Jicho langu mechi ya jana
Team selection ya OGS especially kwa Phil Jones ilikuwa ya kiboya. Why not Axel, why Jones?
Kucheza na timu inayo defend sana, tena timu mbovu (underdog) kwa mfumo wa 3 - 4 - 3 ni uoga
Maguire na Lindelof kati bado hawajawa solid kama watu wengi tulivyotegemea wakati msimu ulipokuwa unaanza. Tukiimarisha kwa kusajili defensive midfielder na ukabaji ukawa huo huo, tutakuwa na haki zaidi ya kuwalaumu, kwa sasa tuwe wapole
Brandon Williams is a real deal, mwanzo ali panic kidogo kutokana na kelele za mashabiki wa the Blades, lakini baadae akatulia, naamini hata angecheza Shaw hali ingekuwa hiyo hiyo au mbaya zaidi. After all amefunga goli muhimu sana, goli la kwanza
Pengo la Tominay limeonekana, Pereira akiendelea hivi msimu huu utakuwa wa mwisho kwake, Martial kama kawaida yake, anacheza vizuri timu nzima inapocheza vizuri, timu ikiwa haina mpira muda mrefu anapotea. DJ ni Mr. Reliable kwetu, he is the signing of the season kwa EPL yote, Mason in two years atakuwa juu ya Rashy na Martial wakati kocha anapanga kikosi chake
Positives.
Tukiwa na midfielders wote ambao msimu ilipoanza hawakuwa first teamer, tumeweza kucheza vizuri especially second half.
Tukitajwa kuwa tuna forward mbovu kabisa katika timu za top six, tumeweza kuitoboa mara tatu timu inayotajwa kuwa haijawahi kufungwa goli zaidi ya 2 kwa muda mrefu sana (hakukuwa na goli la penati safari hii)
Come back spirit ni Positivity nyingine.