nilivyomuelewa muheshimiwa john mweusi
naamini sote tunakubaliana ya kwamba kwenye miaka 26 ya utawala wa sir alex ferguson ni miaka 21 ndio ilikuwa ni miaka yake ya mafanikio makubwa ndani ya klabu ya manchester united ndani ya uwanja na nje ya uwanja (mafanikio ya kibiashara).
muheshimiwa
johnmweusi hoja zake ni hizi hapa kwa nilivyomfahamu mimi kiupande wangu kwa kutumia GPA ya 50 ya chuo kikuu cha romelu lukaku
ndani ya miaka 21 ya mafanikio yake sir alex ferguson alifanikiwa kubeba makombe 13 ya ligi kuu ya uingereza na ndani ya miaka 21 ya michuano ya ligi ya mabingwa alifanikiwa kubeba makombe 2.
- kwa takwimu hizo je inastahili kwa sir alex ferguson kupewa heshima ya kocha bora wa bara la ulaya kwa muda wote?
- au anapaswa tu kupewa heshima ya kocha bora wa nchi zinazounga United Kingdom kwa muda wote
- je kwa takwimu hizi za ligi ya mabingwa bwana john mweusi anauliza inawezekana timu yetu ilikuwa dhaifu sana pindi inapokutana na wababe wengineo wa ulaya ndio maana tuliishia kubeba makombe 2 kwa miaka 20?
- je inawezekana ni media za kiingereza ndio zinatujaza pumzi na ujinga kwa kutuaminisha ya kwamba fergie alikuwa ni genius na hatatokea kama yeye barani ulaya (naamini ndivyo anavyowaza john mweusi jamani sio mimi)
hahahahahahahahhaaaaa hii vita ya hoja ilioanza tokea jana humu ndani inaweza kutuletea ugomvi wa ndugu ila acha kwanza nimtetee
johnmweusi halafu baadae nitaangalia upepo unavyovuma, baadae nitajigeuza kinyonga nimrushie mvua ya mapovu brother john mweusi
Great Thinker anayeitwa
Mc cane ameweka takwimu zinazoonyesha makocha waliofika nusu fainali mara nyingi kwenye michuano ya ligi ya mabingwa ambapo sir alex ferguson ndani ya miaka 20 amefika nusu fainali mara 7.
- 1997: United lose 2-0 to Borussia Dortmund on aggregate : inamaana hapa ilimchukua ferguson miaka 5 kufuzu nusu final ya ligi ya mabingwa na wakati huo huo kama sijakosea alishabeba makombe 4 ya ligi ya uingereza kutoka 1992.
- 1999: United beat Juventus 4-3 on aggregate : ina maana tulikaa miaka 2 ndio tukafuzu nusu final na kufanikiwa kubeba ubingwa. kwa hesabu za kitoto ilimchukua miaka 7 sir alex ferguson kubeba ubingwa wake wa kwanza wa ulaya.2002:
- United lose to Bayer Leverkusen on away goals (3-3 on aggregate) : baada ya kubeba ubingwa tulikaa miaka 4 ndio tukafuzu nusu final, wakati huo huo kama nipo sahihi sir alex alikuwa anashinda ubingwa wake wa 8 nchini uingereza. Ina maana ndani ya miaka 11 fergie ameshashinda makombe 8 ya uingereza na kombe 1 la ulaya. bayern leverkusern anafungwa fainali na real madrid kwa bao la fundi zidane, aigoooo ina maana balaa la zidane na galaticos wenziwe lilipaswa litukute sisi.
- 2007: United lose 5-3 to AC Milan on aggregate: hapa tulikaa miaka 5 ndio tukafika nusu fainal, na alifikisha ubingwa wake wa 9 wa uingereza kwa miaka 15.
- 2008: United beat Barcelona 1-0 on aggregate.= tukawafunga chelsea fainali
- 2009: United beat Arsenal 4-1 on aggregate = tukafungwa na barcelona fainali
- 2011: united beat schalke 6-1 on agregate. = tukafungwa na barcelona fainali
kwa wastani kwa kila baada ya miaka 10 sir alex ferguson ndio alibeba ubingwa wa UEFA.(1998 na 2008)
10 + 10 + 6 = 26 years akiwa madarakani.
kuna nukuu moja niliwahi kuisikia kupitia radio kifua cha mtu (stori za kibanda cha kahawa na siasa) inadai ya kwamba shujaa wa ukweli ni yule anayerudi vitani akiwa hai haijalishi hata kama hajamtoa uhai adui yeyote na si yule anayetoa uhai mamia ya maadui na baadae akafariki vitani.
kwa kuwa nimeamua kumtetea
johnmweusi muda huu basi kwa takwimu hizi za nusu fainali tu kwa maoni yangu bwana john hoja yake ni ya msingi ya kwamba timu yetu baadhi ya vipindi ilikuwa inazidiwa na wababe wengine wa ulaya hivyo basi ni sahihi kumpa heshima ferguson ya ukocha bora wa uingereza na si ukocha bora wa ulaya nzima kwa mawazo yake lakini (najitoa kwenye timu yake).
kumsifia mtu aliyefika nusu final mara saba na kubeba makombe 2 kwa miaka 20 ni sawa sawa na kumsifia mwanajeshi aliyeua wapinzani wake trillion 1.5 halafu akauliwa na jeshi mzembe anayeitwa CAG wa nchini Auditing.
anavyoamini john mweusi ni kwamba ingelikuwa sahihi kwa sir alex kupewa heshima kubwa kama angelitupa angalau makombe 5-7 ya ligi ya mabingwa kwa miaka 20 na si makombe 2 kwa miaka 20.
kwa umri wangu sikubahatika kuiona manchester united mwishoni mwa karne ya 20 lakini nilifanikiwa kuiona manchester united mwanzoni mwa karne ya 21 na siku ya leo nategemea kwa idhini ya Mungu huenda nikaiangalia mechi yetu ya leo dhidi southampton kama nitarudi nyumbani salama.
