D A E M U S H I N
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 22,633
- 121,022
Mourinho aliwasajili Fred na Sanchez ili kuibania Man City,kumbuka Pep alikua anataka kumsajili Fred ili aje kumpunguzia majukumu Fernandinho na Sanchez alikua asajiliwe ili kuziba pengo la Sane alipopata majeruhi..!
Mourinho akaona haiwezekani Guardiola awasajili hao wachezaji,akaamua kutia fitna..!
Kinachotokea ni matokeo ya kusajili mchezaji ambaye haumuhitaji..!
mwenzenu bado nipo dilemma kwenye hii ishu ya kusajiliwa alex sanchez, inaniwia vigumu kuamini ya kwamba ni jose mourinho ndiye aliyependekeza dili la sanchez kuja man utd.
tukumbuke msimu uliopita jose alimuhitaji ivan perisic ili acheze upande wa kulia sasa kwa nini mourinho amkimbilie sanchez anayecheza upande wa kushoto kwa sababu dhaifu kiupande wangu ya kumzuia jamaa asisajiliwe na man city?
tujiulize ni nani aliyefaidika na dili la sanchez kati ya mourinho na ed woodward?
.

