Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Msimu utakua mgumu sana na wakuvutia sana. Usajili utakaofanyika ndio itakua pona ya timu.
Je unaamini katika usajiri tu ndiyo mkombozi?! Vipi kwa timu kama Tottenham ikiwa na vijana hodari na machachali na msimu uliopita walianza tengeneza chemestry na ilionekana ambayo mimi naiona ndiyo bora je wasipo ingia katika soko la usajiri wataweza teteleka msimu huu? Ikiwa bado ilikuwa na mtaji wa vijana wao ambapo kwangu kama yasingekuwa majeraha nilianza kumuona MARCELO wa EPL yaani Dany Rose pamoja LAMELA je unaweza iweka nafasi ipi timu kama hii.?
 
Kumbuka lakini sisi ni mabingwa wa Europa Ligue na ni misimu mitatu kabla ndio hatukufanya vizuri na Viashiria Vyote vinaonesha kurudi kwa ufalme wa Man U next season.

Huwezi ifananisha Liverpool na Man United chief katika hiyo Scenario yako.

Sisi kwa miaka miwili mfululizo licha ya kutokuchukua ubingwa bado tuliongoza kwa mauzo ya Jezi na thamani ya brand Yetu,Man United ndio timu yenye thamani Mbele ya Real Madrid iliyochukua UEFA championship mara mbili mfululizo.

Kwa takribani miaka 10 mfululizo man United haijawa kuwa chini ya namba mbili kwa timu zenye uwezo wa kifedha na thamani.

Hivyo ni rahisi kwetu kuingia sokoni na Zaidi ya 200 mio pounds kununua wachezaji na Makocha kitu ambacho Liverpool hawawezi.

Man United pekee ndio yenye uwezo wa kupambana na Real Madrid sokoni na ndio mana tuna rekodi ya Mchezaji ghali Zaidi Duniani na tunakaribia kutoa 75 kwa ajili ya Lukaku na 45 kwa ajili ya Matic na bado tunaweza kutoka 80 kwa ajili ya Morrata,kitu ambacho Liverpool hawakiwezi.

Ukija kwenye Makocha now tuna World Class kocha ambaye sina hakika kama Liverpool inaweza kumchukua na kumlipa.
Naijua Man Utd haiwezi kurudi level itachukua miaka hata kumi au zaidi. Kwani nyota kusajiliwa ni tatizo. Kama ni biashara hata arsenal wanafanya hawana loss wamejaza pesa tu jiulize nini kinafanyika. Itabaki story tu.
 
Je unaamini katika usajiri tu ndiyo mkombozi?! Vipi kwa timu kama Tottenham ikiwa na vijana hodari na machachali na msimu uliopita walianza tengeneza chemestry na ilionekana ambayo mimi naiona ndiyo bora je wasipo ingia katika soko la usajiri wataweza teteleka msimu huu? Ikiwa bado ilikuwa na mtaji wa vijana wao ambapo kwangu kama yasingekuwa majeraha nilianza kumuona MARCELO wa EPL yaani Dany Rose pamoja LAMELA je unaweza iweka nafasi ipi timu kama hii.?

Bila ya kuongeza nguvu Totenham haitoweza kuchukua ubingwa,lazima wasajili lakini sidhani kama watasajili mchezaji wa gharama kwasababu wanamalizia uwanja wao.
Labda wakimuuza Walker watapata pesa ya kusajili.
Kwenye kuchukua ubingwa,hilo sahau. Hawana kikosi cha kuchukua ubingwa,wao wataendelea kuleta presha kama misimu mingine tu.
 
