Al Watani
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 21,697
- 32,447
Ole ni Oldfashioned manager anapenda defenders wanaoweza kukaba tu inasikitisha sana Man united ilishindwa kumsajili Trieppier au Thomas Munier wakaamua kutupa pesa kwa huyu AWILO LONGOMBA.wan bissaka ameendelea kuwa useless kwenye kupandisha mashambulizi kama kawaida yake, siku tutakayopata mwalimu mwenye fikra za guardiola au klopp basi tutaingia tena sokoni kwa lengo la kutafuta mlinzi mwengine wa kulia, ina maana tutakuwa tunaendeleza tabia ile ile ya kusajili wachezaji kwa kuangalia zaidi mzuka wa mwalimu.
ndio maana tetesi zake za usajili sikuzifurahia kwa kiwango kikubwa sana.
bora ashley young kuliko wan bissaka kimchango kwenye kupandisha mashambulizi, timu inasumbuliwa na tatizo la kukosa wachezaji viungo walio creative jambo linalopelekea utatu wetu wa mbele uonekane butu lakini cha kusikitisha jamaa pia na yeye wala haleti faida kutokea pembeni, waangalie liverpool wanavyofaidika na walinzi wao wa pembeni muda wote wa mchezo.
wan bissaka benchi, brandon williams on ili ashley young arudi upande wa kulia
hivi timu yetu inafanya mazoezi ya kumiliki mpira pindi wachezaji wanapokuwa kwenye presha, mbona tunabutua mipira ovyo kama vichaa?
Hana msaada timu inapokuwa na mpira na anapokaba lazima autoe nje au abutue tu.
Last week nilitaka kuandika humu kuwa kwa Wana Bissaka Crystal Palace walituibia.


