hahahahahahaaaaa nilikuwa sijaangalia marejeo ya mechi ya jana ila ndio nimeliona goli la kijana wilson muda huu, free kick kama zile nimezoea kuziona zikipigwa na mchawi kutoka uholanzi ambaye ndiye kocha wa muda huu wa uholanzi muheshimiwa
ronald koeman.
aigooooo nimeunga bando langu muda huu nataka niangalie magoli yote aliyofunga
romelu lukaku tokea aanze kucheza mpira wa ushindani, dhumuni langu kubwa nataka niangalie amefunga magoli mangapi ambayo ametoka na mpira nje ya eneo la adui, amefunga magoli mangapi akiwa amezongwa na mabeki wawili na amefunga magoli mangapi akiwa na goal kipa, hizi nafasi anazopoteza ndio ziliwafanya kina
didier drogba waonekane ni wafungaji mahiri haliyakuwa walikuwa hawawezi hata kupiga chenga.
najua watajitokeza wenye takwimu uchwara kumlinganisha lukaku na drogba.
kuna baadhi ya wachangiaji wanadai ya kwamba manchester united tuna average player wengi sana ukilinganisha na timu nyenginezo, hoja zao ni za msingi kiupande fulani lakini ninavyofahamu mimi inapotokezea mtoto ni mwenye tabia mbaya lawama zote huelekezwa kwanza kwa wazazi wake wawili ndipo huelekezwa kwa mtoto.
hivyo basi haitatokezea hata siku moja lawama za kufanya vibaya kwa timu zikaelekezwa kwa wachezaji ila kocha ndiye atakeyebebeshwa lawama kwa sababu ni jukumu lake kuwafanya wachezaji kuwa kwenye kiwango kwa muda wote na ndio maana wachezaji wakawekewa ratiba ya kufanya mazoezi chini ya mwalimu na benchi lake la ufundi.
- kama sari ball ndani ya miezi miwili ametengeneza falsafa yenye kueleweka ndani ya chelsea kwa nini jose mourinho ashindwe ndani ya miaka 3, ukimuondoa eden hazard, willian, azpiliqueta na ngolo kante chelsea kuna mwanadamu gani wa ajabu?
- juzi nilibahatika kuangalia mechi ya arsenal dhidi ya everton nilishangazwa na nilichokiona, licha ya kuwa na average player wengi kuliko hata sisi kwenye kikosi chao ila cha ajabu arsenal wameanza kucheza mpira wa kisasa na wenye kueleweka, wanaanza chini vizuri, torreira na xhaka wanakaba na kusogeza timu kwa nidhamu, bellerin anasogeza timu vizuri kuliko valencia, aubameyang anafunga na kutengeneza mashambulizi ya kueleweka kuliko mzimu wetu unaolipwa millioni 700 kwa kila wiki, kama watafanyia kazi eneo la ulinzi basi upo uwezekano wa arsenal kumaliza top 4, na tusisahau kocha wao ana miezi mitatu tokea aanze kazi kwa nini mourinho ashindwe?
mwenye namba za muheshimiwa haraka haraka anitumie tafadhali nataka kuunga mkono juhudi za wasichana kama alivyofanya julia matatiro ,naamini huku sitakutana na kisingizio cha ukosefu wa jenereta kwenye mechi za usiku.
View attachment 878528
wanakondoo muliopotea njia unapoona huwezi kushabikia timu pinzani ya kiume basi tafuteni furaha japo kutoka kwa jinsia pinzani.
usishangae utakapoambiwa ilo goli limefungwa dakika ya 86, naona wachezaji wote jezi zao hazijachafuka, au walikuwa wanarekodi tangazo la biashara?
"We knew that if we go past the seventh we were going to be in trouble with Jones, with Eric, with Lee - not good penalty takers - but we took it all well and we missed one.”.
tofauti pekee iliyopo kati ya
jose mourinho na
jamali pamba maandazi ni rangi ya ngozi zao ila wote hawapendi kuandikiwa hotuba.