Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Wakasema anakuja mou hapo kwako tukamsubiri na kumpiga wakasema tumebahatisha sababu uwanja wetu wakasema nenda kwa mwarabu tukaenda na kumpiga wakasema ooh sababu ni mji mmoja hakuna ugenini wala nini binadamu akikuchukia kila baya atakuzushia ni sauti ya mlevi mmoja ilisikika
 
Wanaosema kwamba kwa kuwa ni timu za mji mmoja basi hakuna tofauti kati ya mechi ya ugenini na nyumbani hawajielewi

Kama huamini angalia stats za United na City (kila mmoja akiwa nyumbani nani ameshinda sana, na wapi?)

Angalia Arsenal na Tot, au Chelsea au Westsham

Pamoja na mambo ya hali ya hewa kuwa ile ile na timu kutokuwa na uchovu wa kusafiri, lakini idadi ya mashabiki uwanjani inaweza kusaidia timu kuwa na nguvu uwanjani au iwe wanyonge. Hapa kuna watu watasema kama ni mji mmoja hata timu pinzani wanaweza kujaza Uwanja, NO, HAIWEZEKANI. Timu mwenyeji ndio inaamua idadi ngapi ya tickets iende kwa wapinzani na ngapi iende kwa mashabiki wao. Kuna % flani imewekwa na mamlaka msimamizi ili timu pinzani isije kukosa ticket hata moja.
Wakasema anakuja mou hapo kwako tukamsubiri na kumpiga wakasema tumebahatisha sababu uwanja wetu wakasema nenda kwa mwarabu tukaenda na kumpiga wakasema ooh sababu ni mji mmoja hakuna ugenini wala nini binadamu akikuchukia kila baya atakuzushia ni sauti ya mlevi mmoja ilisikika
 
1575900267191.png


a) mechi 11 tumepata point 11.
a1) mechi 5 tumepata point 13

b) mechi 5 tumefunga magoli 10 na tumeruhusu magoli 3
b1) mechi 11 tumefunga magoli 15 na tumeruhusu magoli 16

mechi 3 za mwisho (aston villa, sheffield united na brighton) tumefunga magoli 8 kati ya hayo 15 tuliofunga dhidi ya timu ndogo na wakati huo huo tumeruhusu magoli 6.

kufunga magoli 8 ndani ya mechi 3 si mbaya sana na ni dalili moja wapo inayodhirisha kuimarika kwa safu yetu ya ushambuliaji kwa hizi mechi za karibuni lakini kuruhusu magoli 5 ndani ya mechi 2 si dalili njema kwa safu yetu ya ulinzi.

huyu kirusi wetu (kwa mujibu wa brother fuentte na Darmian ) atarudi lini?
huenda ukawa ndio usajili wetu mpya pale mbele.
ndiye mwanadamu atakayeusambaratisha mjadala unaowahusu jesse lingard na andreas perreira.

mara paaap pogba anarudi uwanjani lakini bwana ole anamrudisha namba 8 kama ilivyokuwa mechi za mwanzoni.
ndipo nitakapoamini hata wazungu wana roho mbaya
 
tuchukulie hivyo hivyo unavyotaka wewe ya kwamba leicester city ni upepo wa kisulisuli,

timu bora haijengwi kwa mwaka mmoja kama tutatumia reference za team nyenginezo kama liverpool ya klopp (kwa siku ya leo sipo kabisa kwenye huu mjadala wa kujenga timu imara ya muda mrefu itakayoturudishia nyakati za furaha kwa sababu nafahamu fika tumekosa football heritage hivyo basi tutahitaji uwekezaji mzuri wa wachezaji wenye kuendana na mfumo wa mwalimu aliepo pamoja na muda kama ulivyozungumza na hilo tumeshaanza kuliona baada ya kushuhudia uwekezaji wa wachezaji wote watatu walioletwa na mwalimu wanafanya vizuri sana na baadhi yao pia wakiondolewa mfano fellaini ambaye si mchezaji anayeendana na philosophy tulioizoea pale carrington na wengineo wataondolewa)

