Issue ya Majeruhi Ni more than kocha, niambie mkuu kocha gani wa man U baada ya Fergie ambaye Hana janga la Majeruhi, Hilo Ni tatizo kubwa linalohusiana na structure ya Timu kuliko kocha. Fergie alikuwa na jopo la makocha 24, Sasa Hivi benchi la ufundi Ni Dogo Sana.
Unasema United ime improve defense sababu ya uwezo individual na sio kocha, je hao wachezaji wamenunuliwa na Nani? Hivi watu walikuwa hata wanamtaka AWB? Ole ametuaminisha Ni mzuri na Kuna watu walikuwa Hadi wanaponda Bei yake humu Ila Nani Sasa Hivi anaweza pinga usajili wake? Wangapi wakisema anunuliwe yule beki wa psg? Wangapi walisema anunuliwe wa Norwich?
Pia mkuu napingana na wewe kwamba martial na Rashford wamecheza vizuri zaidi enzi za Mou na lvg nakupa stats.
-kwa Mara ya kwanza Rashford amefikisha double digits goals kwenye ligi Ni msimu uliopita chini ya ole hajawahi fikia hio figure chini ya Mou Wala LVG amefunga goli 10 vs 7 ambazo ndio nyingi zaidi chini ya Mou.
-kwa Mara ya kwanza Rashford amefikisha assist 6 kwenye ligi ambazo hajawahi fikisha nyingi zaidi Ni 5 msimu wa Mou.
So niambie wewe mkuu, goli 10 na assist 6 ndani ya nusu msimu wa ole ndio Bora zaidi kwa Rashford kuliko misimu yote unaanzaje kusema kacheza vizuri zaidi misimu iliopita?
Tuje martial.
Martial chini ya Mou hajawahi fikisha goli 10 Ila chini ya ole amefikisha na chini ya LVG ana goli 11 hivyo lvg alimtumia vizuri zaidi martial kuliko wote na Ole Ni wa Pili, Ila ukiangalia zaidi msimu uliopita ole hajafundisha wote Ni impressive maana amefikisha goli zaidi ya za Mou kwa muda machache zaidi.
Na hata ukiangalia martial msimu huu amecheza mechi 3 tu lakini ana goli 2 na assist 1 tayari inamaana Ni average contribution 1 kwa kila mechi, huwezi kuwa serious ukasema martial anacheza vibaya zaidi chini ya ole.