*SAKATA LA KIBARUA CHA UKOCHA NDANI YA MANCHESTER UNITED.*
Kwanza kabisa ukiizungumzia man utd unaizungumzia klabu tajiri kabisa duniani, kifedha, kishabiki, kimvuto, na pia kwa mataji ni kati ya timu tatu au nne zenye rekodi nzuri sana ulaya hasa kwa miaka michanga ya 2000, chini ya SAF.
Baada ya SAF kustaafu, ni miaka sita sasa united haijawahi sio tu kuchukua kombe la ligi uingereza ambalo ilikua kama utamaduni wake, bali pia hata kufikia kilele cha uwezo uwanjani bado hatujafika,
Nitazungumzia sana sana aina ya kocha ambae atafaa kuibeba manchester united hii kwa kuanzia msimu ujao wa 2019-2020, lakini kabla hatujafika huko ni lazima tuainishe mahitaji yetu kama klabu, na tujiulize ikiwa tunafahamu mahitaji yetu, tumekuwa tukikwama wapi kwa kila kocha aliepita na pia huyo ajae atafaa??
Wakati SAF anastaafu, utukufu wake ulitumika zaidi kumleta David Moyes kwenye klabu yetu,
Kulingana na CV na mwenendo wa klabu yetu na mahitaji yetu ya kipindi kile, ilionekana DM ni chaguo sahihi kabisa,
Kwa sababu zifuatazo,
Mosi, Tulikua wageni kwenye soko la makocha, ugeni huu unadhihirishwa na kukumbatia itikadi ya kumvumilia kocha ilihali hakupi matokeo kwa sababu tuuu SAF alikaa miaka minne bila kombe na leo katuletea mataji 26 old trafford,
Lakini pili, ni kuendelea kukomalia kuwa sisi ni klabu vumilivu kwa makocha wasio na mwelekeo wa mataji,
*Namna DM alivyoiimarisha Everton, tukumbuke namna ambavyo tulikua tukipambana sana kupata matokeo mbele ya everton, pia DM alihakikisha everton ipo ndani ya top 6 kwa misimu mingi tena kwa uwiano mzuri,
Kwa kuwa DM alikaa everton muda mrefu, na kwa kuwa aliitengeneza everton kuwa imara, SAF na bodi ikaona ni vema kumpa timu, pengine ni kukosa pesa tuu ndo kunamfanya ashindwe kugombania ubingwa!!
Haya ndo yalikuwa mahitaji ya awali ya timu mpaka kumleta DM.
Alipofika united, DM akafeli,
Alifeli kwa sababu ya kukosa kwanza kabisa, namna ya kuwamudu wachezaji wakubwa walioshinda mataji kuliko kocha, wenye pesa kuliko kocha, wanaolipwa mshahara mkubwa kuliko kocha mwenyewe,
DM hakuweza kumudu timu kubwa, yenye mahitaji makubwa, inayowaza makubwa, badala yake DM alikua anamuonyesha carrick clip za jagielka acheze kama jagielka anavyocheza, badala yake DM anaiongoza timu kupiga krosi 96 per game bila goli lolote, kuonesha kuwa hana tactic mbadala, siku anaingia carrington anashangaa trainning kits za united, anashangaa trophy room, wachezaji wakubwa wote wakamuona hana kitu, akawapoteza,
Mwisho Moyes akafukuzwa na miaka sita yake ya mkataba!!
Baada ya Moyes kufanya wachezaji kumdharau kutokana na profile yake, vitendo vyake, kauli zake (tunaita peanut talk, yani kauli cheap) , kukosa mbinu na identity ya mpira, haya sasa yakawa ndio malengo ya kocha wetu tunaemtafuta,
LVG akawa ndie chaguo pekee lililokuepo available, ukizingatia mafanikio yake akiwa na uholanzi,
CV ya LVG imeshiba haswa, ndie muasisi wa tiktaka pale barca baada ya Johan cruyff, ndie huyu aliepandisha bayern fainali UCL mara mbili, moja anafungwa na mourinho vs Inter milan, ana falsafa ya mpira na mbinu za mchezo, ana kauli nzito kwa wachezaji na ni kocha mkubwa,
Akaleta falsafa ya pasi nyingi, bahati mbaya sana, timu ilikua haina watu wenye mpira anaotaka yeye, leo hii man city guadiola amesajili wachezaji 22, timu mbili kamili, ilimradi acheze mpira wake, sisi kwetu bodi haikuwa tayari kwa hilo, (overhaul), ikidai kile ni kikosi kikichotoka kuchukua ubingwa!!