Baadhi ya mambo yaliosababisha bwana ferguson kushindwa kubeba ndoo za uefa zaidi ya mbili kwa uelewa wangu mdogo kwa kutumia GPA ya 50 ni:-
- kukosekana kwa ushindani ndani ya ligi ya uingereza kwa miaka takribani 14: haileti maana hata kidogo timu inabeba makombe 4 kwa miaka 5 nchini uingereza halafu inashindwa kufuzu nusu fainali ya ligi ya mabingwa kwa miaka 5 baadae tuseme ligi ilikuwa ni bora na kivyovyote tutakuwa tunakosea, kwa uoni wangu timu zilizokuwa nje ya uingereza inaonyesha dhahiri zilijaza wachezaji bora zaidi yetu kwa vipindi tofauti ndio maana tulikuwa tunapata tabu lakini tukirudi uingereza tulikuwa tunasumbua sana. unateswa na bayern leverkusen, dortmund, porto na nyenginezo ambazo zimewahi kututoa hatua ya 16 bora na mara tatu hatua ya makundi chini ya alex ferguson.
- kukosekana kwa makocha wanaokwenda na nyakati: makocha kama arsene wenger na wengineo ndio walitufanya na sisi kwa muda mrefu tubweteke na kujisahau kama kuna ligi inayozikutanisha timu ngumu kama bayern munich, barcelona, madrid, ac milan ya ancelotti, juventus ya marcelo lippi n.k. fikiria bwana wenger na wenzake wanamuachia ferguson abebe ubingwa mara 7 kwenye miaka 10 kivyovyote vile hali hii ilichangia kumfanya ferguson ajisahau kwa sababu alijiamisha tayari ana timu kubwa yenye uwezo wa kusimama na yeyote yule duniani kumbe ni kinyume chake. kama mzee wenger na wenzake wangelileta ushindani wa ukweli kuanzia matumizi ya fedha na umakini kwenye kufanya biashara za usajili basi ligi ingelizidi kuvutia na kuondoa gape la ubora kati ya timu kama ilivyo miaka 15 hii. fikiria mzee wenger anamsajili pascal cygan, kolo toure n.k unafikiri kwa usajili huu mzee fergie atawaacha ndugu zake wa kiingereza na wanawe wapendwa kama chadwick, brown, silvestre kwenye timu yake?
- falsafa ya ujengaji wa timu: nilipokuwa namjibu great thinker anayeitwa fuentte kuhusiana na nguvu ya man city inayoendelea kukuwa kwa kasi nilizungumzia ishu hii ya ujengaji wa timu wa ferguson ambao alitumia academy kwa mfano vijana kama brown,oshea, scholes n.k. alinunua wachezaji waliokwisha tengenezwa kwa gharama za juu kama ferdinand, nistelrooy, andy cole, dwight yorke n.k. mwisho alisajili wachezaji ambao ilibidi kwanza waje wawekwe sawa kwa mfano heinze, alan smith, ronaldo, vidic, miller (RIP) n.k. kivyovyote timu kama hii itakuwa na aina tatu ya wachezaji ambao ni wenye viwango vikubwa kama andy cole, giggs, nistelrooy n.k , wastani kama vile ronaldo na rooney mwanzoni na pia wenye viwango vidogo kama silvestre, brown, oshea n.k.
- ndio maana baadhi ya nyakati ilituchukua miaka mingi kufika nusu final ligi ya mabingwa kwa sababu wakati wewe unamsubiri chadwick, silvestre, brown, fletcher, beckham wakuze viwango vyao mpinzani wako anavunja benki anamsajili figo, zidane, ronaldo delima, rivaldo, pirlo, roberto baggio, fernando redondo n.k. kivyovyote utahitaji bahati nasibu kumshinda mpinzani wako. Ukweli mwengine ni kwamba ilikuwa ni ngumu kuwakuta average player kwenye timu za AC Milan, barcelona. madrid, bayern miaka ya mwanzoni.
- lakini ukiangalia kuanzia mwaka 2007 hadi 2010 kipindi hiki matunda ya uvumilivu yalitufanya tuwe na timu nzuri sana ndio maana tulicheza nusu final mara tatu, muunganiko wa wachezaji kama rooney, ronaldo, tevez, giggs na wengineo waliokwisha kuiva ulitufanya tuwe bora barani ulaya. Kosa kubwa alilolifanya fergie na hili nitamlaumu ni kurudia mara kwa mara kufanya biashara za average player baada ya kuwaruhusu wachezaji bora kuondoka au pindi waliposhuka viwango. kwa mfano huwezi kuwaruhusu ronaldo na tevez waondoke kwa msimu mmoja halafu unamsajili antonio valencia na michael owen kwa pamoja eti hawa baadae waje waifunge barcelona ya david villa, pedro na mtakatifu messi.
johnmweusi muache sir alex ferguson apumzike au umetumwa na mjomba wako jose mourinho ututoe kwenye mstari wa kuhoji ubora wake?
kama umetumwa mwambie watu wa JF hawadanganyiki na tunamsubiri usiku wa leo akajilinde tena na wabovu southampton na hatimaye tucheze dakika 20 bila shots iliyolenga goli la adui.
tukishafunga goli la krosi aendelee kumsifu the lord marouanne fellaini ndicho alichobakisha.
View attachment 952413
naruhusu kukosolewa ndio raha ya mjadala