Hivi ni soko limebadirika ama uwezo maana dah SANCHEZ anamjambisha Wenger anataka 400 kwa wiki. Lemar uhamisho wake wanataka 80 dah.!
Hali ya Soko limebadilika sana siku za hivi karibuni,hii ni kutokana na uwepo wa Mawakala wa Michezo ambao wao huang alia Zaidi pesa kuliko uwezo wa Mchezaji,lakini vile vile hali hii huakisiwa na ongezeko la Mapato yanayopatikana kutokana na mchezo wa Mpira wa Miguu,mara nyingi timu hufaidika Zaidi kuliko mchezaji ndio mana hawa akina CR7 na Mwenzake Messi wamelibadilisha sana soko la Ulaya la Mpira wa Miguu kwa kulifanya kuwa la biashara Zaidi kwa kila wanachokifanya na hii kupelekea mawakala nao kuanza kuzipiga timu kupitia kwa wachezaji wao.

Let's imagine kwenye dunia ya sasa unadhani Zidane angeuzwa kwa kiasi gani?Ronaldinho?

Leo hii Lukaku anapatikana sokoni kwa 75,hazard 85,Morrata 80 na e.t.c

Gareth Bale alinunuliwa sijui kwa 80+ aaaah na hawa Marais wa Vilabu pia wanachangia kuharibu soko la Ulaya.

Soon nadhani UEFA na FIFA watapitia upya hili soko na kuunda chombo kwa ajili ya kuregulate soko la wachezaji Ulaya ili kubalance timu mana ni wababe na vilabu vyenye uwezo ndio wanaoweza kununua world class players pekee timu nyingine zitachemka so kunaweza kutengenezwa kizazi cha timu 5 au 4 Ulaya ambao ndio watakaoweza kutwaa makombe.

Na hii now tunaiona kwenye League za Spanish,Ufaransa,Ujerumaini na Italy ambazo ni mbili au moja ndio zinazoshinda makombe.

England ni kwa sababu ya timu nyingi kuwa na pesa ndio zinazosababisha ubingwa kutokutulia mahala pamoja.

Wachezaji wamekuwa wakilipwa mishahara mikubwa na kuwa na mikataba yenye thamani kubwa,hizi pesa kwemye Mpira saa nyingine ni kufuru.

Leo Mess analipwa mshahara wa us Dollar 400 kwa wiki,Ronaldo 350,Rooney 300 bila mapato yao binafsi.

Huu Mshahara wa Mess unaweza kuwalipa wachezaji wote wa Bantley pale England au au Betis kwao Spain.
 
ea49daae483b80c495c956f15a11f599.jpg
 
Romelu Rukaku is a decent player but he will need to work harder when he get to Manchester United to be like Tevez, Ibrahimovic or Rooney when he was younger. He will need to improve his link up play, back to the goal work and his first touch to become legend at Man Utd. On other hand is strong, pace and great finisher, therefore if he work on his game he might become one of the best in the world and United Legend. Time will tell.
Rooney first touch was and is still awful but that deficiency never fetters him from becoming Manutd legend.

Why?

His goals made him a legend and so will Lukaku be if he scores 25+ a season for Manutd
 
Jana nilimsikia shabiki mwenzetu wa Manchester united anasema dau la kumsajaili Lukaku ni kubwa Sana na yeye anaumia sana kuwa Lukaku hana hiyo thamani,

Nilicheka sana how come unaumia kwa hela usiyoitoa wewe... Ushabiki wetu wa simba na yanga wa kutaka tuwe involved kwa kila kitu kwenye team uwe na mipaka jamani ... Sisi tujiandae na Kupiga kelele kwenye vibanda umiza financial issues za team hazituhusu


GGMU
Mashabiki hela siyo sheda bali kufungwa hutuachia simanzi nzito
 
Naijua Man Utd haiwezi kurudi level itachukua miaka hata kumi au zaidi. Kwani nyota kusajiliwa ni tatizo. Kama ni biashara hata arsenal wanafanya hawana loss wamejaza pesa tu jiulize nini kinafanyika. Itabaki story tu.
Bro unaongea kama shabiki wa Mpira anayeujuwa mpira au unataka tujaze Sever tu hapa,any way kwa faida yako na wengine acha tuendelee na mjadala na hivi leo ni sabasaba so we're free.

