Heshima sana wanazi wa Manchester United.
Mechi ya jana yapo mambo matatu niliyoyaona ambayo kama LVG atapenda kuyafanyia kazi hakika nafasi ya kwanza au ya pili inatuhusu.
Mosi, Viungo Michael Carrick 34 na Bastian Schweinsteger 31 ni wachezaji wakubwa kwa umri si busara kuwapanga wote katika mechi moja.Kama ulitazama game vizuri bila kengeza la ushabiki Carrick na Bastian walizidiwa na wachezaji vijana Francis Coquelin,Alexis Sanchez na Santi Cazorla ambao walikuwa wameshika kiungo haswa huku viungo wa Manchester United wakipeleka pass taratibu sana ungedhani hawana haja ya ushindi.
Pili,Ni wakati muafaka sasa LVG akamweka bench Rooney na Depay.Kwa kweli Rooney kiwango chake kimezidi kushuka siku hadi siku mara nyingi awapo uwanjani timu inakuwa inacheza kama na wachezaji kumi uwanjani.hana mbio,hana uwezo wa kumiliki mipira,hana msaada timu inaposhambuliwa hana uwezo wa kufunga mabao kama zamani.
Tatu,Ni muda muafaka sasa LVG akamchezesha Ander Herrera nafasi ya Rooney anaweza kuisaidia timu zaidi ukimlinganisha na Rooney anayevuta mshahara mkubwa lakini hana mchango wa maana kama Anthony Martial ambaye alikuwa mchezaji pekee alionysha kiwango cha juu katika mchezo na Arsenal.