Pitieni comments zangu za nyuma humu ndani kuhusu team yetu. Nilionesha wazi wazi kuwa mourinho hana uwezo wa kuipeleka hii team tunapopataka ila nilishambuliwa sana na Radika na wenzake.
Niliegemea zaidi kwenye mbinu za mourinho dhidi ya soka la kisasa. Soka la kisasa halihitaji kucheza kwa kujihami. Soka la kisasa kujihami ni wewe kushambulia ili team pinzani wasije golini kwako na sio kupack bus unawaruhusu maadui kuja golini kwako kila muda, hiyo ndio Njia ya kisasa na aina ya uchezaji wa kisasa.
Team yetu sasa hivi imekuwa ikishinda watu haturidhiki kwa sababu ya kiwango kibovu. Ikifungwa pia haturidhiki.
Niliwahi kusema humu na ninaomba mpitie tena muone kwamba chini ya Mourinho wachezaji wengi wataonekana wa hovyo licha ya kuwa wachezaji wazuri hapo awali ... Nilisema micktaryan ( Bahati nzuri tayari tumepata ushahidi kumechotokea). Nilimtaja Pogba ( Tunaanza kuona ), anaefuatia ni Lukaku. Na wengine wengi.
Huwezi kuniambia wachezaji wote hawa kiwango chao kimeanguka kwa sababu za uwezo wao binafsi kushindwa kulisakata Kabumbu. No. Sababu ni Mourinho. Nikipata muda nitakuja kuezelea sababu za kiufundi kwa nini lundo la wachezaji wa team yetu viwango vyao vimeonekana kuwa domant kwa mbinu za kipuuzi za Mourinho. Leo tunamlaumu Lukaku ,niwaulize swali hivi Jana usiku striker Wetu Jana mfumo wa kiuchezaji wa team umemtengenezea Nafasi ngapi ???? Wote tuliona Nafasi walizotengeneza sevila na De gea kuokoa ,Je, Nafasi nyingi vile Kama zingekuwa kwa upande wa Manchester united tungeshindwa kweli kufunga . Siri ya mpira na kufunga magoli ni kutengeneza Nafasi nyingi. Nafasi chache unajipa Nafasi ndogo ya kufunga magoli. Kwa aina ya uchezani Wetu wa kujihami team haitengenezi Nafasi tutafungaje ????
Narudia tena Mourinho hafai hafai hafai .... Atatuharibia wachezaji viwango
Nawakumbusha tu, hivi ni lini mwisho team yetu ilifunga goli la kona