Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

439700F400000578-4826082-image-a-59_1503773190813.jpg
 
Idadi ya magoli ambayo Manchester United imefunga katika dakika 15 za mwisho kwenye mechi za ligi kuu:

2015-16 (38 games): 9
2016-17 (38 games): 11
2017-18 (3 games): 6

Kwa msimu huu pekee tumefunga goli 6 ndani ya dakika 15 za mwisho. Sijui wengine mnaonaje ila kwa upande wangu natamani team ijitahidi "ku-kill" the game mapema zaidi ili hizo dakika 15 za mwisho tuwe tunacheza kutafuta magoli ya ziada na sio magoli ya ushindi.
 
Hii tabia ya MUFC kuwabomoabomoa wenzao magoli manne manne imeanza kuniathiri maana tukishinda chini ya hizo naona kama tumepoteza..

Upo sawa kabisa.

Jana nilikuwa kwenye harusi, nikawa nafuatilia kupitia livescore.

Nilivyoona tumeshinda goli mbili nilipooza sana.

Huwa siridhiki na magoli kabisa., tukishinda 4 ntaanza kujiuliza kwanini tusishinde 6 au 7?
 
manchester united ndio timu pekee duniani ambayo wachezaji wake wanawania kuanzia benchi kwenye mechi.
  • lord fellaini akianzia benchi akiingia anabadilisha movement nzima ya timu
  • martial akitokea benchi anafunga magoli
  • rashford akitokea benchi anafunga magoli
  • lingard akitokea benchi ana assist magoli nina wasiwasi mechi ijayo martial na rashford watagoma kuanza kikosi cha kwanza kwa sababu kila mmoja atamtegea mwenzake hivyo basi jose mourinho anapaswa aende uwanjani na bakora kama mwalim wa madrassa.
rashfordmartial-cropped_1i9jzt6vzgiv51q4pnxp3r54y5.jpg

Mechi ijayo nna uhakika Rashford ataanza.

Stoke City huwa wanaharibu sana furaha za timu kubwa.

Ni ngumu kuifunga Stoke City kuliko Arsenal au Liverpool.
 
Back
Top Bottom