Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kwanza mshahara wa Sanchez sio mkubwa Kama unavyoripotiwa. anapata hizo Hela nyingi ikiwa hio wiki Kuna Uefa na akacheza (25% bonus toka mshahara), na pia akicheza mechi 2 kwa wiki (75K appearence). Ila akikaa benchi bila kucheza mshahara wake Ni chini ya 300K, ndio maana de Gea moja ya masharti ya kubaki man UTD alitaka awe highest paid player, na mkataba mpya Ni 300K ama 350K.

Pili inter wanalipa zaidi kuliko sisi, man UTD watalipa 6M ya mshahara wake na inter watalipa 10m.

Tatu hakuna clause kwenye huo mkopo hivyo akimaliza mkopo wake hata Kama atacheza vizuri sisi tutakuwa na advantage ya kutaja transfer fee tunayoitaka.
 
Na Ed atafanya hivyo ili abaki msafi.

Mimi sioni Ole akitoboa kabisa kwa hii timu.

Labda tusubiri kuona Fred anarudi katika hali gani,bado timu ni kisanga.

Tuko vizuri nyuma tu,na ikitokea AWB anapata majeruhi tunarudi kuleee.
Hatujapata majeruhi tupo hivi tukiyapata itakuwaje? Sijui.

Tatizo sio kuwa na depth ndogo ya wachezaji, hata hao wachache hawana hizo quality za kuwa hapo.

Liverpool nao wana depth ndogo ila wanaitumia vizuri sana.

1. Hatuna quality players.

2. Hatuna kocha mwenye quality ya Man Utd.

3. Hatuna management supportive. Hakuna DoF, hata akija kocha mwingine ataleta squad yake yote mpya na kufukuza hawa waliopo.
 
MAJIRAN VIPI TENA ,AU NDIO SAFISHASAFISHA IMEANZA...KAMA TUNAVYOFANYA SISI, ...MWENYE MAGARASA SI ATABAKI CHELSEA PEKE YAKE SASA

Chris Smalling to AS Roma from Man United, here we go! Total agreement for a simple loan (€3M to Man Utd) without buy option. The player has accepted.
#MUFC #Roma #transfers
 
Ole at the wheel
 
Sio wanne tu, Chelsea haina quality players wakupambana hata na Everton, Leicester , wolves , achilia big 6, Ollachuga anajifariji tu, ila hakawii kujipiga Ban ,

Ukweli Chelsea kupata point kiuhakika ni kwa timu zilizopanda daraja tu, ukimuangalia Burney ,wolves ,Leicester , Watford ,Everton , hata astonvilla unaona kabisa Chelsea hawez kuchukua point kwa hao kirahisi .

Ndio maana kabla ya msimu niliwaambia Chelsea wakikaza watamaliza nafas ya 10

Wakikubali vipigo ovyo bas watakuwa wanagombania nafas ya 15 .

Chelsea wanamtegea William ambaye hana historia ya kuvuka magoli 5 kwa msimu, toka aanze KUCHEZA, ni Mara moja tu alifikisha goli 8.

Wanamtegemea Abraham ambaye game tafu kama za kina wolves , Everton , itakuwa ngumu kuwabeba , tukija beki yao inavuja , ndio maana mpaka sasa wameruhusu goli 7 ,

Muda utaongea zaidi
 
Jesse lingard is a fuckest player he can’t even make a bench at spurs,city,Liverpool...That’s why Man Utd we are far away from the top 4..Scott Mctommy can’t even start at Leicester city but he’s a regular starter at Man Utd.
 
Hapo kwenye beki kuna vituko sana.. timu ambayo haitapata magoli kwa ukuta ule basi wajitathmini.
 
Lukaku hajawahi kuwa deadwood kwenye premier league stats ziko wazi ,the issue ni OGS hamtaki

Namkubali OGS anavyoendelea kufanya clearence but alipaswa kuwa na altenative/short time altenative especially kwenye foward it will be disaster kama key 3 players wakipata majeruhi hali itakuwa mbaya sana.Currently Martial ni majeruhi ikitokea Rashford nae akapata injury ni disaster.United ilipaswa kusajili backup striker
 
Mkuu mlaumu Woodward, ole wachezaji wake aliowataka hawajakuja sio kosa lake. Tume flirt na dybala, mandzukic, Bruno, longstaff na wengi tu mwisho wa siku hajakuja yoyote.

Na Lukaku msimu wa pili kacheza mechi takriban 45 na goli 15 na performance yake haikuridhisha na mwishoni akazidi kubweteka. Kwenye Uefa ana goli 2 ambazo zote kafunga mechi ya psg, jumla ya mechi alizocheza Ni 9. Mimi pia nampenda Lukaku lakini Kuna vitu anafanya vya kijinga Sana.

1. Ameongezeka kilo Hadi kufikia 104, Hivi mchezaji gani unajisahau kiasi hiki? Watu walidhani Garry Neville anatania lakini medical za inter zilithibitisha jamaa ana kilo 104. Angalia hii picha Lukaku anakuja Man U na anaondokaje, alikuja Kuna utofauti wa tumbo na kifua anaondoka bila huo utofauti.


2. Kuvujisha data za mazoezini, na kujinadi kwamba yeye ana speed.

3. Kuwapiga vijembe wachezaji wenzake Twitter Kama alivyomponda martial kwa kutochaguliwa kombe la Dunia etc

Unaweza kuangalia full article Hapa
 
kepa hamna goal keeper hapo
 
sawamk&nd*kuw*ka
 

I know players anaowataka OGS ni ngumu kuwapata hana ushawishi sana na timu haiko Champions League but alipaswa kutafuta short time solution kulikuwa kuna free agent wengi ambao hawahitaji mishahara mikubwa na wangesaidia kwa kipindi hichi (LLorente,Ribery,)tatizo timu ikifanya vibaya Woodward/Glazer hawatamwacha watamfukuza

Issue ya uzito ni propaganda za Waingereza (GNeville ndio alianzisha story), mashabiki wamekuja kumchukia baada ya yeye kuanza kujibu hizo shutuma.Luke Shaw misimu karibu yote tangu atue United ni overweight but huwezi kusikia kina GNeville wanamponda sababu ni kijana wao.Pogba alivyokosa penati GNeville alianza kumponda but alivyokosa Rashford akabadilisha gia

Lukaku amechemsha United last season sababu makocha wameshindwa kutengeneza mfumo wa kumfanya afunge magoli mengi,Hatuna wingers wanaopiga krosi na one of the streghth za Lukaku ni mipira ya juu na muda mwingi alikuwa anakuwa isolated peke yake

Game ya away against PSG Lukaku alidhihirisha anaweza kucheza formation ya OGS (4-3-3) I think ulimuona alivyo-press.The same player ambaye ana 104 kg alikuwa akicheza Belgium anafunga magoli (kuanzia 2018-2019 kacheza mechi 16 kafunga magoli 17)
 
Kwani Ole mlichaguliwa na nani?
 
Garasa Luiz tumeliondoa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…