Kingine ni wachezaji kutomuelewa lvg, kuwa waoga wa kucheza na kutokua na vipaji vya kucheza mpira wa tikitaka, ndio maana lvg akaona aanze moja kwa kuweka blackett, wilson, martial, rashford, aanze kuwafundisha upya, akina smalling hawawez kupiga pasi katika tight space, jones hawezi, ndio maana akamleta rojo, akamleta bastian schwei, watu wanaoweza kupokea mpira hata kama anavamiwa bado akatoa pasi bila kubabaika miguu wala kupiga pasi mkaa, ndivo city wanavyocheza sasa, na tunawasifu kuwa ni bora ulaya kwa sasa, wanapiga pasi hata kwenye box lao wanapiga pasi, hawana kitete, hawaogopi, ndivyo barca wanavyocheza,
Kwetu uoga wa kupoteza mipira ukafanya wachezaji wapige pasi safi tuu, yani hakuna anaethubutu kupiga pasi ya kujiongeza, hii pia inachangiwa na kocha kuwa mkali sanaa,
Mwisho wa siku lvg akafukuzwa pia,
Kutokana na kukaa muda bila makombe, na klabu bado tunataka kocha mkubwa, aibebe brand yetu, tukaacha habari za kutaka falsafa ya mpira, tukataka sasa tupate makombe tuu,
Hii ilidhihirishwa wazi baada ya ed woodward kumleta Mourinho ilihali SAF na Sir bobby charlton kugoma kukubaliana na woodward kuhusu suala la mourinho,
Mou anafahamika, hanaga mpira mzuri, hanaga falsafa maalum, lakini pia ni mtu ambae anailinda sana brand yake, yuko radhi amchafue yoyote ila sio yeye achafuke,
Ni wazi yaliotokea chini ya mou sote tunayajua, kugombana na wachezaji, kejeli, kukosa mbinu pia,
*Sasa kocha ajae anatakiwa awe vipi??*
Kuna majina mengi sana yametajwa, Zidane, Allegri, Potchetino, na mengine mengii,
Kocha ajae anatakiwa awe na falsafa ya mpira, inayoruhusu timu kufunguka zaidi na kushambulia, yani ikidhi attack attack attack, ilihali ndani ya falsafa hiyo hiyo iweze kuzuia vizuri tusifungwe,
Anachocheza OLS kwa sasa sio falsafa ile, wala hakuna mbinu pale, pale ni kawapa tu uhuru watu waende mbele wakashambulie, bado tactics hazipo, katika vita, plan ya vita ni muhimu kuliko bunduki yenyewe,
City wana defense kwa kukaa na mpira, ndio maana watu wengi city ni wale ambao wana mpira mguuni, hauchukui mpira hovyo, ukiuchukua wanakua na high defensive line, na kipa nae anasogea kusaidia beki, wakienda mbele kuna movement nyingi sana wanafanya kwenye box, kutafuta kuwekewa pasi ya mwisho,
Liverpool wanakaba wengi wengi kwa kuvamia, wakienda juu wako speed sana na wanajua nani anapita wapi kwa muda gani mpira ukiwa wapi,
Hizi ni timu bora EPL kwa sasa, lakini tuangalie aina ya wachezaji inaowachukua pia,
Leroy sane, ederson, mendy, stones, laporte, jesus,
Robertson, salah, firmino, wijnaldum, hawa wote ni under 25 yrs, ina maana wanakupa miaka 5 ya kucheza kitimu ukiwaweka pamoja chini ya falsafa nzuri,
Sisi tulisajili ilimradi tuu, usipojua unataka nini, kika mchezaji mzuri utamsajili, lakini sio kila mchezaji mzuri anakufaa,
Nimesema haya ili tujue kuwa kocha tunaemtaka je, hatutakwama kama mwanzo?
Zidane hana falsafa, mafanikio yake ya muda mfupi kwa timu iliokamilika kila idara, ni sawa na kumrudisha mou mwingine tu,
Carlo ancelloti umri umesogea sana, japo kimbinu yuko vizuri sana,
Potchetino, je hatakuwa david moyes mwingine??
Ataweza kuwamudu pogba na wenzie??
Kwaiyo tunapotafuta kocha tuangalie profile ya mahitaji yetu,
Vinginevyo naamini tuwekeze kwa potchetino tuu, ni risk lakini lazima tukubali kuanza mwanzo, tusajili wachezaji wataofit mfumo wake, sababu ni attacking pia.
@Udeh_United
Sent using
Jamii Forums mobile app