Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Screenshot_2017-04-27-08-26-01.png
 
Blind hana mbio akina Aguero na De bruyne watampelekesha sana
Sahihi kabisa,Blind anamapungufu mengi akicheza namba 4,kuliko namba 6,na kwa kuwa Rojo ni majeruhi na hatuna mbadala wake,moja kwa moja Blind anapata nafasi so leo anatakiwa kuwa makini sana hasa kwenye counter attack,City Wana Watu wazuri na wepesi kwenye nafasi za ushambuliaji.

Saa nyingine natamani leo Carrick acheze full back akisaidiana na Baily kama namba 4 wake.

Mbele tukaweka Viungo na washumbuliaji Wenye kasi Zaidi.
 
Chicha kwa mtazamo wangu
kwa mfumo na aina ya mpira na wachezaji/Viungo waliopo pale united kwa sasa,Chicharito atatufaa Zaidi kuliko Griezman.

Nitafurahi Zaidi tukimsajili Chicharito mana tunaenda kutengeneza mchezaji mkubwa Mwingine ambaye vilabu vikubwa vitamgombania kama ulivyokuwa kwa CR7

Ingawa Griezman ni Fundi by nature.
 
Kama mi ndo mou pogba hata angekuwa mzima asingecheza
Mkataba wake unakipengele cha yeye kucheza dakika zote anapokuwa fit na Evaluation yake itafanyika baada ya msimu mmoja.

Hope mwakani asipojituma na kuonyesha thamani yake basi bench litamuhusu kama tutafanya usajili mwingine katika nafasi yake,now hana mbadala ndio mana anakata viuno tu uwanjani.

Pogba ni mchezaji mzuri sana Zaidi tunavyomjuwa,namfatilia toka akiwa kinda United pale na mafanikio yake kule Juve lakini sijajuwa nini tatizo tangu aje United ameshindwa kuonesha kipaji chake halisi.

Ila ni Fundi hasa dimbani hasa akiwa dimba la Juu nyuma ya washambuliaji.
 
tushafungwa mapema tu

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
Haaa haaa haaa humjui Mou, huwa hafungwi mara mbili au tatu mfululizo na kocha mmoja,anamfahamu vizuri sana Gurdiola na anazifahamu mbinu zake,ameshajuwa udhaifu wa Pep kutokuwa na aina ya wachezaji watakaomfanya atumie mifumo yake.

Leo tutawabana Man City vizuri kabisa,sioni Ushindi mkubwa ila Man U anashinda ama Droo.
 
Back
Top Bottom