Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tunajua mpira ni magoli lakini msijidanganye kuwa mpo vizuri. Mvua za kiangazi zikikatika mtakuja kutafutana kwa mara nyingine. Nimeangalia kwa kuibia but wapenzi wenu (wanaoujua sio hawa wa JF) wanasema tofauti ilikuwa nyie kuwa clinical na Arsenal kuwa butu middle na mbele.

Sasa mzee mwenzangu, United kuwa clinical na Gooners kuwa butu, siyo ndiyo maana United ikaibuka mshindi?

Tupo vizuri zaidi yenu, ndiyo maana tumewapiga goli 3 hapo kwenye dance floor ya Lingard, sijui ninyi mnapaita Emirates Stadium.

Za kupotea lakini?
 
ole ole ole ulikuwepo wapi nyakati zile tunateseka?
ni takribani wiki 9 tokea uanze kazi pale AON cha ajabu umetufanya tuonekane na wapinzani wetu tumefanya usajili wa timu nzima kumbe ndio wale wale wa kila siku.

tokea uanze kazi mimi lofa na wenzangu tunashangazwa kuona morali yetu na nidhamu ya kupambana imeongezeka sana ukilinganisha na makocha wote waliopita, nyakati zile arsenal wanasawazisha goli moja naamini kama tungelikuwa bado tupo kwenye utawala wa bwana yule tungelishuhudia khofu kubwa ikitawala kuanzia wachezaji hadi mashabiki lakini tulichokishuhudia jana ni tofauti kabisa na tulichozoweshwa kwa miaka 3.

ole umeturudisha nyakati zile nilizokuwa napendelea kuangalia mechi zetu kila wiki, nakumbuka nyakati zile ni wachezaji wachache walikuwa na uhakika wa kucheza kila wiki huku tukiwapa nafasi wachezaji wengineo (rotation) wakuze viwango vyao, tokea awasili ole gunnar kama nitakuwa sikosei ni antonio valencia, smalling, na marcos rojo ndio wachezaji waliosafiri na kikosi mara chache, ni matumaini yangu wiki ijayo atampa tena nafasi fred apate kujisahihisha.

umetufanya kwa muda mfupi tusahau anguko letu huku tukijawa na morali ya kurudi tena pale tulipofikia msimu uliopita, najua siku moja tutapoteza pambano japokuwa siombei tupoteze mechi yoyote chini yake, sina wasiwasi kwa jinsi unavyozungumza kupitia mahojiano yako ya kila wiki ni matumaini yangu utakuja na sababu za msingi za kufungwa kwetu tofauti na bwana yule anayesukumia mizigo wachezaji wake hata kama tatizo ni yeye.

ili defence yetu izidi kupata mapumziko ya mara kwa mara tunahitaji midfield yetu ifanye kazi zaidi ya sasa kwa kumiliki mpira zaidi (ball retention) huku tukishambulia kwa haraka zaidi kama alivyokuwa akifanya paul pogba dakika 30 za mwisho, ninapowaangalia liverpool na manchester city wakicheza hushuhudia utofauti mkubwa sana wa kiuchezaji dhidi yetu, nitafurahi sana endapo tutakapokutana tena na timu kubwa na nyenginezo sisi ndio tuwe bora zaidi eneo la midfield kuliko wapinzani wetu, naamini hii ndio solution nyengine itakayosaidia kupunguza kuonekanwa madhaifu ya defence yetu ukiondoa solution ya usajili ambayo kwa sasa kuna uwezekano mdogo wa kuingiza mlinzi mpya.

dirsha lijalo kama tutapata mwanadamu mwengine mgumu kama herrera (tackle and break up) na wakati huo huo akawa na uwezo wa kucheza na mpira (ball playing midfield) ) kama herrera yule wa miaka ya mwanzoni basi tutakuwa tumeua ndege wawili kwa jiwe moja kuliko kusajili wachezaji wawili kwa eneo moja, nimeanza kuwachukia barcelona kwa tabia yao ya kukusanya midfield 11 kwa wakati mmoja huku wakituache wengine tukihangaika sokoni.

kumbe huyu romelu lukuku akitokea pembeni anakuwa hatari zaidi kuliko anaposimama kati kati, sijui kwa nini amenyimwa skills na speed.
kiupande wangu man of the match kwa siku ya jana alikuwa ni ander herrera.

happy birthday jose mourinho
 
Timu inahitaji marekebisho kidogo sana upande wa ushambulizi tunafanya poa maana mwanzo hata ushambulizi ulikuwa hovyo tupate bek mmoja na namba 2 au hata 6 maana siku akiumia herrera tutaimba hapa
Mou alionekana kama anataka kununua timu nzima.

