Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

timu tatu zinaweza kutuma offer kwa mchezaji mmoja hapo sasa inabaki kazi ya timu na mchezaji kusikiliza offer nzuri.
pia usikute United hawana mpango wowote na huyo dogo isipokuwa wakala wake na magazeti yanataka kufanya biashara.
Barca na Madrid wanahusishwa na Jovic lakini sio habari ya mjini, je ushawahi kujiuliza ingekuwaje huyo dogo angehusishwa na timu yako??
huyu Herrera pamoja na uhodari wake lakini angeachwa na Madrid au Barca wala isingekuwa story.
Kama J.Sancho bei yake daah.. bora dili limekufa, wanatufanyia mtimanyongo sana
 
WAKALA WA POGBA AFUNGIWA DUNIA NZIMA

Wakala wa wachezaji mashuhuri barani Ulaya, Mino Raiola amefungiwa kufanya shughuli zake kwenye mataifa yote duniani.

Awali, Raiola alikuwa amefungiwa kwa muda wa miezi mitatu katika taifa la Italia pekee lakini Kamati ya Maadili ya FIFA imeongeza adhabu hiyo na kumzuia kufanya shughuli zake dunia nzima kwa kipindi hicho hicho cha miezi mitatu.

Chama cha Soka nchini Italia (FIGC) hakikuweka bayana sababu za kumfungia wakala huyo wa wachezaji wakubwa akiwemo Paul Pogba, Matthijs de Light, Zlatan Ibrahimovic, Henrikh Mkhitaryan, Marco Verratti, Gianluigi Donnarumma na Mario Balotelli.
Hata hivyo Mino alinukuliwa akisema kuwa FIGC ilimuhukumu kwa madai ya uongo na alipanga kukata rufaa akisema “adhabu hii haishangazi wala si bahati mbaya, ni adhabu ambayo imegubikwa na utashi wa kisiasa bila kujali haki”
Mino aliongeza “Nafikiri FIGC haijanisamehe pale nilipowakosoa kwa kuwa sababu ya anguko la soka la Italia pamoja na kuendelea kuwepo kwa tatizo la ubaguzi wa rangi kwenye soka nchini la nchi hiyo”
 
Braza hazadi ndiye anayeifanya chelsii kuwa timu tofauti na agresivu kwenye kushambulia. Akiondoka mtalimia meno. Hazadi pale chesii ni kama Messi pale Baselona,akiondoka tu hata swansii wataomba wahamie Hispania ili wakainyanyase Baselona
Sikatai juu ya uwezo wake, lakini ni Mara ngapi hukaa benchi na team inashinda
 
Mbn unapinga ukweli unaoujua kabsa! Aondoke hazard tu na wachezaji wengine wabaki, uone mtakavyopukutika na
kitakachotokea kweny timu yenu. Bora hata umejitahid kutaja wachezaj wa3 wa united kuliko nyie ambao mnao mmoja tu.
Sio kweli hata kama akiondoka kumbuka anakuja Christian Pulisic
 
Sikatai juu ya uwezo wake, lakini ni Mara ngapi hukaa benchi na team inashinda
Ha ha ha ha hamuwezi kufanya long run na mkafanikiwa bila yule kijana. Labda aondoke halafu mtengeneze mfumo mwingine wachezaji waelewane ndipo mrudi mstarini. Kwa hyo akiondoka tegemeeni kuyumba kwa msimu mmoja au miwili mbele kabla hamjarudi mstarini. Tunza hii comment na ikitokea nimesahau unikumbushe pale yatapowakuta
 
Pulisic huyu anaekaa bech Dortmund?
Mchezaji anasoteshwa bench na Overrated wa Kiengereza (Sancho) unataka kusema ataziba pengo la Hazard?
Tungelikwisha Mkuta katuwa Bayern
Huyu Pulisic toka akubali kwenda Chelsea benchi limekuwa lake kitambo sasa...
 
Back
Top Bottom