Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mzee bab umeandika kitu chenye maana sana..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu fanya uhamie manchester united kwa sababu umeshakuwa muathirika wa hii thread.
Acha kumdanganya mwenzako.

Jana nilikua naangalia gemu yenu na mwenzenu wa Man U. Ikaja ile faulo ambayo refa akatoa red.

Akaanza "Yule kapewa red kwakua alikua beki wa mwisho" nikamwambia "Red itatoka kokote kutegemea na dhamira ya mcheza faulo. Mfano kama huyu angefuata mpira angepewa njano"

Akaanza makelele. Sa mi si nnajua man u wengi mpira hamjui mmezoea kubebwa na marefa nikamuacha. VAR ikaonyesha ile ni yellow.

Akaanza tena "Ujue kagewa yellow kwakua alikua kakunja miguu hakuikunjua"

Tukamfukuza.
 
mkuu itakuwa umechanganya madawa, Tafadhali jaribu kupitia tena comment yangu halafu uangalie tena kwa makini hicho ulichokiandika.
havifanani kabisa kama maziwa na maji​
 
Mkuu, toka msimu wa 2014 Hadi Leo Man U wametumia zaidi ya 600 milions pound, Man City wametumia 680 milion
, Chelsea na Liverpool wote chini ya 500 milion

Mbona watu bado wanalalamika kuwa Man U/ Edwoord& Glazer hawatoi fedha za usajili
...
Walimu wote waliopita Moyes,LVG na Mou mamesajili wachezaji wa milion 600
ambao ufanisi wao haonekani Kama wenzao City (tofauti ya city na man u KWENYE usajili Ni 80milion pound, tofauti ya ubora wa timu hizo wote tunajua)

Wamiliki wa man u Ni wafanyabiashara(investors) lazima washawishiwe kuwa Ni Nini kimebadilika isijekuwa wachoma hela Kam kwa DEPAY,DE MARIA, BLIND, LUKAKU, SANCHEZ, POGBA, HENRICH, BASTIAN, na nk wote hao wakiuzwa/wameuzwa kwa nusu Bei ya kusajiliwa ndani ya miaka 2.5 wakiwa hawajazalisha kulingana na hell walizo nunuliwa
Afu bado wanaaambiwa wawekezaji/glazer/bodi watoe hela zaidi za usajili.... Duh


Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu itakuwa umechanganya madawa, Tafadhali jaribu kupitia tena comment yangu halafu uangalie tena kwa makini hicho ulichokiandika.
havifanani kabisa kama maziwa na maji​
Mbona naona kama unamshauri jamaa ahamie Man U?

Ndiyo maana nikaanza na usimdanganye.

Au wewe siyo Man U?
 
Mbona naona kama unamshauri jamaa ahamie Man U?

Ndiyo maana nikaanza na usimdanganye.

Au wewe siyo Man U?
ishu iko hivi: jamaa ni mpenzi mkubwa sana wa chelsea humu JF lakini muda mwingi sana unamkuta ndani ya hii thread akileta upinzani wake.
nimezungumza kama ni utani kwa kumwambia ahamie manchester united kwa sababu hii thread imeshamuathiri.
 
They must find someone who understand football before they splash money otherwise cycle will continue.
And you must know how much they get since they bought club

Woodward is responsible to recruit technical team (managers) and aprrove all purchase and sales of players
Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Zaha alisajiliwa na fergie,
2. Nikumbushe lini depay na Di maria walicheza Wing ya kulia man U.
-depay kuanzia world cup chinj ya lvg mpaka man u alicheza either wing ya kushoto ama akitokea katikati, kulia alikuwepo mata/januzaj/lingard
-same kwa di maria alicheza kushoto kwenye diamond ya lvg na baadae kupokonywa namba na young kwenye 4-1-4-1
 
Wolves 2 - 1 United

Haya ni matokeo mabaya kuwahi kutokea katika zama za OGS, lakini si mabaya kuwahi kutokea kwa klabu yetu pendwa ya Manchester United

Nikumbushe tu, msimu huu tulitolewa hatua ya awali kabisa na timu inayoitwa Derby County katika kombe la Carabao, Derby ni timu ambayo hata haipo EPL. Pia hatupaswi kusahau kuwa hawa Wolves waliotufunga jana (sijui ni jana au leo) walilazimisha kutoa draw dhidi yetu pale OT msimu huu

Ieleweke, hapa silengi kufananisha kocha aliyepita na huyu aliyopo. Hapa nataka kuonesha kwamba kupigwa na hizi timu type ya akina Wolves inawezekana.