Timu zitakazomsajili Mou ziwe makini sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Same old story
10year.jpg
 
Ndombile kiungo wa Lyon bonge la mchezaji anafaa Sana pale Kati Seema tatizo man city nao wanamtaka

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo jamaa ni fundi sana

City kumtaka sio hoja sana, we can compete mkuu. Na mimi nikisikia hivyo ndio nafurahi, hata barca, real madrid n.k wakimtaka poa tu. Hiyo ni ishara kwamba huyo ni mchezaji mzuri

Nadhani angetusaidia sana kwenye kiungo ya kushambulia kama tungempata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatzo ni kwamba mnataka defance isio ruhusu goli hata moja kwa msimu mzima kitu ambacho hakijawahi kutokea toka dunia iumbwe, sio kwamba tuna tatzo kuubwa la defance kiasi cha kila mtu kulalamika kama vile ndo timu inayoongoza kwa kuruhusu magoli mengi toka OGS akabidhiwe timu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli

But still tunahitaji beki hususani wa kati (hili ni urgent)

Mabeki wa pembeni kwa maana ya kuwa na warithi wa Young ni jambo la msingi

Kiujumla hata mimi sijaona kama Young alicheza vibaya kiivyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niliangalia ile mechi jana kipind arsenal wanatafuta goli kusawazsha na wakamuingza Ozil na Matheo,
Nkajikuta tu akil za ki mourinho zinnijia sasa na sie tuingze beki
Kuja kuchek kumbe zama za OGS, Mwendo wa toa kitu weka kitu....
Ni kweli Mkuu

Japo mwishoni kau-Mourinho kalitumika kidogo alipotoka dogo Lingard akaingia Jones

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hahaaa, nini maana ya football?
Kikubwa ni kupunguza makosa madogomadogo.
Hata ukuta Rio na Vida uliruhusu magoli.
Mkuu watu wanataka timu icheze mechi 38 bila ya kuruhusu goli, sijui wameiona wapi timu hiyo, mchezaji kutokua fiti gemu moja au kufanya kosa ambalo lilisababisha tufungwe goli hiyo si kipimo cha mchezaji huyo kuisha

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, hii habari ya Young achana nayo kabisa, huu ndio mzizi pale united. Siku akiachwa nje ndio utajua umuhimu wake. Tackle zake ni za kiutu uzima sana. Huyu anatakiwa azeekee hapa kama kina Pirlo walicheza mpaka over 40. Young ana akili kubwa sana ya kuzuia mashambulizi, utaona wakati ule aliudaka mpira akapigwa yellow. Anajua ule mpira ungempita nini kingetokea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Naunga mkono hoja

Man watumie option ya kuongeza mwaka mmoja

Msimu ujao akiendelea kung'ara aongezwe tena

Iwe mwendo wa mwaka mmoko mmoko

Hakuna kijiji kisicho na wazee, hakuna timu isiyo na ma- senior players

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe plastic fan ulipotelea wap?

Wenzako wakina radika wako apa muda wote wewe unaonekana timu ikipata matokeo mazuri tu.

Huo ni ushamba mkuu.

Ila hongereni kwa ushindi wa kawaida.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kwa jinsi ninyokuhisi utakuwa unateseka sana kwa haya matokeo

Ila nakukubali sana maana unaonekana unaipenda United sababu huu uzi haipiti siku hujautembelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwa jinsi ninyokuhisi utakuwa unateseka sana kwa haya matokeo

Ila nakukubali sana maana unaonekana unaipenda United sababu huu uzi haipiti siku hujautembelea

Sent using Jamii Forums mobile app
Asee kuliko niipende Man United ni bora nisiwe mshabiki kabisa wa clab yeyote ile ya mpira. Mimi ni Chelsea fan na nitabaki kuwa Chelsea forever.

Kuja hapa sio kwamba napenda hichi kikundi kinachojiita Man united, napitaga majukwaa yote ya soka ili kuleta changamoto tu kama mdau wa mpira.

Enewei hongereni naona munajitahidi kufuta aibu ya Mourihno.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa mzee mwenzangu, United kuwa clinical na Gooners kuwa butu, siyo ndiyo maana United ikaibuka mshindi?

Tupo vizuri zaidi yenu, ndiyo maana tumewapiga goli 3 hapo kwenye dance floor ya Lingard, sijui ninyi mnapaita Emirates Stadium.

Za kupotea lakini?
Eti dance floor ya Lingard.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu naona saivi umekuja na Higuein pale mbele hatari sana tunawasubiria OT.
Asee kuliko niipende Man United ni bora nisiwe mshabiki kabisa wa clab yeyote ile ya mpira. Mimi ni Chelsea fan na nitabaki kuwa Chelsea forever.

Kuja hapa sio kwamba napenda hichi kikundi kinachojiita Man united, napitaga majukwaa yote ya soka ili kuleta changamoto tu kama mdau wa mpira.

Enewei hongereni naona munajitahidi kufuta aibu ya Mourihno.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom