Unajua Man Utd before SAF ilikuwa ni timu yenye mafanikio ya kawaida? Ninaposema before SAF ninamaanisha kabla ya mwaka 1986
Unaposema Man Utd ni business club na haiwezi kusubiri miaka 3, kwani mpaka sasa imeshakaa miaka mingapi bila EPL, miaka 6
Kuifananisha situation ya Man Utd na Real Madrid au Bayern ni kupotoka.
City, Chelsea, Liverpool na kiasi flani Arsenal, Everton, Spurs wana power ya kununua kama United. Je Utd ana uwezo wa kutaka mchezaji yoyote kwa Spurs, Everton, Arsenal n.k na kumnunua? haiwezekani. Pale Uingireza hadi timu inayopambana isishuke daraja inaweza kununua mchezaji kwa £30milion (kumbuka Benteke kwenda Cristal Palace)
Kwenye soko la usajili kule Spain, Madrid anasumbuliwa na Barca tu. Atletico, Valencia, Sevila hawana uwezo wa kununua kama hao wakubwa wawili. Ligi sio competitive kiasi hicho. Na Madrid au Barca wakimtaka mchezaji kutoka hizo timu za laliga (second class) lazima wamchukue, hawana jeuri ya kukataa.
Ujerumani hivyo hivyo, Bayern ndio baba lao. Dortmond, Leverkusen, Wolfborg, Schalkle n.k hawana uwezo wa kununua kama Bayern. Bayern anachukua mchezaji Dortmund (second biggest in German).
Kwahiyo kwa Spain na Ujerumani nguvu ya pesa inaweza kutumika ku maintain status ya club lakini si Uigerezs