Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Halafu tuclarify kitu kimoja Hapa.

Academy inasajili wachezaji na sio wazazi wanapeleka wachezaji kwenye academies.

Hao wachezaji wa zamani unaoona watoto wao wapo city Ni sababu hawana viwango, vya kuingia United, mfano mzuri Harvey Mtoto wa Neville alitrain kwenye academy ya city, alipokuza kiwango mwaka Jana ndio amekubaliwa kujiunga na academy ya man UTD.

Ingekuwa wazazi wanapeleka watoto wao academies basi watu wenye hela ndio watoto wao ungewaona academies kubwa duniani.
 
Unajua niaje.. Mashabiki tunaongea sanaa yani..
..ila Mbivu na mbichi zitajulikana kesho kutwa..
 
1. Fergie hakumuacha asepe, mwenyewe kwenye kitabu chake anasema alimfuata Evra akambembeleze pogba asiondoke, na Evra Kama rafiki wa karibu wa Pogba pia amethibitisha hili ukitaka ushahidi nitatoa mpaka page za kitabu.
Alirudi MUFC kwa sababu ya mapenzi yake ya Club na aliondoka MUFC kwa sababu ya Mapenzi yake kwa Club, au sio? Yaani mpaka anabembelezwa bado kaondoka halafu unatwambia ana mapenzi ya Club.

Yap Mina Raiola alisema ivi au sio

"
‘For me I have been for three years in Manchester and have been doing great, some good moments and some bad moments, like everybody. Like everywhere else. ‘After everything that happened this season, with my season being my best season as well… I think for me it could be a good time to have a new challenge somewhere else. I am thinking of this: to have a new challenge somewhere else.’

"
3. Halafu we Jamaa wa ajabu Sana, nimekutajia wachezaji zaidi ya 20 wa academy ya man U wanaocheza Timu mbali mbali ligi ya Uingereza, wewe umeshindwa kutaja hata mmoja halafu unakazania Man U wanabebwa na Media,
- Kasper Schmeichel - Leceister
- Angelino - PSV
- Ben Mee - Burnley
- Jason Denayer - Lyon
- Kirena Trippier - Tottenham
Just to name some...

As i said, ishu ya Man city ni kutowapa makinda mda uwanjani.

Kama unajua unajua tu na uutakapoenda uta perform vizur? Coutinho aliperform vizuri Liverfools, kaenda Barca tafrani tu. Hii Logic ni nonsense.... kwamba eti kama unajua unajua tu?
 
Uchambuzi mzuri sana
 
Kwa hio unatwambia kuwa Academy kazi yao kusign players TU, sio kwamba ni shule ile unapeleka mtoto wako akiwa mdogo anajaribiwa na kutizamwa kama kuna potential yoyote ya kisoka? - Ofcourse sio bure-

Kwaio City walimsign mtoto wa Neville, walimsaign mtoto wa Van persie na sio kwamba hawa waliwapeleka watoto wao huko?
 
Hapo hatujagusa class of 1992
 
Mbona hutaji mifano mzee

Tema fact, tuache maneno

Mimi nimetaja, taja wewe hao machachari machachari walio juu ya level za akina Rashford ambao wametoka City

Facilities za City ndio zinakutisha, sisi Tunaangalia product
 
Ndio academy Ina scout na kusajili na sio unapeleka tu mtoto na kukubaliwa hasa kwa academies kubwa.

Na hao watoto walienda kutrain (hawakusajiliwa)
 

Watano tu mkuu? Nimekutajia 26 toka academy mbovu, wewe academy nzuri umepata watano tu? Tena Hakuna hata mmoja ambae unaweza sema Ni world class.
 
Unaweza kututajia hata mmoja ?
 
manchester united ni bora wafanye mipango ya kuanzisha kikundi cha ulinzi shirikishi, timu ina walinzi 13 lakini ni walinzi watatu tu ndio wana muelekeo wa kupata namba kikosi cha kwanza kwenye timu kubwa kama vile manchester city na liverpool.

  • vidic, ferdinand, jonny evans, brown (kiraka), oshea (kiraka), neville, evra.​
  • maguire, smalling, jones, bailly, lindelof, rojo, darmian, dalot, young, tuanzebe, shaw, bissaka.​
tokea dirisha la usajili halijaanza mpaka limemaliza kama tungelikuwa tunatafuta mchangiaji asiyekuwa na chembe ya uoga wa kusimamia anachokiamini basi kura yangu ningelimpa bwana PTER .

