radika mimi siamini kama ile ilikuwa ni game plan eti kwa ajili ya kujipanga na mechi ya chelsea isipokuwa ndio style yetu tunayocheza kwa takribani mechi tano zilizopita na jaribu kurejea mechi ya tottenham, newcastle, huddersfield, burnley na hata mechi yetu ya FA tuliocheza tena na huddlesfield town. leo sevilla walipokuwa wanashambulia unakuta zaidi ya wachezaji 6 wanavamia eneo la adui lakini kwetu sisi ni lukaku peke yake ndiye anayesimama mbele ya eneo la adui.
- mechi ya huddlesfield mpaka naondoka baada ya kuchoshwa na soka bovu half time tumepiga shoot target mbili au unataka kuniambia ya kwamba mechi ya huddlesfield tulicheza mpira ule kwa ajili ya kujiandaa zaidi na sevilla ili wachezaji wetu wasipate majeruhi?
- eneo la ulinzi kiukweli tunajitahidi sana lakini kwenye ushambuliaji tunacheza ovyo na tatizo linaanzia kwenye kupanga mashambulizi wachezaji wetu hawasogei eneo la adui kwa ajili ya kumpa ushirikiano lukaku a.k.a mtu mzito, matokeo yake mipira mingi sana wanainasa timu pinzani.
- na kwa style hii tunayocheza mechi nne zijazo tutamchoka alex sanchez kwa sababu haiwezekani sanchez akimbie na mipira lakini akifika kwenye eneo la adui anamkuta lukaku peke yake, akina matic, pogba, lingard, mata wote wanajificha nje ya box la adui kwa kuhofia eti adui ataunasa mpira na kupiga counter attack, hahahahaaaa adui wenyewe unayemuhofia ni newcastle united na sevilla ambayo midfield wake ni nzonzi ambaye aliuzwa na stoke city.
- tatizo jengine nililoliona kwenye timu yetu ni kukosa kujiamini kwa wachezaji wetu, ndani ya dakika tisini chris smalling anarudisha mpira kwa kipa mara kumi, ndani ya dakika tisini ashley young atapiga pasi mbovu na long ball mbaya zaidi ya 10, ndani ya dakika 90 lingard atapoteza mpira na kufanya maamuzi mabovu mara 6,inashangaza sana kwa proffesional player kuwa na uoga uliopitiliza,inafika wakati unajisikia aibu hata kuangalia mechi zetu za marejeo, zaidi ya wachezaji sita wa kikosi cha kwanza ni wazito wa kufanya maamuzi wanapokuwa na mpira.ukimuangalia umtiti na smalling unahisi utofauti mkubwa sana wa kiuchezaji.
- uwezekano wa kuifunga sevilla mechi ya marejeo ni asilimia 80 lakini uwezekano wa kubadili aina ya soka letu chini ya jose mourinho ni asilimia 10 tu.hata kama tutatumia pound millioni 300 kwenye dirisha la usajili chini ya jose mourinho soka letu halitabadilika, tafsiri yake ni kwamba tutakapocheza na man city, liverpool, chelsea, arsenal na totenham wakiwa nyumbani kwao tutaendelea kucheza mpira wa kujilinda zaidi.
- kama mourinho anahitaji mafanikio anapaswa pia aache kusikiliza kelele za waingereza, huwezi kumkuta mchezaji kama lingard, ndani ya bayern munich na real madrid akicheza kikosi cha kwanza nafasi ya kiungo wa juu, hata kama lingard atafunga bao 40 kwa msimu lakini ukweli utabaki vile vile kuwa uwezo wake hauendani na brand ya manchester united na hata ashley young na rashford naye hivyo hivyo, munaweza kunipinga kwa rashford lakini tukumbuke hata walcott alikuwa maarufu sana alipokuwa na miaka 18 na waingereza waliamini atakuwa bora atakapofikisha miaka 23 lakini cha kushangaza kadri umri ulivyokuwa ukiongezeka kitu pekee kilichokuwa kikiongezeka kwa walcott ni sura nzuri na ndevu, yuko wapi danny welbeck ambaye alifananishwa na dwight yorke?, yuko wapi tom cleverley aliyekuwa akishindanishwa na fabregas? yuko wapi wilshere aliyewafundisha mpira midfield maestro xavi na andres iniesta? yuko wapi sturridge? kuwa na matumaini ya kwamba siku moja rashford atakuwa mfungaji hodari kuliko thiery henry ni ujinga zaidi ya kuamini ya kwamba siku moja jose mourinho atacheza mfumo wa total football akiwa uingereza.
david degea >= ederson
valencia == walker
ashley young +shaw == fabian delph + mendy
bailly >= kompany
smalling == stones
jones == otamendi
laporte == lindelof
matic == fernandinho
mata <= david silva
pogba <= kelvin debruyne maestro
martial >= sterling
rashford <= gabriel jesus
lukaku < aguero
lingard < leroy sane
sanchez > bernardo silva
herrera == gundogan