Mimi mkuu sikuelewi kwanini unaona kama SAF kukaa timu moja ni privilege aliyopata, hiyo sio privilege bali matokeo ya uwezo wake. Wewe unadhani Mourinho hapendi kukaa timu moja muda mrefu, au Pep au Ancelot au Zidane? Mimi nadhani unapaswa kumsifu kwanza ameweza kukaa muda mrefu timu moja.
Pep na Zidane ni mifano mizuri sana. Wewe unadhani Pep kwanini alikimbia Barca, alijua within 3 to 5 years hatakuwa na Xavier, Iniesta, Puyol, Messi, Bosquet and co. (Na hata wakiwepo hawatakuwa wa kiwango hicho sababu ya umri) ( Hii ilikuwa CORE ya Barca)
Unadhani Zidane hakupenda kufundisha Madrid miaka 20+, alisoma upepo, aliona wachezaji wake tegemeo kama akina CR 7, Ramos, Modrick, Pepe, walikuwa mwishoni, (Pepe alishaondoka) Bale (Zidane angebaki, yeye angeondoka n.k), Alikimbia fedhea (Hawa ni CORE ya timu ya Madrid)
Nadhani wewe tu ndio utakuwa una wasiwasi na uwezo wa SAF katika UCL, lakini dunia nzima wapo tofauti na wewe.