Nimesikia tetesi zinadai ya kwamba FA wameamua kuiongezea muda wa kufanya usajili klabu ya manchester united kwa sababu CEO ed woodward alikuwa na likizo ya kazi kwa takribani wiki mbili.
 
mkuu nimeielewa hoja yako unayoisimamia ila sielewi kwa nini hao wengine wameshindwa kuielewa hoja yako.
umejaribu kuizungumzia man city hii ilioasisiwa miaka 10 iliopita na sheikh mansouri na si ile ilioasisiwa takribani miaka 100 iliopita.

man city hii iliosisiwa miaka 10 hata mimi nakubaliana na wewe ya kwamba wamewekeza miundo mbinu bora sana kwenye sekta ya kusaka vipaji na kwa hali inavyokwenda ndani ya miaka 10 ijayo upo uwezekano wa ndugu hawa wawili kuwa level moja au kaka mkubwa kuzidiwa kwa uzalishaji wa wachezaji kutoka shule wanazozisimamia.

jadon sancho = dortmund
brahim diaz = real madrid
phil phoden = mrithi wa david silva
denis suarez =
amerudi barcelona kutoka arsenal
iheanacho kelechi = leicester city​
 

Kuna baadhi ya wachezaji upande wa ulinzi wana uwezo wa kucheza nafasi ya kiungo.
1.Timothy Fosu Mensah
2.Diogo Dalot
3.Phil Jones
4.Ashley Young
 
Kuna baadhi ya wachezaji upande wa ulinzi wana uwezo wa kucheza nafasi ya kiungo.
1.Timothy Fosu Mensah
2.Diogo Dalot
3.Phil Jones
4.Ashley Young
mkuu kucheza kwao kiungo si tatizo ila cha kujiuliza wanafikia matarajio ya sehemu husika wanazocheza?
chukulia mfano mdogo wa fabinho ana uwezo wa kucheza kiungo mkabaji kwa ufasaha, ana uwezo wa kucheza mlinzi wa pembeni kwa ufasaha vile vile zipo baadhi ya mechi amecheza mlinzi wa kati pale liverpool kwa kiwango kizuri kuliko cha bwana jones.
hao wa kwetu uwezo huo wamebarikiwa kuwa nao?
=======================================================================

baada ya kufungwa magoli manne na everton
"some of these players won't be here next season" = ole gunnar solskjaer 🙂🙂🙂
kumbe kilaza alikuwa ni lukaku peke yake?
 
Plastic fans Hao achana nao
 
But for me, I'm very confident that we'll get goals from Anthony Martial, Rashford... Dan James will come in and create, Jesse Lingard will get more.
msimu uliopita marcus rashford na antony martial kwa pamoja wamefunga magoli 20 kwenye ligi kuu ya uingereza kama nitakuwa nipo sahihi.
ili tusolve tatizo la ushambuliaji mabwana hao wawili watalazimika kutufungia magoli takribani 40 kwenye mechi 38.
je uwezo huo wanao?

naomba tuzungumze mambo ya soka tukiweka mbele uhalisia na si matumaini ya uongo ya kumpa ahueni mgonjwa mahututi aliyebakisha nusu saa kabla hajakata roho.

nilisema na nitaendelea kusema timu yetu tulipaswa kwanza tuongeze mshambuliaji mwengine atakeyetufanya tuwe na safu kali ya ushambuliaji kama waliokuwanayo liverpool au man city, tulichokifanya sisi ni kumuondolea mgonjwa kifaa kilicho chakaa cha kumsaidia kupumua bila ya kuwa na mipango ya kutafuta kifaa chengine.

sielewi kwa nini timu tajiri kama manchester united wanazidiwa na klabu ya arsenal kwenye harakati za usajili wa mchezaji hodari kama pepe, jamani huyu pepe alipaswa aje manchester united ili aongeze nguvu safu ya ushambuliaji na si arsenal. nyakati za SAF nimewahi kushuhudia timu yetu ikiwa na washambuliaji wanne mahiri kwa miongo miwili tofuti, sielewi kwa nini nyakati hizi imekuwa ngumu.
andy cole + dwight yorke + sheringham + solskjaer
nistelrooy + rooney + saha
rooney + tevez + berbatov + ronaldo
rvp + rooney + hernandez

leo hii tunaianza ligi tukiwa na mshambuliaji asiyekuwa na uhakika wa kufunga magoli 20 kwa msimu halafu kuna wadau wanajipa matumani ya uongo eti tutafanya vizuri.​

kuna wadau wameshukuru kuondoka kwa lukaku huku wengine wakimdhihaki kwa sababu ya mwili wake kuwa na uzito mkubwa akiwemo gary neville, lukaku huyu mzito mwenye kg 300 ana uhakika wa kukupa magoli 20 kwa msimu haijalishi timu ipo kwenye kiwango kibovu kama ilivyokuwa msimu uliopita.

kupitia kurasa hii mutakuja kumuomba radhi romelu lukaku kwa aibu na fedheha itakayowakumba.
mume wetu wa soka wolverhampton anatusalimia​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…