lakini huo ujengaji wa timu bora isiwe sababu kuu ya kuamua kujitoa ufahamu kwa makusudi pale timu inapofanya vibaya, wewe jenga timu yako lakini hakikisha timu inaendelea kupata matokeo yenye kuridhisha na ndio maana kwa kulifahamu hilo uongozi wa man utd kwa kiasi kikubwa sana japokuwa hawajaliweka hadharani wamewawekea makocha kipaombele kikuu cha kuhakikisha timu angalau inapata tiketi ya kushiriki UEFA kila msimu (hatuna uwezo wa kushinda ubingwa basi hata UEFA ndio itushinde licha kufanya uwekezaji mkubwa kila mwaka)

achana na mlango wa europe league na utapataje tiketi ya uefa kama utashindwa kuzifunga timu ndogo ambazo ndio nyingi?

kama nipo sahihi
tumepata alama 14/18 dhidi ya timu kubwa (well done)
tumepata alama 10/30 dhidi ya timu ndogo (poor, poor, poor)

tunachohitaji ni kuiona nguvu ile ile yenye kuambatana na nidhamu ya uchezaji kwenye mechi kubwa pia tunaitumia kwenye mechi ndogo na mwenye wajibu wa kulisimamia hilo ni mwalimu hata kama yeye si mchezaji wa uwanjani ila kumbuka mtoto anapokosa nidhamu mtu wa kwanza anayepaswa kuangushiwa lawama ni mzee ndio maana mwisho wa siku anayetimuliwa kazi ni mwalimu na si wachezaji.

=============================================
brendan rodgers ameanza kufanya kazi february 2019 pale leicester city.
ole gunnar solksjaer ameanza kufanya kazi december 2018 pale man utd

kwa nini leicester city wanacheza vizuri zaidi ya man utd
kwa nini leicester city wanapata matokeo mazuri zaidi ya man utd.

tunapaswa tujitofautishe na blackburn rovers ya damien duff (wazee wa kukamia mechi kubwa)
Unadhani kwa wachezaji hawa hawa man utd ingekuwa na Brendan Rogers kama Coach je,ingekuwa kama Leicester city?.
 
Kusema ukweli ari ya upambanaji ipo juu mno kwa United kwa sasa....

Kutopoteza dhidi ya timu 6 za juu EPL sio kazi ya kitoto na kwa hili nampa heko sana Ole Sendeka maana anafanya kitu ambacho Unai ameshindwa fanya pale Arsenal...kuamsha marali ya upambanaji kwa wachezaji.

Ukiangalia kwa makini utaona timu nzima,wanapambana kwa kila hali kwa kazi chafu na safi....

Napenda DJ na Scott wanavyojiamini utasema ni 25's players kumbe bado sana.

Nilicheka sana lile buti alilopigwa Stearing na Perreira ndio maana halisi ya HAINA KUFELI....

Bigup
Ole hana tabia ya kukandia au kutumia lugha yenye ambiguity kwa wachezaji wake, napenda anavyo wakumbatia wachezaji wake kila baada ya game.

Angalia anavyomzungumzia pogba..inawezekana akamuuza bila hata kumtupia neno ovu. Hakumpenda fellain na Sanchez na lukalu sio kwa sabb hawajui,lkn kwa sabb ya ufaza, kama mafaza vile. Ole hamfanyii mtu kazi, anafanya kile anachikiamini

Ni muongeaji sio mlalamikaji. Ole hana stress hicho kinamfanya asipanic hovyo. Kingine ole hana komedy hata kidogo. Utani ule wa kawaidaaa sana. Ni kama Ferguson.
By so doing hata wachezaji wake hawana na hataki upuuz wa mazoea mabaya, pogba anapenda upuuuzi, anachezacheza lkn angekuwa na sura ya ole angekuwa mtu bora duniani
 
Back
Top Bottom