Mafanikio ya Timu Yeyote yanategemea Vitu Vinne, Moja historia au ukubwa wa timu kiasili sifa hii nadhani timu hizi zote mbili zinazo Liverpool ndio wanaongoza kuchukua UEFA champion Zaidi ya Man U lakini wakifatiwa na Man United lakini katika historia Man United ndio mbabe kwa kuchukua makombe pale EPL,mbili uwezo wa kocha kwa misimu Zaidi ya mitatu tulikosa World class kocha,Moyes hakuwa top cocher duniani wakati anasajiliwa kuja kufundisha Man United,uwezo wa wachezaji binafsi,baada ya Ufalme wa Sir Fegurson ambaye aliweza kuwatengeneza wachazaji wa kuwa kuja kuwa World Class top player,aliopondoka waliomfatia walishindwa kuwa na uwezo huu na kufanya kuona vipaji halisi vya wachezaji wetu, na thamani ya timu katika kuvutia Wawekezaji, kulipa na kununua wachezaji wapya Wenye uwezo,Moyes na Van Gaal hakujuwa ukubwa wa Man United hawajuijuwa thamani halisi ya Man United na ndio mana uliona usajili wa kwanza wa Mou na Wenye thamani ni kumchukua Fellain ambaye hakuwa mchezaji Mkubwa Ulaya.

Van Gaal yeye katika utawala wake aliuza wachezaji wengi wazuri kama Chicharito na kutuletea wapaka Poda wake.

Any way tulikuwa ni kipindi cha Mapito na Mabadiliko now timu ipo kwa kocha mwenye kujuwa Vyote hivi na nzuri Zaidi anajuwa Kiu ya Mashabiki wake.

Bodi ya Man United inakiri kuwa ilifanya makosa makubwa sana kukubali timu kuachiwa Moyes na ndio tulipoanza kuyumba,Van gaal ni top class kocha alitusaidia kutengeneza barabara lakini alipishana na Falsafa ya timu.

Sasa Mou ni mtu sahihi pale Man United anaendana na Falsafa ya timu,ni kocha Mkubwa hivyo anahitaji na timu iwe kubwa na ndio mana aliweza fanya usajili wa uhakika na Mkubwa kurudisha hadhi ya Club Yetu.

Asernal wanakosa baadhi ya Sifa hapo kaka,Asernal sio timu kubwa Ulaya ni timu kubwa England so sio vizuri kuifananisha na Man United,Yes wanafanya vizuri sokoni lakini sio timu yenye kulipa wachezaji mishahara mikubwa sio Wenye kutoa pesa ndefu kwenye usajili.

Asernal imesajili nadhani ni wachezaji wawili top class players kwa misimu miwili ya hivi karibuni lakini sio timu kubwa kuifananisha na Man United na ndio mana wanakosa mbinu za kuchukua makombe.

Nimekwambia tumerudi katika ukubwa wetu au Level Yetu, Man United ni Mabingwa wa Uropa Legue,Kombe kubwa la pili bara ni Ulaya sasa hiyo miaka kumi ipi unayosema.

Kutwaa EPL msimu wa 2017/2018 tusubiri sina shaka na hili,mana hata msimu uliopita zile droo zingebadilika tungeongea mengine.
 
Japo sijawahi changia humu jukwaani ila kwa hili naomba nichangie kidogo kwa ufahamu wangu.

Navyo jua jinsi timu zinavyo sajili wachezaji kwa bei kubwa na mishahara mikubwa hii inapelekea gharama za uendeshaji wa timu kuongezeka. Kwa kuongezeka huko gharama mauzo ya TV rights zitapanda sababu timu ni brand na gharama ya kuendesha hiyo brand imepanda. Kwa hiyo mfano DSTV itabidi alipie gharama kubwa hali itayo pelekea na wao kupandisha bei za huduma. Mwisho wa siku sisi wa kibnda umiza tutakuja kulipia bandani pale. Sasa katika hiyo scenario usiombe na thamani ya pesa yetu ishuke dhid ya dollar.

