Kwa kifupi leo tumeshinda bila kucheza vizuri hiyo ni dalili ya kuchukua ubingwa
Mi naona tofauti,tumeshinda kwa sababu tumecheza vizuri,L.city sio timu ya kubeza,angalau wamekuwa kipimo kizuri kwetu,hasa kutathmini plan za kocha wetu.
L.cty kimpira hawana tofauti na Man City this season kama umewaona Man City,wanashambulia kwa muda,wanakaba sana na kuzuia timu pinzani isicheze katika game plan yao,walifanikiwa hili katika kipindi cha Kwanza.
Kipindi cha Kwanza tuliposhindwa kupata goli kocha hakuwa na Jinsi zaidi ya kuhamia plan b ya game plan yetu nayo ni kuforce pale Mbele ili magoli/ushindi upatikane huku tukilinda tusifungwe,and always Big Fella aka Fundi Mao ameendelea kuwa game plan B yetu.
Tukiwa tumeshinda Big Fella huja kuzuia na kulinda ushindi wetu,tukiwa tunahitaji ushindi Big Fella huja kuhold mipira pale mbele huku akizuia timu plan kushambulia aka Mkata Upepo.
Vizuri Mou ni mzuri katika game plan,L.city walikuwa na nia ya kujilinda/kuizuia Man U wasicheze mpira wao,ndio mana leo unaona Matic alicheza zaidi nyuma,hakucheza mpira wake tuliouzoea,L.city walifanikiwa katika hili,huku wakitafuta angalau goli 1 la kushtukiza ili wajilinde zaidi.
Na kama wakifungwa basi isiwe kwa Magoli mengi,nimefurahi kuona sasa Man United ikianza kuogopwa nje ya Uwanja, timu inakuja uwanjani na game plan ya kutuzuia au kuzuia kufungwa goli nyingi na sio kuja kutufunga kama misiwi mitatu iliyopita,hii itatusaidia sana msimu huu kwa vitimu vidogo kuvipiga mapema.
L.city nia yao ilikuwa ni kuizuia United bahati mbaya sio kwa United hii ya Kiungo cha Matic na Pogba,na wangefunguka wangepigwa nyingi sana.
Katika Match hii nilitegemea kuanza na viungo watatu, Matic,Herera na Pogba sijajua kwa nini Mou amemiacha Herera, ila naamini Mou ameona kitu Match zijazo za namna hii naona Herera atapewa nafasi,ni mzuri timu pinzani inapokuwa na game plan ya kushambulia na kuzuia kwa wakati mmoja.
Kuanza na Martial badala ya Rashford ni game plan tu hii ni baada ya Consistence nzuri ya Martial kwenye match mbili zilizopita.
Tofauti ya Martial ni mzuri timu inapokuwa imeshashinda tofauti na timu inapotafuta ushindi while Rashford ni mzuri timu inapokuwa inatafuta ushindi,kucheza wote kwa dakika chache ni dhahiri tulikuwa tunatafuta ushindi wa goli zaidi ya mbili.
Nimependa Sub za leo,Matta na Mikh kuwapisha Fellain na Rashford,Mata bado anaendelea kutafuta fitness yake uwanjani baada ya majeruhi ya muda mrefu,anendelea kucheza vema lakini hastahili kucheza dakika zote tisini,bado mpira haujaanza kumtii,n adhani na umri nao umeanza kumtupa mkono.
Mikh bado anatakiwa kumshawishi kocha bado hajawa na makali yake kuifanya timu kumtegemea yeye zaidi, ana kazi ya zaidi katika hili ili kuja kuwa Star wa timu.
Hadi sasa mashabiki hatumtegemei yeye zaidi badala yake tunamuangalia Lukaku,Matic,Rashford au Martial na Pogba katika kutupatia ushindi.
Samtime naonelea Namba 10 ni bora akacheza Rashford kuliko Mikh au Mata.
Lukaku hakuwa na bahati katika hii match but ameendelea kuonesha tofauti pale mbele,jamaa ni zaidi ya simba mwenye njaa Mbele ya kundi la pundamilia,anahangaika uwanja mzima.
Tuendelee kutegemea mabadiliko makubwa kutoka kwa Pogba,ameanza kutafuta nafasi yake kama Pogba,mashuti yake yananikumbusha enzi za Scolse.
All is well,Huu msimu ni wetu.
Timu kidogo itakayotusumbua this season ni Liverpool,jamaa wana kikosi tofauti kidogo hasa pale mbele lakini tuna Herer na Matic kati, Baily na Darmian.
Natamani kuona kurejea mapema kwa Roho kabla ya kukutana na Majogoo wa Jiji.
Sent using
Jamii Forums mobile app