eden kimario
JF-Expert Member
- Jun 13, 2015
- 10,356
- 16,400
Amemwelezea vizuri mourinho kwa kweli ndivyo alivyo mourinho siku zoteIla Hazard bhana...Moja haikai, Mbili haikai...... Soma hii mpya.
Eden Hazard ameweka wazi majuto yake ya jinsi gani muda wake na Jose Mourinho ulivyoisha na kuthibitisha kwamba anataka kufanya kazi tena na kocha huyo wa Man United.
Akifanya mahojiano na gazeti moja la nchini Ubeligiji HLN, hapo jana , Hazard alisema:
"Katika miaka 12 nilikuwa na msimu mmoja tu ambao mbaya, miezi sita ya mwisho chini ya Mourinho na kwa kiasi kikubwa ilikuwa ni kosa langu . Baada ya kutwaa Ubingwa tulimuomba Mourinho kuongeza muda wa mapumziko . Nilirudi klabu nikiwa ovyo kabisa kimwili."
"Msimu wa mwisho chini ya Mourinho hakuwa wa furaha . Hatukuwa tunashinda. Tulikuwa tunafanya mazoezi bila kufurahia, ni ilikuwa kitu kizuri kwa pande zote mbili tuachane ( Klabu Vs Mourinho ) . Lakini kama nikiulizwa sasa hivi ni kocha gani natamani nifanye naye tena kazi , nitasema Mourinho."
" Sijutii vitu vingi sana katika maisha yangu ya soka , lakini moja ambalo najutia ni kutofanya kazi tena na Mourinho pale Chelsea. Tulikuwa na timu ambayo ingeweza kutwaa mataji mengi zaidi . Tuliishia kwenye mzunguko hasi ."
" Nilimtumia ujumbe wa simu kumuomba msamaha baada ya kufukuzwa , sikuonesha kiwango kizuri sana, tulifurahia mafanikio pamoja, nilikuwa mchezaji bora wa mwaka , halafu msimu uliofuata sikuonesha kiwango kizuri."
Hazard ameongeza kwa kutetea staili ya uchezaji wa Mourinho kwa kusema:
" Picha ya Mourinho ambayo watu wengi wanaamini ni kocha wa kujihami sana sio sahihi. Sio wa kucheza sana soka la kushambulia kama Pep Guardiola , lakini ule msimu ambao tulikuwa mabingwa , tulifunga magoli mengi sana na tulicheza mechi nzuri sana."
" Kama matokeo yakianza kuwa mabaya , lazima atakosoa wachezaji wake, lakini nilishaanza kuzoea na kukubali kwasababu ndio alivyo hivyo huwezi kumbadilisha."
" Lakini ukiwa unashinda mechi, Mourinho anakuwa kocha mzuri sana huwezi kuamini, anakuwa rafiki yako , unaweza kufanya chochote unachotaka , ukitaka siku moja ya kupumzika , anakupa mbili."
Man united pogba, martial, na wengine inabidi wamzoee
Lakini atakutana nae tarehe ishirini amemsifia ili aache kupaki basi ili amfunge vizuri
