nzima ya watu 12 hakuna mtu wa mpira pale.
 
Hii kitu ni mbaya sana timu ishakuwa daraja la kati hata wolves hatuwez kupambana nayo.
 
Hata mech ya arsenal alizingua sana alikuwa upande wenu KDB alitumia akili yake tu kuamua mech pale kwenu bila hivyo city angetoa suluhu na arsenal
Mech ya Leo ilikuwa mle mkono first half labda kama umesimuliwa

Naona mna Norwich next week mpunguze machungu
 
punguza jazba.ndio tayari imeshatokea unalia lia nini..?!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana nakataa bora nilienda kuona timu ilikuwa inakosa wachezaj wa tatu muhimu ambapo city alikuwa full
City haikuwa full kwani mpaka muda huu inakosa huduma ya mabeki wao ambao wapo majeruhi na Pep anampanga Rodri na Fernandinho kama mabeki.....yaani beki wa asili alikuwa mmoja tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi wale kina Garry Neville waliokuwa wanamsakama Mou, van gall siku hizi siwasikii kabisa , wanamuonea aibu Ole Masai nini? Wakiangalia kwenye bench kuna team mate Carrick ,

Maisha bila unafik hayaendi
 
HABARI ZILITOKA HIVI PUNDE.
KIPIGO CHA MAN CITY, CHAMFUKUZISHA OLE
HABARI zilizotoka asubuhi hii, ni Ole kutupiwa vilago vyake baada ya Manchester City kumpiga Manchester United magoli ma3 kwa moja pale Old Trafford.
Ulikuwa ni usiku mbaya sana kwa mashabiki wa Manchester United baada ya kutolewa kwenye FA Cup na timu hasimu wanayotoka Jiji moja la Manchester. Goli pekee la United lilifungwa na kinda M-Brazil; Pereirra huku Man City tukiona wakimiliki mchezo mzima kwa kipindi cha kwanza ambapo KDB au De Bruyne akiwa mwiba mkali langoni mwa Manchester United.
Manchester United iliwakosa watu wake muhimu kama vile Scott McTominay na Paul Pogba ambao wote ni majeruhi. Pia Tony Martial alikuwa anatoka kuuguza vijeraha vidogo alivyovipata siku za nyuma hivyo hakuonyesha cheche zake. Meneja wa Manchester United alijitetea hivi mbele ya waandishi wa habari.
Mbali na hapo, Fred Boy mapafu ya Mbwa, yeye alibahatika kucheza nafasi ya DM au tuseme Defensive Midfield (Namba 6) huku Perreira akiua AM - Attacking Midfield na Lingardinho akimaliza CAM as namba 10. Kwa hali halisi unaweza kuona hizi Middle zinaweza kufanywa nini zinapokutana na wababe kama KDB, Fernadinho, Silva nk. Na wakati huo Phil naye alikuwepo uwanjani akizungushwa na kugeuzwa kama chapati na KDBizo.
Baada ya matokeo haya, ndipo uongozi wa familia moja ya Kimasai huko Arusha vijijini uliamua kumtupia vilago vyake ndugu Ole Sendeka baada ya kukataa kumuoa mtoto wa tajiri ng'ombe mmoja wa kijiji kinachopatikana huko Arusha. Ole alichukua vilago vyake viwili alivyoshonewa na mama yake pamoja na begi lake la nguo na kisha kwa masikitiko aliiambia familia yake kuwa watamkumbuka sana.
Tukio hili lilitokea saa sita ya usiku punde tu mechi ya Man U na Man City kuisha. Ole Sendeka ambaye alifika studio za Upepo wa Pesa zilizopo Chato, alikutana na akina Mshana Jr na kumpa mkasa mzima na mimi nikaamua kuuleta mkasa huu hapa JamiiForums.
Asante.
 

Kwenye forum serious namna hii unaleta huu ujinga?

Kweli wewe ni Baharia wa Buza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…