Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Screenshot_2017-08-27-09-03-18.png
 
Nimeangalia hailaiti za OUSMANE BEMBELE, dogo anaonekana ni fundi sana, sijui kwa nini barcelona walikua wanang'ang'ania kwa coutinho, anastahili kununuliwa kwa ile hela kutokana na soko lilivo sasa, mou hakumuona yule dogo mpaka na yeye kung'ang'ana kwa perisic?

Sent using Jamii Forums mobile app
Upo sahihi sana mimi mwenyewe dembele ameniacha na mshangao mkubwa sana kutokana na kipaji chake hususan kwenye kudribble mpira. Ila hatupaswi kumlaumu mourinho kwa kushindwa kumfatilia dembele ila maskauti wa timu ndio wanapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kuona kipaji chake alipokuwa ufaransa na mpaka dortmund wanamsajili kwa pesa kidogo mnoo.kwa wakati huu ambapo soko la usajili limekuwa baya club inapaswa kuwa na maskauti kila kijiji ili kuhakikisha wanapata wachezaji vijana wenye ubora kwa bei nafuu.inashangaza kuona dortmund sasa hivi wana skauti wazuri kuliko timu yetu.
 
Jones hatari sana sioni nafasi ya smalling kabisa pale akirudi na rojo ndo itakua balaa.

Xmass Boy.
  • Smalling na bailly hawaendani wanapocheza pamoja
  • Fellaini na pogba hawaendani wanapocheza pamoja na ndio maana msimu uliopita licha ya kuwa tulishinda mechi za mwanzo lakini kiwango kilikuwa hakiridhishi na bahati mbaya sana ilimchukua jose mourinho zaidi ya miezi 3 kuweza kugundua suala hili mpaka tulipodhalilishwa na chelsea ndipo akaanza kubadilisha chemistry na kumuanzisha rojo na herrera kwenye 4-2-3-1. kwa uoni wangu mimi mafanikio ya timu yetu msimu huu kuanzia pre season yamechangiwa zaidi na jose mourinho kuweza kuwatambua wachezaji mmoja badala mmoja.
  • ili smalling apate nafasi ni lazima aumie bailly na kuumia kwa jones hakumaanishi kama smalling atapata nafasi ya kucheza na bailly ila marcos rojo ndiye atakayepata nafasi ya kucheza kwa sababu anaendana na bailly.
  • Kama lindeloaf atashindwa kuendana na kasi ya timu tafsiri yake ni smalling naye ameshindwa kuendana na kasi ya timu hivyo basi ataendelea kukaa benchi.
 
Upo sahihi sana mimi mwenyewe dembele ameniacha na mshangao mkubwa sana kutokana na kipaji chake hususan kwenye kudribble mpira. Ila hatupaswi kumlaumu mourinho kwa kushindwa kumfatilia dembele ila maskauti wa timu ndio wanapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kuona kipaji chake alipokuwa ufaransa na mpaka dortmund wanamsajili kwa pesa kidogo mnoo.kwa wakati huu ambapo soko la usajili limekuwa baya club inapaswa kuwa na maskauti kila kijiji ili kuhakikisha wanapata wachezaji vijana wenye ubora kwa bei nafuu.inashangaza kuona dortmund sasa hivi wana skauti wazuri kuliko timu yetu.

Kwanini muwalaumu Mascout wa timu? Mnafikiri hao mascout hawajawahi kumuona? Sawa anaweza kuwa mzuri, je anafit kwenye mipango ya Mourinho? Kama angekuwa anamtaka seriously sidhani kama angekaaa kimya, kocha mwenyewe Mourinho na klabu yenyewe Man Utd yaani hawajui kujibana, wanapata wanachokihitaji.

Hivyo sioni sahihi kumlaumu kocha wala Mascout wetu. Turidhike, mbona timu naona ina dynamic nzuri tu? Pace services zipo, strong attacking services zipo, Penetration services zipo, so hata kama tukikosa natural winger bado kuna watu wanaweza kucheza vizuri tu nafasi hizo.
 
Hapa West Brom pekee ndo ana uhakika wa kuwa na point sawa na sisi endapo atashinda leo.

Otherwise, gape la points limeanza kuonekana.

Mechi tatu nyingine zijazo tukishinda kwa goli nyingi, basi sioni wa kutupokonya kombe.
Hahaha ndo unavyowaza hivyo. ..

Pole sana.

Soon tu kila timu itarudi kwenye nafasi yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Game za Manchester sasa hivi kuzitazama zinasaidia kuondoa harara, chunusi, utangotango.. zinarudisha mvuto, zinaongeza nguvu za kiume, kupandishwa cheo kazini, inaondoa mikosi pamoja na nuksi, vile vile inaongeza vitamini D na kurudisha hamu ya kula.. KWA PAMOJA TUENDELEE KUZITAZAMA
 
Back
Top Bottom