Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

875d731c3648aceb5b25766b48587ce8.jpg
 
wapo kwa ajili ya sub dakika kuanzia ya 86
Nadhani kama umeshindwa kusoma kikosi cha leo hapo juu... basi ungejiuliza tu swali dogo... Kwanini jamaa kauliza hivi?

Hao jamaa wote hawapo kwenye ubao wa wachezaji wa akiba kwa mechi hii.
 
Sergio Romero ataanza dhidi ya CSKA Moscow kutokana na David De Gea kupumzishwa baada ya kazi kubwa wikendi iliyopita
Manchester United wanahitaji sare au ushindi wa aina yeyote ile dhidi ya CSKA Moscow ili kuweza kuwa kinala wa Kundi la A.
Cska Moscow kwao ni mechi muhimu sana kwani wanahitajika kushinda kwa ushindi wa aina yeyote huku akimuombea Fc Basel apoteze au atoke sare dhidi ya Benfica

Mourinho ameahidi kuichukulia mechi hiyo kwa uzito mkubwa, licha ya kuwa ana kibarua kigumu kwenye Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya Manchester City Jumapili.
Amesema: "Mimi nitafanya mabadiliko machache lakini sio mabadiliko mengi sana. Bado hatujafuzu na sifa bado kuna vilabu vingine pia vina nafasi ya kufuzu ninahitaji kuweka usawa fulani katika timu. "
 
TAARIFA KUHUSU HALI YA KIKOSI

Mourinho ameamua kumpunzisha kipa David de Gea, kufuatia mechi dhidi ya Arsenal Jumamosi. Kocha wa United amethibitisha kwamba Sergio Romero ataanza katika mchezo huo huku Joel Pereira anatarajiwa kuanzia benchi.
Luke Shaw kuna uwezekano wa kuanza kwa mara ya kwanza tangu Oktoba 24, wakati Paulo Pogba, ambaye amesimamishwa kwenye Ligi Kuu na hivyo kuhukosa mchezo wa dabi siku ya Jumapili dhidi ya Manchester City, anatarajiwa kucheza kwa dakika zote dhidi ya Cska Moscow
Eric Bailly, Phil Jones, Marouane Fellaini na Michael Carrick wote wataukosa mchezo huu kutokana na kuumia pia Zlatan Ibrahimovic ana nafasi ndogo ya kucheza

TAARIFA MUHIMU KUHUSU MCHEZO HUO

Katika mechi tano za Mwisho CSKA Moscow haijawahi kuifunga Man United, wamepoteza mara tatu na sare mbili tu, zote zikiwa kwenye hatua ya makundi kwenye Ligi ya mabingwa. Pia katika mechi hizo tano zote wameruhusu goli.
Man United wamepoteza mechi 2 kati ya 48 Old Trafford kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya mabingwa, wameshinda 34 na sare 12, wamefungwa na Besiktas 2009 na Cluj

2012. CSKA Moscow wamefanikiwa kushinda mechi zake zote mbili za ugenini kwa msimu huu
CSKA Moscow wameshindwa kuvuka hatua ya 16 katika misimu minne mfululizo waliyoshiriki huku mara ya mwisho kufuzu hatua ya 16 ni msimu wa 2011/2012 ambapo walienguliwa na Real Madrid
 
Manchester United XI: (3-4-1-2): Romero; Lindelof, Smalling, Blind; Valencia, Pogba, Herrera, Shaw; Mata; Lukaku, Rashford.

Manchester United Substitutes: Pereira, Martial, Lingard, Young, Darmian, Tuanzebe, McTominay.
 
There are six changes to the Manchester United side that beat Arsenal 3-1 at the weekend. Sergio Romero takes the place of David de Gea in goal as expected, as well as Paul Pogba starting in midfield. Daley Blind replaces Marcus Rojo defence, while Ashley Young is replaced on the left-wing by Luke Shaw. Up front, Marcus Rashford and Juan Mata come into the side in place of Jesse Lingard and Anthony Martial.
 
Back
Top Bottom