siwezi kuwacha hawa watu wanakera sana,mafanikio ya Man united yanawaumiza sana.Mfano shabiki wa Arsenal,miaka saba timu haijachukua hata kikombe cha kahawa.Baada ya kuijadili timu yake anashobokea Man united.Hawa jamaa vipi? Semeni basi zile goli nane refa kabeba.MAN UNITED ndio baba ka soka la uingereza kwa sasa. Na bado tutatesa kwa sana tu. Halafu kuna hawa wapenzi wa Liverpool, hawa jamaa wanashangaza sana.Mwaka wa 22 huu hawajachukua ubingwa wa Uingereza, hii ni sawa mtoto anazaliwa,anatambaa,anatembea,anaanza shule,anamaliza shule,anaingia chuo,anamaliza chuo na kuanza kazi.AIBU GANI HII. Baada ya kutafakari aibu yao,wanaishupalia Man united,wanachekesha hawa. Wapo tayari kufungwa ili Man united isichukue ubingwa.Si mnakumbuka steven Gerald alivyompasia mpira Drogba ili wafungwe?kwani hizo timu mmelazimishwa kuzishabikia?kama vipi hameni kuliko kuleta maneno ya kinafiki kila siku eti ohoo Howard web ni shabiki wa Man united. Chelsea hawa sina hata haja ya kuwazungumzia kwa sababu washawahi kukuaa miaka 50 bila ya ubingwa wa ligi kuu.