Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

kwa mwendo huu wa timu yetu ninaoushuhudia tunapocheza na chelsea nimejivunza ya kwamba
  • hatuwawezi chelsea kwa jambo lolote lile,miaka iliyopita nimezoea kuona tunafungwa na chelsea ila tunamiliki mpira sana dhidi yao ila sasa ni tofauti wanatufunga na wanamiliki mpira wao.

  • bado hatujapata dawa ya kumdhibiti hazard na ataendelea kutusumbua kila mechi, wakati wa Alexander Ferguson alikuwa anamuweka Rafael mlinzi wa kulia na valencia namba 7 kidogo ilikuwa tunapata nafuu

  • huu ni msimu wa nne chelsea wana viungo bora kuliko sisi,kutoka utawala wa ramirez,obi,essien,lampard mpaka amekuja matic,fabregas na kante bado wao ni bora kuliko sisi sehemu ya kiungo.

  • juzi nilisema ya kwamba hatuwezi kuwafanya mabeki wa chelsea wakawa hawana amani kwa aina yetu ya washambuliaji, kutoka utawala wa super rooney, berbatov, chicharito, van persie mpaka utawala wa used ibrahimovic, poor rooney, rashford tuna safari ndefu sana ya kuweza kuzifunga timu kubwa kwa ushindi wa uhakika na ndio maana hatujawahi kumfunga mtu bao 5.

  • huu ni msimu wa nne chelsea bado wametengeneza utatu mtakatifu bora unaotusumbua kule mbele kutoka utawala wa mata +oscar+hazard mpaka pedro+moses+hazard+willian lakini sisi mpaka leo wachezaji wetu hawakui kimpira sasa wamekua hawana tofauti na wachezaji wa arsenal.

  • mpaka anapewa kadi nyekundu herrera nafikiri timu yetu ilikuwa haijapiga shoot target hata moja kwa hivyo hii hoja ya kuwa tumefungwa kwa sababu ya herrera ni hoja mbovu tukumbuke tulicheza na bournermouth wakiwa kumi tena uwanjani petu tulishindwa kuwafunga.
kwa mtazamo wangu
  • tunapaswa kuelekeza nguvu zetu kwenye kombe la europe league kuliko kuwania nafasi ya 4, kwa sababu tulishapata nafasi mara mbili ya kuwa katika nafasi ya 4 hadi ya 2 ila tumeshindwa tena katika wakati ambao matokeo ya maadui zetu tulishayafahamu jambo ambalo ni mara chache kuwahi kulishuhudia. sifikirii kwa mwendo huu kama tunaweza kuwa na uhakika wa kuwafunga
chelsea - nyumbani (kwa sababu hatuwezi kuwazidi kimpira)
arsenal - ugenini (labda hawa ndio tunaendana nao kwa aina ya wachezaji wao na uwezo wa kufikiri wa kocha wao)
man city - ugenini (wako vizuri kuliko sisi)
tottenham - ugenini (wana viungo na washambuliaji bora kuliko sisi)
southampton - nyumbani (final walituzidi kimpira)
everton - nyumbani (mechi ya mwanzo walituzidi kimpira tukawa tunajihami kwa dakika 30)
middlesborough-ugenini (mechi ya mwanzo walituzidi kimpira kwa muda mrefu tukapata bao la ushindi dakika za nyongeza)
sunderland - ugenini
burnley - ugenini (tulitoa suluhu uwajani kwetu)

tumebakiza timu 3 ili tuweze kubeba ubingwa wa europe na kupata nafasi ya kushiriki UEFA mwakani


Chelsea ndio timu ambayo imepata matokeo mazuri inapokutana na United kuliko timu nyingine zote kwenye ligi,hii haijaanza leo

Again hata Ferguson alikuwa anapata taabu sana kuwafunga Chelsea nakumbuka ile era ya kwanza ya Mourinho akiwa Chelsea United ilishinda game 1 tu dhidi ya Chelsea ndani ya misimu 3 goli alifunga Fletcher,bado hatujafikia wakati wa kulinganisha timu hii na ile enzi za SAF.Tunapaswa kutengeneza timu ya kupambana na timu zote sio Chelsea peke yake kumbuka Chelsea hajafungwa na Liverpool na still amemzidi point zaidi ya 10 na United imepoteza points dhidi ya Watford,Hull,Everton,WestHam,Bournemouth,Stoke,Burnley,Arsenal

Tatizo kubwa kwenye kiungo tunahitaji defensive midfielder kijana wa kuziba pengo la Carrick acheze na Pogba na Herrera,karibia msimu unaisha Pogba ni mzigo kwenye kukaba anapenda kucheza free timu ikizidiwa hana msaada wowote sometimes ni bora Blind apewe nafasi kucheza kama DM enzi za LVG alicheza vizuri na tatizo kubwa ni timu nzima imekuwa butu kwenye ufungaji magoli ukilinganisha na nafasi tunazotengeneza

Game za mtoano na ligi approach ni tofauti,approach ya jana ilikuwa sawa ukizingatia striker hawakuwepo na ile kadi iliharibu mipango ikabidi Mikhi atolewe

Unasema tuwekeze kwenye Uropa huku kwingine tuachanane nako,nani amekupa guarantee kuwa huku kwenye Europa tutashinda wakati unaamini United haitashinda against Arsenal,Chelsea,Spurs,City,Sunderland,Everton,Mido,Burnley,Southampton
 
Kwahiyo nawe unaona Chelsea nayo ni timu kisa MUFC hajakufunga since 2012.

Timu yako ni ya kawaida sana kama St Etienne
Kama wew yako ilivyo ya kawaida sana ..yani tangu 2012 hujatufunga huoni kama timu yako ni mbovu kuliko laana ya ubaguzi wa rangi dhidi ya Mikel Ob itawatafuna tu; mpaka pale mtakapoenda China kumuomba radhi. Nyambafu!!!!
 
