Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

1469519154504.jpg
 
Heshima sana wanazi wenzangu wa Man.

Sakata la usajili wa Pogba linaendelea bila kufika mwisho mapema.Nadhani hili laweza kuingiza doa katika maandali ya team hasa tukitilia maani ujio wake waweza kuwa chanzo cha kuondoka wachezaji wengine.

Uhamisho wake sasa umefikia pound 105 huku agent wake akitaka kulipwa pound 25.Man imekubali kulipa 50% Juventus wamegoma kulipa ndururu.Ikiwa manchester watakubali kulipa ada ya agent maana yake gharama za kumnunua Pogba zitafikia pound 130 million ?.

Tatizo langu kubwa ni je tulijiandaa na option B maana naona gharama za kumnunua mchezaji mmoja kwa ada ya pound 130 milion ni kichekesho kikubwa hapo bado mshahara wake na mkataba wa miaka mitano unaweza kufikia pound 65 milion + 130 + bonus.... pound 200 milion ?.

Ni vyema Manchester inaangalia option nyingine kuliko kulazimisha deals ambayo inaweza kuvuruga mipango ya team.
 
Kama ningekuwa Mourhino ningemsajili Blaise Matuidi ambaye cost yake si zaidi ya pound 30 milion na bado angeleta uhai katika kiungo badala ya kutumia 130 milion.
 
Naona hata Tony akija*ba msaga sumu wewe utatutaarifu....hicho kigazeti cha udaku na chenye mlengo wa kipopulist kama alivyo mtukufu rais JPM, hata kuchamb*a hakifai

ebana serikali ya mtukufu wanzuki ipo ipo kama wapenzi wa Manchester United mlivyo.
 
Kama ningekuwa Mourhino ningemsajili Blaise Matuidi ambaye cost yake si zaidi ya pound 30 milion na bado angeleta uhai katika kiungo badala ya kutumia 130 milion.

Mkuu unajua staili ya Mourinho if it is not very expensive then it is not good/worth. Jamaa atakuwa ni mzaramo (no pun intended) wa kireno anayeamini ponda mali kufa kwaja. Anapenda timu zenye pesa kama wademu wa Kihaya, kichagga (Pund intended or not) au kipare, wanavyopenda wanaume wenye pesa
 
Kama ningekuwa Mourhino ningemsajili Blaise Matuidi ambaye cost yake si zaidi ya pound 30 milion na bado angeleta uhai katika kiungo badala ya kutumia 130 milion.
Na bado hiyo ni ndogo mkuu,Juve hawataki kuinclude commission ya agent,hivyo Man u wakikubali ina maana ngoma itagonga 140!
Na Juve wanamfukuzia huyo huyo Matuidi baada ya hapo.
 
Hahaha kwa hiyo hata alivyounfollower timu katika Twitter na Instagram ni uongo? Wapenzi wa Manchester United na wengine wanaliongelea hilo mitandaoni. Najua Metro ni la bure hata mitaa hii lakini sio pekee lililoongelea hilo, angalia express.co.uk nao wamepost hii issue. Bbc gossip wanapost vitu toka magazeti mbalimbali na social media za watu maarufu pia wana verify kabla ya ku-quote. Unajua jambo linapokuwa ni positive kwa timu wapenzi wanalikubali hata kama limetoka mdomoni mwa bubu likiwa negative linapingwa.

Achana na mambo ya United. Ongeza juhudi mshauri Wenger asajili watu wa maana sio kina Takuma.
 
Baada ya misimu miwili Manure watashuka daraja. Hawajajifunza kwa Chelshit bado. Mouthrinho sio wa kuamini kabisa for long term investment. Atakupa vikombe kadhaa, then anakurudisha unakostahili
 
Back
Top Bottom