Sikatai na wala sipingi Mou kuendelea kuwa kocha wa Man United kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kibiashara, na ninapoongelea Soka la Kushambulia na kasi simaanishi soka la Asernal or Liverpool, naongea Falsafa, Barca wanacheza Sexy football na wana makombe ya kutosha.
Man United kwa kikosi cha Msimu huu haina sababu ya kujilinda au kucheza kwa kuhofia/kupack basi, tuna kikosi kizuri na kikubwa.
Tuna Kipa ambaye kwa sasa ndio Kipa namba moja duniani, mabeki wazoefu na wazuri, Viungo na washambuliaji wa uhakika, kinachotukwamisha ni Falsafa yetu tu.
Tunapack bus had kwa Benley? Tunafunga na timu ndogo, timu kama Crystal Palace nayo ni ya kuipakia bus.
Tuache wachezaji wafunguke, tushinde goli nyingi na soka liwe la uhakika hata hizi timu ndogo zitatuogopa kama ilivyokuwa enzi za SIR Alex.
Tulikuwa hatufungwi na timu za kijinga jinga au dro kama tunazopata sasa.
Mfumo wa kujilinda unazifanya hata timu ndogo kutudharau, soka lina kuwa sio la uhakika, ushindi unakuwa wa tabu au shida.
Wachezaji wanapoteza confidence na Radha ya Mpira, waone akina Martial, Mikh, Rashford n.k
Rashford alikuwa anakuja vizuri lakini mfumo unamfanya apoteze Confidence, akiwa timu ya taifa anakuwa tofauti na akiwa kwenye Club.
Martial amepoteza nafasi timu ya Taifa n.k
Enzi za SIR wachezaji wa timu yote walikuwa wanaitwa kwenye timu zao za Taifa.
Mbinu, Itikadi na Falsafa za Mourihno zinaenda kuua confidence na vipaji Old T tuwe wakweli.
Ni shabiki wa Man U since msimu wa 97/98.
Naijua vizuri, sawa tutachukua makombe lakini sio kwa mbinu sahihi.
Magwiji na Mafundi wa Soka wote wanamlaumu Mourihno kwa mbinu zake, tumeona kwa Scoles, Gary Nevel, Gigs na hata Sir Alex.
Ni kweli heshima yetu imerudi nje ya uwanja na si uwanjani, uwanjani bado tunasumbuliwa na timu ndogo.
Hatuna uhakika wa ushindi kwa match zaidi ya tano.
Bado tunashumbuka kupata ushindi hata kwa timu kubwa za top 4.