Kwa hiyo kwa namna moja au nyingine na sisi inatuathiri.
Haiko hivyo
Kupanda kwa dau la TV rights ni ubora wa EPL siyo gharama za uendeshaji kupanda

Ila gharama za uendeshaji zimepanda kutokana na mapato ya TV rights kupanda na kupaaisha matarajio ya wauzaji wachezaji ya kuwa timu za EPL wanazo....they can afford to pay those crazy fees

Ila ubora wa ligi ya EPL ukishuka basi na TV rights zitashuka na madau ya usajili, mishahara ya wachezaji kuporomoka

Madau pia yanapanda kwa sababu makocha hawataki kuwaamini wachezaji mahiri nje ya European ligi wakati Africa na South America kuna vipaji vingi lakini EPL hawawataki kwa madai hawana European experience

Timu ndogo za EPL nazo hukosea kuhangaika na kusaili wa kwao kwa madau makubwa mwishowe hufilisika kumbuka LEEDS UNITED wako wapi leo

Nionavyo, umiliki wa hizi timu utachukuliwa na mabilionea vinginevyo uendeshaji wake tuendako hata hizo TV rights, udhamini, mapato ya milangoni n.k hazitafua dafu na mishahara na tozo za usajili zitaendelea kuwa juu ya bei stahiki za soko
 
Ni kweli lakini angalia ni kwenye mechi zipi kapata magoli mengi...yeye sio day to day scorer...akiwakuta vibonde anawanywa goli za kutosha...mechi za maana haonekani kabisa
Mind you still tuna UCL ambako ni league ya wakali tu wa ulaya
Musimu uliopita tulipoteza pointi nyingi na timu ndogo na Lukaku ni mahiri wa kucheka na nyavu zao na hilo Mourhnio kalipa uzito stahili
 
Mtu anafuga mbwa mkali nyumbani na getini anaweka kibao kuwa kuna mbwa mkali hapa pita kwa tahadhari. Watu wote wanaheshimu huo mtaa.
Bahati mbaya mbwa mkali anakufa kwa siri wengi hawajui wanabaki kuogopa bango tu ambalo mwenye mbwa kasahau kulitoa.
Man united ile ya wakati wa akina bathez kurudi nyuma haipo na haiji kuonekana.
Hii Man inayotunguliwa nne hadi na timu za mk donas ni shida. Imebaki story kama ilivyo kwa Liverpool. Man u haina meno kwisha habari yake.
Weka haya maneno rehani khalafu musimu utakapokwisha jipime mwezi wa tano mwakani
 
Rashford ni msimu wake wa pili.

Msimu wa kwanza (2015/16) kacheza mechi 11 kafunga goli 5.

Msimu wa pili (2016/17) kacheza mechi 32 (16 sub) kafunga tena goli 5.

Lukaku kuanzia 2012 yuko juu ya goli 15 kutoa 2014/15 alikuwa na goli 10.
Hizi ndizo takwimu za kuzingatia
 
Bro unaongea kama shabiki wa Mpira anayeujuwa mpira au unataka tujaze Sever tu hapa,any way kwa faida yako na wengine acha tuendelee na mjadala na hivi leo ni sabasaba so we're free.

Mafanikio ya Timu Yeyote yanategemea Vitu Vinne, Moja historia au ukubwa wa timu kiasili sifa hii nadhani timu hizi zote mbili zinazo Liverpool ndio wanaongoza kuchukua UEFA champion Zaidi ya Man U lakini wakifatiwa na Man United lakini katika historia Man United ndio mbabe kwa kuchukua makombe pale EPL,mbili uwezo wa kocha kwa misimu Zaidi ya mitatu tulikosa World class kocha,Moyes hakuwa top cocher duniani wakati anasajiliwa kuja kufundisha Man United,uwezo wa wachezaji binafsi,baada ya Ufalme wa Sir Fegurson ambaye aliweza kuwatengeneza wachazaji wa kuwa kuja kuwa World Class top player,aliopondoka waliomfatia walishindwa kuwa na uwezo huu na kufanya kuona vipaji halisi vya wachezaji wetu, na thamani ya timu katika kuvutia Wawekezaji, kulipa na kununua wachezaji wapya Wenye uwezo,Moyes na Van Gaal hakujuwa ukubwa wa Man United hawajuijuwa thamani halisi ya Man United na ndio mana uliona usajili wa kwanza wa Mou na Wenye thamani ni kumchukua Fellain ambaye hakuwa mchezaji Mkubwa Ulaya.

