Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mchizi boti unayumba, mwanaume akimbii majukumu, kuwa shabiki la manyumbu ni jukumu lako hivyo usikimbie,, hahaha hili timu ndio ulilipenda hivyo kifa naloo haha mchizz botiiiiii
Timu ni mbovu kwa sasa na hata suruhu ya hilo tatizo haijulikani.
Tushabadili Makocha, wachezaji mpaka benchi la ufundi na uongozi kwa ujumla, lakini ngoma ngumu.

Kwakua sina uvumilivu ndio maana siangalii mezi za timu yangu.
Ila mimi ni United mwanzo mwisho.
 
Sesko nje
IMG_8383.jpeg
 
Maguire pamoja na kejeli zote alizowahi na anazoendelea kuzipata,ameendelea kuipambania timu yake na kuipa heshima iliyoikosa kwa muda mrefu. Mwenye kukumbuka atajua ni mara ya mwisho lini manU kuifunga liva nyumbani.
Maguire anatufundisha kutojidharau,hata kama dunia nzima itatukataa, kila mtu ana upekee wake.
 
Licha ya kwamba tuna mengi ya kuboresha, positively tumekomaa na tumeondoka na ushindi, hiki ni kitu muhimu Sana Kwasasa kwenye hii timu yote, hii itaongeza kujiamini.

Ningeshangaa Sesko angeanza Leo, wangetuvuruga vibaya pale katikati. Mount ni mchezaji very flexible changamoto Yake ni majeruhi na kukata Moto baadae, Jamaa anatusaidia Sana.

Kusema kweli Kila timu imekosa nafasi za wazi, ninachokiona kuna wachezaji bado kama vile wanakuja halafu wanakataa...
 
Eneo la goalkeeper tayari ni kama tumepata afadhali.

Kocha apate LWB na RWB hao kina dorgu Bado hawawezi kumpa anachokitaka kweny mfumo wake.

Kiungo tuboreshe msimu ujao tusimtegemee casemiro Wala Bruno, maino kocha amtafutie nafasi.
Tusajili na winger Moja.

Msimu huu tunaweza kumaliza top four Kwa sababu kikosi na kocha wote Wana growth and improvement rate pia tutasajili kiungo na LWB dirisha dogo la January.

Leo ni furaha, lakini nmegundua mfumo wetu Kwa msimu huu ambao Bado hatupo imara Bora tuwe tunacheza kama second team, mpizani tumuue Kwa quick counter attack na long balls
 
Back
Top Bottom