Akachukua Champions League 3 na Atletico kachukua 3? Labda swali hili ndio litakwambia tofauti ya izo timu mbili.
Kwaio hapa tunaona Star ambae alikuwa akicheza kwa determination, na sio POGBA anaedai mishahara tu.
Tatizo lilikuwa nini sisi kutokufika nusu final miaka sita hio?
Kwaio mashine zimekuja izo, hebu nambie tatizo lilikuwa nini hata tukose mafanikio? Kwanini mashine hizo zikienda kwengine zina perform fresh?
Fact is at that time, EPL big teams zilikuwa ovyo tu. Kama aliweza kujenga kikosi cha ushindi anashindwaje kutengeza chengine basi kama wao wanategemea kukuza wachezaji ndio watese England.
Mkuu pengine hii comment yangu ya mwisho kwako.
Tatizo kubwa la watanzania na Binadamu wengi huwa tunaangalia mafanikio pale yanapotokea na hatujishughulishi kujua yametokea vipi, nitakupa mfano mzuri man UTd ya 2008, moja ya kikosi Bora kupata kutokea. Baada ya mafanikio ya 1999 timu yetu ilidrop na ulaya tukawa tunafanya vibaya Sana na kuna muda Fergie alikuwa anazomewa, kipindi Fulani Arsenal Invicivble na Mou miaka 2 mfululizo anachukua ubingwa huku sisi Hata kuvuka makundi Uefa ni Tabu. Hadi mashabiki walikuwa wanazomea wanataka Fergie Afukuzwe.
Lakini at that time tulikuwa tunajenga kikosi upya walisajiliwa wachezaji Hawa
1. Rooney kitoto Cha Everton
2. Ronaldo kitoto chengine Toka Sporting
3. Nemanja vidic beki asiyejulikana Toka spartak Moscow
4. Patrice Evra
5. Ji sung park (Evra na park kidogo walikuwa wanajulikana lakini still huwezi kuwaita ma super star at that time)
6. Carrick etc
Hao wachezaji around 2004 mpaka 2006 walikuja plus watoto wengine waliokuwepo Kama Rio Ferdinand,
Strategy hio ilikuja baada ya strategy ya kununua ma super star kufeli, kabla ya hao tulinunua masuper star Kama
1. Juan Sebastian veron fundi wa Ki Argentine
2. Kleberson mshindi wa world cup 2002
3. RVN
4. Fabian bhartez
5. Laurent Blanc etc
Hivyo mkuu huo ni mfano halisi Toka Man United kwamba kununua machine hakujengi tu kirahisi timu Bali unatakiwa kuanzia na squad players kwanza.
Baada ya hao kina Evra na park na timu kukaa sawa tukai re enforce na masuper star akaja Tevez, Hargreaves, Anderson etc
Sio man U tu naweza kupa mifano ya Timu nyingi, Barcelona walivyopoteana alienda LVG pale decision alizofanya aliblock mauzo ya watoto Kama puyol, Valdez, xavi, iniesta etc hao walikuwa Hata hawajulikani, akawa anawapiga benchi kina Rivaldo, Leo ukiona Barcelona wanasajili Suarez ama coutinho unadhani Wana mafanikio sababu hio unasahau struggle walioipata miaka kadhaa iliopita.
Same kwa Bayern hicho hicho kilitokea.
Kama nilivyosema comments za juu Hata uwe na Ronaldo na Messi Kama hauna Backbone ya Timu haisaidii, unamuona Messi na Aguero Argentina? Si wazuri wale mbona wanaflop? Masuper star wanakuja baadae baada ya kutengeneza timu.
Wachezaji tuliosajili msimu huu ni wazuri na Kama tunapata hao ambao tetesi zinasema wanakuja Kama Bruno, Ben Yedder, Maguire etc wote ni squad players wazuri watatu improve.