D A E M U S H I N
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 22,633
- 121,022
GT Belo,umerudi tena pale pale kwenye mtazamo wangu wa kwa nini sipendelei man city abebe tena ubingwa msimu huu kwa sababu tayari hawa majirani kwa kikosi walichonacho wana uwezo wa kubeba ubingwa mara tatu mfululizo jambo ambalo litapelekea majirani zetu kuzidi kutukalia juu wakati ambao tunataka kujikwamua, vile vile kubeba kwao ubingwa ndio kutazidi kumfanya guardiola aonekane ni untouchable na ligi yetu pia ionekane ni ya upande mmoja.Man City hata wasiponunua tayari wana timu ya kugombania ubingwa hata miaka 4 ijayo Pep anahitaji backup/replacement ya Fernandinho tu
milner, henderson, matip, lovren, origi, lalllana, clyne, sturidge, moreno, ings, gomez n.kUnadhani Liverpool wakichukua ubingwa ndio timu yao itakuwa weak ?
Football ya sasa ni pesa Klopp aliponda usajili wa Pogba baada ya mwaka akanunua GK & CB kuvunja rekodi na umeona hao wachezaji 2 ndio wameifikisha Liverpool ilipo.
Don Clericuzio na washabiki wenzako wa liverpool FC naomba muwe wa kweli; hivi munafurahia kuona timu yenu imekusanya wachezaji niliowataja hapo juu kama ndio backup yenu na wengineo ndio first eleven?
kama munafurahia basi nitakuwa sipo sahihi kwa kile ninachokiamini
hata muda huu ambao bado hawajabeba ubingwa nawaona liverpool wakiwa ni dhaifu ukiwalinganisha na manchester city, timu inayoundwa na wachezaji hao niliowataja hapo juu kama ndio backup yao pindi linapotokezea tatizo kwenye timu kwa nini nisiwaite dhaifu.
timu ambayo ikitokezea virgil amepumzishwa nafasi yake inachukuliwa na lovren kwa nini isiwe dhaifu?
hata kama liverpool wataingia tena sokoni chini ya matajiri wa kimarekani kwa sera zao za matumizi naamini itawachukua tena miaka miwili ili waweze kuwaondoa wachezaji hao niliowataja na kuwaleta wengine wenye uwezo zaidi ya hao, kimtazamo wangu nawaona liverpool wanasumbuliwa zaidi na tatizo la ukosefu wa wachezaji wengi wenye ubora ukilinganisha na manchester city hata kama itatokezea atabeba ubingwa, na huo ndio udhaifu ambao nauona mimi kama ni faida kwetu sisi msimu ujao endapo kama tutafanya biashara sahihi.
lakini ukija kwa upande wa majirani zetu kwa nguvu yao ya usajili wana uwezo wa kutafuta mrithi wa fernandinho, david silva, vicent kompany kwa msimu mmoja tu bila hata ya guardiola kutakiwa auze kwanza mchezaji ili aongezewe fungu la usajili.
vile vile kwenye ishu ya matumizi sidhani kama liverpool wana uwezo wa kusimama na manchester united kama ilivyo sisi tusivyoweza kusimama na manchester city kimatumizi na si kwa kulinganisha thamani za klabu, hivyo kiupande wetu naamini kama tutafanya biashara sahihi kwa kuangalia zaidi udhaifu uliopo kwenye kikosi chetu upo uwezekano mkubwa wa kufikia level walioionyesha liverpool msimu huu hata kama na wao wataingia sokoni.
mimi naona kuna tofauti ndogo sana kati yetu na liverpool FC lakini kuna utofauti mkubwa kati ya kikosi chetu na kikosi cha manchester city ndio maana sipendelei man city abebe tena ubingwa.
bado akili ya josep guardiola haijachoshwa na maisha ya etihad.
kama sipo sahihi naomba nikosolewe kistaarabu ili ujinga uliomo kwenye ubongo wangu upungue.