Kwenye hoja ya kwanza nipo na wewe 100%, ni ujinga kulazimisha mchezaji abaki na wakati yeye hataki kubaki, japo timu nyingine ni ving'ang'anizi mfano Klop aliwahi kulazimisha Lewandosk abaki pale Dortmund, Bayern wakaja wakamchukua bure

Kwenye suala la pili, ni kwamba ni kweli potential na proven players wamefeli pale United. Swali ni kwamba ni bora usajili mtu kwa £50mil+ halafu a flop au usajili kwa £12mil ili hata aki flop iwe hasara ya kawaida na atafutwe mchezaji mwingine?

Na point yangu ya msingi, United hawana utamaduni wa Galacticos, na tulivyo adopt huo utamaduni mambo ndio yakawa mabaya zaidi, kwanini tusiende back to our roots?

Guys, kilichotokea MUFC sio Galactico signings, binafsi sijaona wachezaji walokuja MUFC ndani ya miaka sita tangu aondoke Ferguson ambao unaweza kusema kuwa ni wachezaji moto. wachezaji waliokuja ni wazuri ila sio wakupewa sifa ya ki galactico.

Mkuu, kwa mimi (Nazungumzia mfano ningekuwa manager) wote wa 50 na 12 million, si expect waje kuflop. Yaani mmoja akiflop, regardless of their price tag ujue basi kuna tatizo, ama hakustahiki kununuliwa kwa pesa izo na alikuwa over priced ama nimeshindwa kumdevelop, ama nimebuma mimi kumnunua mchezaji sie. Ata Fergie makosa haya yalimkuta.

Tatizo letu tumekuwa tunanunua wachezaji for the sake of signings.

Sipingi kuleta vijana kuja MUFC, lakini tunampa mkataba Young na kumuacha herrera, miaka nenda miaka rudi tumeona Jones na smalling hawatufai ila bado wamebaki Club!.

Halafu inawezekana hamukunielewa, mnafikiria kama mimi nataka tununue ma stars tu, mimi nataka wachezaji wenye experience na wanaojua kazi zao. Mtizameni Pep alivojenga timu, mpe milioni miliono 100 atakuletea wachezaji wawili ambao in a very short time wanakuwa tishio.
 
Your manager
IMG_20190708_171700.jpeg
 
Mkuu sidhani Kama mazoezi anapanga kocha mkuu, timu Kama man U kunakuwa na jopo la zaidi ya watu 10 ambao Kila mmoja ana specialize kwenye kitu chake.

Na kitu kimoja ambacho mashabiki naamini tunaafiki ni kwamba timu yetu haipo fiti, wanahitaji kuwa fit zaidi kuliko kitu chengine chochote, mtu kama phelan naamini ana uzoefu na knowledge ya kutosha ku oversee Jambo Kama Hilo.

Tumuachie kocha afanye kazi yake maana yeye ndio mtaalamu, hao waandishi wa habari wanapenda tu kuandika vitu negative ili wapate attention,
 
Unapokuwa unatuambia "Your Manager" unakuwa kama unatutukana..as if sisi ndo tuliomuappoint..

Stop that man
Nyie ndio mlie msapoti since day one, you were so busy singing Ole's at the wheel when he was beating relegation folders.
 
Youri tielemans amereja jumla Leicester kwa pauni mil 40..... jamaa alikuwa decent sana, deal zetu sijui huwa zinakwama wapi...... Inafika kipindi naomba hata hao waingereza waje tu huenda tukalamba dume la kupata Carrick mpya na Lampard mpya......
 
Sioni shida kwenye hilo

Msimu uliopita wakati wa Jose, United ilikuwa top 5 ya timu zilizokimbia kidogo uwanjani/wavivu. Kiufupi physically hawakuwa fit

Unadhani ni wakati gani kocha atautumia kuwaweka wachezaji wake timamu kimwili? Ligi itakapoanza?

Kuna zaidi ya mwezi wa timu kujiandaa, lazima kuna wakati timu itafanya mazoezi ya kucheza mpira, kufanyia kazi formation n.k.

Kukosoa kila kitu hakutasaidia timu. Timu ameshapewa OGS, tumpe benefit of the doubt. Aliomba sana pre season, sasa wakati wake ni sasa. Mwisho wa msimu tuone kama ametusogeza mbele, tupo pale pale au ameturudisha nyuma

Yote haya yanategemeana pia na wachezaji atakaopatiwa na Ed
 
VVD hana pace????sio hana pace sema ni mara chache inatokea yeye kuhitaji kukimbia kutokana na defense yake nzuri.Na pia si kawaida kuona beki wa kati anakimbia kimbia maana wao ni watu wa mwisho zaidi kubaki nyuma timu inapopanda sasa wakimbizane kwenda wapi.
Unachotakiwa kujua tu ni kwamba VVD msimu wa UEFA ulioisha yeye ndio aliongoza kwa sprint yenye kasi zaidi.
 
simchukii daniel james kwa asili yake alipozaliwa bali ni kwa kiwango chake cha wastani alichonacho kinachongezwa udambwi udambwi na media za kiingereza wakiongozwa na legend ryan giggs, binadamu tunatofautiana sana kiuelewa inawezekana wenzangu mumenizidi mno hivyo basi pengine mtazamo wangu juu ya daniel james ni dhaifu.

kwa mujibu wa situation ilivyo ndani ya manchester united uwezekano wa kusajili winga mpya haupo hivyo basi tunakwenda kumbebesha majukumu mazito huyu bwana mdogo haliyakuwa huko anakotoka hakuwa fundi kama neymar yule wa santos au frank ribery yule wa olympique marseille na uthibitisho wa hilo ni hizo takwimu zake na video zake kwa wale ambao hatujawahi kumuona dakika 90 zinatuonyesha ni mchezaji wa aina gani kwa kutumia macho yetu dhaifu.

kwangu mimi namuona daniel james ni species ile ile iliotuzalishia wright phillips, theo walcott na oxlade chamberlain (wazee wa harakati nyingi kama pimbi). klabu ilipaswa kwanza itafute winga ambaye ameshauthibitishia ulimwengu kiubora ndipo baadae tumtumie daniel james kama ni nyongeza kwenye kikosi kama ilivyo manchester city wanavyomtumia phil foden au liverpool wanavyomtumia shaqiri.

kama daniel james ataniaibisha mbele ya jamii kwa kuonyesha kiwango bora basi tutakuwa tumeramba dume na nitakuja kuomba radhi humu ndani kama nilivyofanya kwa ole gunnar solskjaer, si hivyo tu atakuwa ni mchezaji wa pili kuniaibisha baada ya zoran tosic.

lakini ikiwa kinyume chake tutakuwa tumekula hasara kwa sababu itatulazimu tena kuendelea kumtumia juan mata na jesse lingard upande wa kulia ambao wamekwisha feli kwa muda mrefu na jambo hili sitaki kuliona likitokezea tena.

alichokosea bwana ole ni kumweka daniel james kama ni kipaombele chake cha kwanza kwenye usajili ndio maana si ajabu kumuona bwana ed woodward amemkimbilia huyo kijana kwa sababu ni rahisi kumpata.

ni rahisi sana kulipa paundi millioni 50 kwa mchezaji baadae ukalipa tena paundi millioni 15 kwa mchezaji anayecheza nafasi ile ile.
ni rahisi sana kulipa paundi millioni 15 kwa mchezaji lakini ni vigumu sana kulipa tena paundi millioni 50 kwa mchezaji mwengine anayecheza nafasi ile ile.
===========================================================================================

hivi ni nani anayemdanganya ole gunnar solskjaer kama atapewa muda mrefu wa kujenga timu kwa kutumia wachezaji ambao ni underdog kama alivyo yeye na CV yake ya ukocha?

ni nani aliyemwaminisha bwana ole ya kwamba wachezaji wa kiingereza ndio pekee wenye haki miliki ya kuzipigania timu (wazalendo)?
Walisajiliwa wakina Di Maria , falcao waliifanyia nini timu licha ya majina yao Makubwa??
 
tatizo letu la kwanza tumekuwa na tabia ya kuwavumilia wachezaji wabovu kwa muda mrefu na hii tabia ilikuwepo tokea zamani na tumeshindwa kuiacha.

  • huu ni mwaka wa nane tunaendelea kumtumia phil jones asiye na uwezo wa kumweka nje lenglet wa barcelona, bado tuna matumaini mjinga yule atakuwa kwenye ubora
  • huu ni mwaka wa nane tunaendelea kumtumia cris smalling asiye na uwezo wa kumweka nje varane wa real madrid
  • tumemvumilia luke shaw kwa takribani miaka mitatu bila ya kutafuta mbadala wake na mpaka muda huu luke shaw ameanza kurudisha thamani yake pia hatujawa na fikra ya kumtafuta mchezaji mwengine atakayemletea changamoto.
  • tutaendelea kufanya kazi na jesse lingard mpaka atakapofikisha miaka 50 haijalishi kiwango chake ni kidogo
  • tuatendelea kufanya kazi na marcus rashford mpaka atakapotimiza miaka 40 haijalishi kiwango chake ni kidogo
  • hata kama itatokezea msimu huu diogo dalot na wan bissaka wakashindwa kuonyesha kiwango kikubwa pia tutaendelea kuwavumilia miaka mengine 30 mpaka wawe na kiwango kikubwa
mfumo huu umebaki manchester united peke yake, hata hao arsenal kwa sasa wameshaanzisha kampeni ya kusafisha nyumba yao.
Katika kipindi cha hiyo miaka nane taja idadi ya mabeki waliosajiriwa ...
 
Back
Top Bottom