Man Utd midfielder Ander Herrera will be suspended for the next two domestic fixtures after being sent off vs Chelsea.
 
Chelsea ndio timu ambayo imepata matokeo mazuri inapokutana na United kuliko timu nyingine zote kwenye ligi,hii haijaanza leo

Again hata Ferguson alikuwa anapata taabu sana kuwafunga Chelsea nakumbuka ile era ya kwanza ya Mourinho akiwa Chelsea United ilishinda game 1 tu dhidi ya Chelsea ndani ya misimu 3 goli alifunga Fletcher,bado hatujafikia wakati wa kulinganisha timu hii na ile enzi za SAF.Tunapaswa kutengeneza timu ya kupambana na timu zote sio Chelsea peke yake kumbuka Chelsea hajafungwa na Liverpool na still amemzidi point zaidi ya 10 na United imepoteza points dhidi ya Watford,Hull,Everton,WestHam,Bournemouth,Stoke,Burnley,Arsenal

Tatizo kubwa kwenye kiungo tunahitaji defensive midfielder kijana wa kuziba pengo la Carrick acheze na Pogba na Herrera,karibia msimu unaisha Pogba ni mzigo kwenye kukaba anapenda kucheza free timu ikizidiwa hana msaada wowote sometimes ni bora Blind apewe nafasi kucheza kama DM enzi za LVG alicheza vizuri na tatizo kubwa ni timu nzima imekuwa butu kwenye ufungaji magoli ukilinganisha na nafasi tunazotengeneza

Game za mtoano na ligi approach ni tofauti,approach ya jana ilikuwa sawa ukizingatia striker hawakuwepo na ile kadi iliharibu mipango ikabidi Mikhi atolewe

Unasema tuwekeze kwenye Uropa huku kwingine tuachanane nako,nani amekupa guarantee kuwa huku kwenye Europa tutashinda wakati unaamini United haitashinda against Arsenal,Chelsea,Spurs,City,Sunderland,Everton,Mido,Burnley,Southampton
nimependa uchambuzi wako,nimejaribu kutolea mfano wa timu ya chelsea kwa sababu ndio timu yenye uwiano bora kwa wachezaji kuliko timu nyengine tunazo shindana nazo,pia sijamaanisha ya kwamba izo timu hatuwezi kuzifunga tutapokutana nazo ila nimejaribu kukumbushia changamoto tulizokutana nazo katika mechi za kwanza na ndio maana nina wasiwasi na mechi za marejeo hazitakuwa rahisi, kwa nafasi tuliyokuwepo inatupasa tuombee njaa kwa maadui zetu wawili waharibu wote namaanisha arsenal na liverpool jambo ambalo ni gumu kwa nyakati hizi kwa sababu hata wenzetu wanataka kushinda, arsenal ni mabingwa wa kukosa kuchukua taji la uengereza ila ni mabingwa wa kuchukua nafasi ya 4, pia liverpool nao wapo vizuri na hawajapoteza mechi kubwa hata moja na wanapoharibu na sisi tunaharibu na ndio maana nina khofu ya kukosa nafasi ya nne.
tuna mechi dhidi ya arsenal, tottenham, man city, chelsea hizi zote ni top four.
 
nimependa uchambuzi wako,nimejaribu kutolea mfano wa timu ya chelsea kwa sababu ndio timu yenye uwiano bora kwa wachezaji kuliko timu nyengine tunazo shindana nazo,pia sijamaanisha ya kwamba izo timu hatuwezi kuzifunga tutapokutana nazo ila nimejaribu kukumbushia changamoto tulizokutana nazo katika mechi za kwanza na ndio maana nina wasiwasi na mechi za marejeo hazitakuwa rahisi, kwa nafasi tuliyokuwepo inatupasa tuombee njaa kwa maadui zetu wawili waharibu wote namaanisha arsenal na liverpool jambo ambalo ni gumu kwa nyakati hizi kwa sababu hata wenzetu wanataka kushinda, arsenal ni mabingwa wa kukosa kuchukua taji la uengereza ila ni mabingwa wa kuchukua nafasi ya 4, pia liverpool nao wapo vizuri na hawajapoteza mechi kubwa hata moja na wanapoharibu na sisi tunaharibu na ndio maana nina khofu ya kukosa nafasi ya nne.
tuna mechi dhidi ya arsenal, tottenham, man city, chelsea hizi zote ni top four.
Kumbuka United ni moja ya timu iliyocheza mechi nyingi kuliko timu zote, kutolewa kwa FA Cup kutatupa nafasi ya kupigania top four na Uropa kwa ushindani wa EPL so far Chelsea na Spurs tu ndio wana uhakika kuingia top 4 so United,City,Arsenal na Liverpool watagombania nafasi 2 zilizobaki
 
Aisee mchezaji anasifiwa akicheza na mtu tisa walipo kuwa 10 sikumuona huyo kanté
toka kante amesajiliwa na chese amefunga goli 2 na zote amefunga man u kwenye ligi mkiwa 11na kwenye fa mkiwa 10 baada ya kuleta vurugu
vip kuhusu pogba siku mlipocheza na bournmouth wakiwa pungufu huyo pogba alionekana?
 
Man Utd midfielder Ander Herrera will be suspended for the next two domestic fixtures after being sent off vs Chelsea.


Pia Kuhusu Huyu ROJO lolote Laweza Kumtokea iwapo FA watachunguza Coz inaonekana Wazi hapa Kuwa Alimkanyaga Hazard Kwa Makusudi.....
 

Attachments

Back
Top Bottom