Van Gaal yeye katika utawala wake aliuza wachezaji wengi wazuri kama Chicharito na kutuletea wapaka Poda wake.

Any way tulikuwa ni kipindi cha Mapito na Mabadiliko now timu ipo kwa kocha mwenye kujuwa Vyote hivi na nzuri Zaidi anajuwa Kiu ya Mashabiki wake.

Bodi ya Man United inakiri kuwa ilifanya makosa makubwa sana kukubali timu kuachiwa Moyes na ndio tulipoanza kuyumba,Van gaal ni top class kocha alitusaidia kutengeneza barabara lakini alipishana na Falsafa ya timu.

Sasa Mou ni mtu sahihi pale Man United anaendana na Falsafa ya timu,ni kocha Mkubwa hivyo anahitaji na timu iwe kubwa na ndio mana aliweza fanya usajili wa uhakika na Mkubwa kurudisha hadhi ya Club Yetu.

Asernal wanakosa baadhi ya Sifa hapo kaka,Asernal sio timu kubwa Ulaya ni timu kubwa England so sio vizuri kuifananisha na Man United,Yes wanafanya vizuri sokoni lakini sio timu yenye kulipa wachezaji mishahara mikubwa sio Wenye kutoa pesa ndefu kwenye usajili.

Asernal imesajili nadhani ni wachezaji wawili top class players kwa misimu miwili ya hivi karibuni lakini sio timu kubwa kuifananisha na Man United na ndio mana wanakosa mbinu za kuchukua makombe.

Nimekwambia tumerudi katika ukubwa wetu au Level Yetu, Man United ni Mabingwa wa Uropa Legue,Kombe kubwa la pili bara ni Ulaya sasa hiyo miaka kumi ipi unayosema.

Kutwaa EPL msimu wa 2017/2018 tusubiri sina shaka na hili,mana hata msimu uliopita zile droo zingebadilika tungeongea mengine.
Subiri hizo droo zibadilike muone mengine maana umeandika kama unapiga ramli. Mambo mengi ni ya kufikirika.
Umejaza maneno mengi ya kufikirika huyo kocha kafukuzwa alikotoka subiri mtamfukuza muda si mrefu.
 
Japo sijawahi changia humu jukwaani ila kwa hili naomba nichangie kidogo kwa ufahamu wangu.

Navyo jua jinsi timu zinavyo sajili wachezaji kwa bei kubwa na mishahara mikubwa hii inapelekea gharama za uendeshaji wa timu kuongezeka. Kwa kuongezeka huko gharama mauzo ya TV rights zitapanda sababu timu ni brand na gharama ya kuendesha hiyo brand imepanda. Kwa hiyo mfano DSTV itabidi alipie gharama kubwa hali itayo pelekea na wao kupandisha bei za huduma. Mwisho wa siku sisi wa kibnda umiza tutakuja kulipia bandani pale. Sasa katika hiyo scenario usiombe na thamani ya pesa yetu ishuke dhid ya dollar.

Kwa hiyo kwa namna moja au nyingine na sisi inatuathiri.

Mkuu kama nakumbuka vizuri, msimu ulioisha timu zote kuanzia Chelsea hadi Sunderland walilipwa Pound Million 98 kama TV rights.
Sasa hapa sijaelewa Sunderland ilikuwaje wakapata mgao sawa na Man Utd wakati wao wana Defoe tu (At least)
 
Back
Top Bottom