Paul Scholes anatajwa kuwa miongoni mwa viungo bora kuwahi kuchezea ligi ya malkia,kila mtu anamtolea mfano kama kiungo bora kwa kuwa kipindi chote ambacho amekuwa mchezaji,na amekamilika idara zote. Anakaba,anashambulia,anapandisha timu kwa wakati na hakuwa na maneno mengi uwanjani (inasemekana ni mtu wa aibu sana) Hakuwa na madoido ya kupiga chenga na tobo sana ila first touch zake zilikuwa na uwezo wa kubadili upepo wakati wowote.
De bruyne kwa namna nyingine anauchezaji unaoendana na wa scholes kwa kiasi kikubwa. Kiujumla wanaendana mambo mengi sana ndani na nje ya uwanja. Tena kwa uchezaji wa city hii ya guardiola,jamaa anatoa assist nyingi kuliko scholes.
Ukirudi kwa kiungo wa Manchester united Paul Pogba,ubora wake umekuwa katika kushambulia zaidi,ana msaada mdogo katika kuzuia,anachezea sana mpira hadi wapinzani wanajipanga vizuri kuzuia,kupiga chenga zisizo na maana,ubora wake unategemeana siku na siku,achilia mbali tabia yake isiyoridhisha kama taswira kwa wenzake.
Huwa napata wakati mgumu sana kukubaliana na mashabiki wanaosemea kuwa pogba ni bora kuliko de bruyne wakati huo huo wakimtukuza scholes kuwa ni kiungo bora kabisa ndani ya EPL,kigezo chao huwa ni nini haswa? De bruyne ni copy na paste ya scholes anayekubalika kwa kazi yake lakini wakati huo huo wanaona pogba ni zaidi ya huyu de bruyne!
Inawezekana tumetofautiana katika kuangalia ubora wa mchezaji lakini ubora wa pogba unapimwa kwa vigezo vipi hasa? Hoja ya kujifichia ni watu wanaowazunguka katika timu zao,lakini hiyo haimaanishi mchezaji kupoteza mipira katika mazingira rahisi kabisa,kutokukimbia uwanjani na kadhalika. Hata alipokuwa juventus na timu ya taifa,pogba amekuwa katika kiwango cha kawaida kabisa na huwezi kumlinganisha na de bruyne.
Mimi ni shabiki wa kutupwa wa Manchester united lakini ninapenda wachezaji wazuri bila kujali wanacheza timu gani.
Wakati wa utawala wa mourinho pale Trafford, Scholes aliwahi kusema kuwa "the problem of Manchester united is first Paul pogba and then mourinho",watu hawakumuelewa.