Labda ili kuwafahamu vizuri Wolves, hawa ndio walio toa draw na City mwaka jana, wakaifunga Arsenal, wakaifunga na ku draw na Chelsea na pia waliifunga na kuitoa Liverpool katika kombe la FA. Kwa hiyo si wabovu kiivyo, lakini kwa kuwa sisi ni Manchester United hatupaswi kuridhika kufungwa, eti kwa kuwa timu nyingine zilifungwa na hii timu

OGS ana kubarua kizito, kuna watu wataanza kuhoji uwezo wake hususani kutokana na hivi vipigo viwili vya karibuni alivyopata mfululizo. Lakini itakuwa ni makosa ku judge kwa matokeo ya mechi hizo, itakuwa ni busara ku judge kipindi cha May (hata huko nyuma nimewahi kulisema hili)

Kama kuna jambo OGS anapaswa ku improve katika kutafuta umeneja wa United ni kuondoa emotion linapokuja suala la ku deal na hawa watoto (Martial na Rashford). Anapaswa kuwaambia ukweli ili wa improve. Kusema hivyo, sio kusema kwamba hawa watoto hawana uwezo. Awaeleze wawe wanatoa pasi kwa wakati, wasiwe wachoyo wa pasi (Rashford na Martial) na wajitume zaidi (Martial)

Jambo lingine ambalo OGS anapaswa ku improve ni kuwa bold enough, kuwaambia ukweli Board na wamiliki kuhusu mapungufu yaliyopo pale United ili apewe fedha asajili. Kuna wakati OGS anaongea kauli zinazoonesha anabembeleza kazi, mfano juzi nilimuona anasema timu iongeza mtu mmoja au wawili ili kuboresha kikosi (kwa kweli sikumuelewa)

Vipigo si vizuri, lakini kuna msemo unasema kwenye kila jambo kuna jambo chanya ndani yake. Labda kwenye haya matokeo Board itaona Man Utd tuna mapungufu na tunahitaji kusajili. Pengine Board itaona Jose was right na hivyo kutoa mpunga wa maana kwa ajili ya usajili

OGS bado hajapata kazi. Hivyo anapaswa kukaza. Lakini hakuna kocha ambaye huwa hapotezi mechi.

Jose alikuwa right kuhusu bodi. Mpaka sasa eti inaendelea kutafuta Director of Football. Angekuwepo DoF angeweza anza mikakati ya usajili hata kama meneja bado hajatajwa. United kuna tatizo kubwa zaidi ya individual players, zaidi ya kocha.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fixed

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ishu iko hivi: jamaa ni mpenzi mkubwa sana wa chelsea humu JF lakini muda mwingi sana unamkuta ndani ya hii thread akileta upinzani wake.
nimezungumza kama ni utani kwa kumwambia ahamie manchester united kwa sababu hii thread imeshamuathiri.
Hahahahaha hahaha siwezi huu kufanya upumbavu kama huu ..nikifanya hivi kizazi changu chote kilaaniwe...

The Bluez forever ..hata wajukuu zangu nitahakikisha wanakuwa Bluez fans.

KiNG OF LONDON..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Lvg hakupewa hela za usajili wa kuimarisha Timu bali za kureplace wachezaji, anapewa timu hali ya kuwa mabeki watatu wa kutegemewa ndani ya club wanaondoka kwa mpigo, Vidic, Rio na Evra, midfield nao wanaondoka kina scholes, fletcher etc alibaki carrick, Giggs kastaafu, timu haina quality kabisa, ukiangalia usajili wa LVG alileta tu squad players kina shaw, Herrera, blind etc hao kina Di maria, Falcao etc waliletwa tu na timu kocha alikuwa na Target zake Muller, Robben Etc.

2.Hio 600 unayoitaja ina double counting kibao, mfano Di maria kanunuliwa kwa 60m kisha kauzwa kwa 45m hela yake ikanunuliwa mtu kama Depay na martial kwa around 60m again, huwezi kusema eti tumespend 120m kununua wachezaji watatu, ni hela ile ile imezungushwa.

3. Huu ni ushahidi wa uhuni wa Glazer na Woodward.

-miaka 10 iliopita Man U ndio timu ilioingiza hela nyingi zaidi ligi ya Uingereza kutokana na Activities mbalimbali. 1.3B pounds, kwa comparison timu ya pili ni Arsenal around 700m pounds, hivyo uone gap la hela baina ya Man U na timu nyengine, Man city ni around 140m tu.


-pamoja na kuingiza hela nyingi hawa jamaa wanazichota zote na kulipia Madeni ya Mmiliki, ikumbukwe kabla ya Glazer Man U ilikaa miaka zaidi ya 70 bila deni, ilikuwa ni Timu ya kuigwa Ila jamaa walivyofika na kuinunua Club wakahamishia Deni lao Binafsi kwenye Timu na kisha Wanatumia Hela zetu kulipia Deni lao.

Ukiangalia hizo data utaona kati ya 1.3B ilioingia almost 800m inalipa madeni na Riba.

-Hili graph linaelezea zaidi


Ukitoa spurs na arsenal, Man U ni timu ya tatu kutoka mwisho kwenye kutoa hela zake inazoingiza kwenye usajili. Imagine mkuu club tajiri zaidi duniani inashika nafasi ya tau toka mwisho kwenye kutoa hela za usajili unategemea nini?

Na bora hata hizo hela za timu wangeziweka kwenye cash ungesema labda wanasave for future na kuweka reserve kubwa,

Kiufupi mkuu tumepatikana sana, na sijui nani wa kututoa hapa, matajiri wengi wana Approach kuirudisha Man u ila jamaa wanatoa Unrealistic figures ili timu iendelee kuwa yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…