Newfame
JF-Expert Member
- Feb 27, 2015
- 485
- 1,134
Yeah Sure, tuna tatizo katika beki line yote kuanzia namba 2 hadi 5, beki ambao tuna uhakika nao angalau wakiwa fiti ni Marcus Rojo na Baily, kuna haja ya kuongeza fullback mmoja kwa ajili ya kuwareplace mmoja wao kati ya Baily na Rojo wanapokosekana, Jones majeruhi yanamfanya kuwa beki wa kawaida ingawa ni beki wa uhakika anapokuwa fiti tatizo hawezi kucheza match 5 au 10 mfululizo, Valencia anahitaji sasa mbadala umri umeshaanza kumtupa mkono, Smalling naye.Tatizo tulilonalo kwa sasa ni beki na 2 na 3 tupate na kiungo mmoja mkabaj upande wa ushambulizi hamna shida lingard namuona kabadilika mno anazidi kukomaa kwa sasa rashford utoto bado ila atabadilika tu sanchez tayar kaanza kuzoea mfumo siona shida ktk ushambuliz ni viungo wetu tu kukosa viwango maalum leo wapo vizur kesho wanapoteza mipira hovyo lazima kupata kiungo mmoja wa maana wa kusaidiana na pogba
Sina wasiwasi na kwenye kiungo cha ukabaji, kwa kuwa Carric ana staff vema kuongeza kiungo mwingine kwa ajili ya buck up ya akina Matic, Pogba na Herera.
Itapendeza Zaidi kuongeza mshambuliaji ama kiungo mshambuliaji aliyekamilika kusaidiana na Lukaku.
Pamoja na mapungufu tajwa lakini timu yetu inachangmoto katika Creativity hasa katika eneo la ushambuliaji na hii ni kutokana na Falsafa ya Kocha, ya uzuaji zaidi kuliko kushambulia.
Matic anamalizia msimu akiwa hayupo katika top ten ya Viungo waliotembea km nyingi uwanjani tofauti na kawaida yake, timu yetu imezidiwa na timu nyingi katika kumiliki mpira licha ya kushinda baadhi ya michezo.
Ni vema sasa kocha kubadilisha falsafa na kucheza soka la kutumia washambuliaji wawili badala ya mmoja, kuna goal score (Lukaku ) na kiungo namba 10 (Mshambuliaji msaidizi) ili Pogba apande juu namba 8 kuongeza Creativity wakati timu inashambulia, Matic na Herera wakiwa viungo wakabaji.
So far so good jana tumeshinda lakini tunatakiwa kuwa na timu ya uhakika mwakani yenye uwezo wa kushinda match zaidi 10 - 15 mfululizo.

